Pages

Translate

Saturday 8 February 2014

WATANZANIA WAKOSA USTAARABU UWANJA WA TAIFA DAR



Pichani juu ni baadhi ya wadau wa Soka waliokutwa hivi karibuni wakijisaidia kwenye masinki ya kunawia mikono kama waonekanavyo pichani.
Hapa baada ya kumaliza shughuli yao haoo wakaondoka,je wahusika wanalichukuliaje jambo hili lisilo la kiungwana kabisa ndani ya uwanja wa wetu wa mpira,ambao umejengwa kwa gharama kubwa,lakini kuna baadhi ya watu kama hawa wamekuwa wakiharibu maeneo na vifaa mbalimbali ya uwanja huo ikiwemo na kugeuza matumizi yake.

KIJANA AKUTWA AMEJINYONGA KISA UGMU WA MAISHA





nyongaKijana huyu aliyetambulika kwa jina moja la Bahati ambaye alikuwa akijishughulisha na uuzaji wa mifuko ya plastiki maarufu kama rambo amekutwa akiwa amekufa baada ya kujinyonga juu ya mti jirani na ufukwe huko mjini Bukoba mkoani Kagera.
U fukwe huo ambao upo jirani kabisa na stand ya mabasi ya mkoani humo na marehemu alionekana akifua nguo zake na ndipo baadae kisa kikawa mkasa kijana huyu akafikwa na haya yaliyomfika.
Mwili wa marehemu umepelekwa hospitali kwa kuhifadhiwa kwa ajili ya utambuzi na utaratibu mwingine kuendelea.

Waandishi na mashuhuda wakishuhudia tukio
Mwili wa marehemu ukiwa umeshushwa tayali kwa safari ya hospitali

Wednesday 5 February 2014

KONDO WA YANGA AONJA SELO BAADA YA KUINGIA ANJANI BILA KITAMBULISHO

 







MSHAMBULIAJI Shaaban Kondo wa Yanga amejiunga na kikosi hicho juzi baada yakuaachiwa huru kutokana na kosa la kuingia uwanjani bila kitambulisho wala jezi kitu kilichopelekea polisi waliokuwa dolia kumshikilia wakizani ni kibaka.

KIINGEREZA NI ISHU KWA WABUNGE WENGI TZ: LISU

 Mbunge wa Singida Mashariki, mnadhimu wa upinzani na mwanasheria mkuu wa CHADEMA mh. Tundu Lissu, amesema kuwa wabunge wengi wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania hawajui lugha ya kiingereza kitendo kinachowafanya wakose ufanisi katika kazi zao za kibunge hususani mijadala mbalimbali bungeni na nje ya bunge. 

Mwanasheria huyo amekiita kitendo hicho kuwa ni janga la taifa ambapo ameshauri suala hilo litazamwe upya ili tuwe na wabunge wanaoweza kuwa tija kwa taifa.

Ikumbukwe kuwa wabunge wengi wa bunge hili wamekuwa wakituhumiwa kuwa na elimu za kidato cha nne (iv) au chini ya hapo na wengine kidato cha sita chenye matokeo mabaya.

Tuesday 4 February 2014

MAINDA AONYESHA MSIMAMO KATIKA KUOKOKA

Msanii wa Filamu Bongo,Ruth Suka 'Mainda', akiwa Hospitali na mmoja wa wauguzi wa hospitali hiyo ambayo jina lake hakutaka kulitaja mara moja. 
SOMA UJUMBE ALIOUANDIKA KWA MKONO WAKE HAPO CHINI...

maindasmallbabyTrowback.......imebaki historia tu......maana magonjwa sasa hayana nafasi kwangu....nimejua kwa kupigwa kwake Yesu mimi nilishaponywa kitambo. Asante yesu kwa kuchukua udhaifu wangu,magonjwa yangu,unyonge wangu...na Umenipa Tumaini maisha yangu yote acha nikutumikie ipasavyo.japo najua nitakutana na vikwazo ila nitashinda coz wewe ulishafanya njia siku nyingi.mapambano yanaendelea huku nikizidi kukukili wewe Yesu kuwa ndie Bwana na Mwamba wangu....EMMANUEL:GOD with US.........

WAPINZANI WAKIWA PAMOJA WATAFANIKIWA KUING'OA CCM: MSEKWA

 Kiongozi Mstaafu wa CCM, Pius Msekwa amesema endapo vyama vya upinzani vikiungana na kuweka mikakati makini ya muda mrefu, vinaweza kuking’oa CCM madarakani.

Akizungumza kwenye mahojiano maalumu na mwandishi wetu jana, Msekwa alisema kwa mtindo wa sasa wa vyama vya upinzani kila kimoja kusimama peke itakuwa ndoto kukishinda CCM.

“Kama vyama vya upinzani vinataka kuwe na upinzani wenye nguvu dhidi ya CCM ni lazima viungane vyote. Tena viweke mikakakati ya muda mrefu ya kujiimarisha,” alisema Msekwa kwenye mahojiano hayo.

Hata hivyo, alisema kuiondoa CCM madarakani siyo kazi rahisi kwa sababu mizizi yake imeenea kila kona ya nchi huku akisema wazo la upinzani kuungana halitakuwa rahisi kwa kuwa wengi wao ni walafi wa madaraka na hakuna atakayekuwa tayari kuvunja chama chake na kuunda kimoja kwa hofu ya kukosa uongozi.

Akijibu swali kuhusu nguvu ya Chadema kwa sasa Msekwa alisema: “Wanapambana na CCM kwenye majukwaa ya kisiasa lakini si kuwa na watu wengi wanaokiunga mkono.”

Alisema CCM kina mizizi hadi ngazi za chini kabisa nchi nzima tofauti na vyama vingine.

Alisema Chadema kiko katika baadhi ya maeneo ya Tanzania Bara wakati Zanzibar hakina nafasi, tofauti na CUF ambacho alisema angalau kinaonyesha kuwa na nguvu visiwani huko.

Kuhusu Chadema kuwa na wabunge wengi Tanzania Bara, Msekwa alisema ni neema iliyokiangukia baada ya CCM kufanya makosa ya uteuzi kwa baadhi ya majimbo.

Msekwa ambaye aliwahi kuwa Spika wa Bunge alisema pamoja na neema hiyo, Chadema hakiwezi kufikia asilimia 40 ya wabunge wote.

“Kweli Chadema kimejitahidi lakini ukichunguza utabaini ni neema iliyowaangukia kutokana na makosa ya CCM kuteua watu ambao wapigakura walikuwa hawawataki,” alisema Msekwa.

Alisema Chadema kimekuwa kikionekana kufanya vizuri kwenye siasa za majukwaani kwa sababu kina nafasi kubwa ya kukosoa na hata kutoa madai ya kutunga dhidi ya CCM ili mradi yawe yanawagusa wananchi.

Kuhusu uwezekano wa vyama vya upinzani kuchukua nchi kutokana na CCM kuwa na makundi mengi ambayo yanaweza kukisambaratisha katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 Msekwa alisema: “Hakuna mtu anayeweza kuondoka CCM na kuivunja nguvu. Hata akiwa ni kiongozi mwenye nguvu ya kisiasa kiasi gani

ATEMBEZWA UCHI BAADA YA FUMANIZI

afumaniwa

Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Hussein Shaban(35) amefumaniwa katika nyumba ya kiongozi mmoja wa Chama cha Mapinduzi (CCM) huko Tegeta jijini Dar es Salaam. 


Kisa hichohilo kilitokea kitongoji cha Nyeishozi, Tegeta kwa kumuhusisha Hussein ambaye ni mfanyabiashara na mke wa kigogo huyo ambaye jina lake tunalihifadhi.
Baada ya kukamatwa ugoni mwanaume huyo inadaiwa kuwa watu wenye hasira kali walimvua nguo na kumtembeza uchi

MBOWE AMSHUTUMU RAISI JK

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amemvaa Rais Jakaya Kikwete, akimtaka kuacha kutafuta huruma ya Watanzania juu ya suala la Katiba na badala yake atumie nafasi hiyo kuwataka wabunge wake kuheshimu maoni ya wananchi.


Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alisema kuwa hotuba ya Rais Kikwete juzi kwamba Katiba haiwezi kupatikana kwa ngumi imejaa upotoshaji kwa wananchi.

Katika hotuba yake ya maadhimisho ya miaka 37 ya kuzaliwa kwa CCM, yaliyofanyika mkoani Mbeya, Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, alimshangaa Mbowe kwa kauli yake kwamba mfumo wa serikali tatu ukikataliwa katika Bunge hilo nchi haitatawalika.

“Huku ni kuwadanganya wananchi, pale hakuna ngumi wala vurugu yoyote, kila ibara iliyopo katika rasimu itajadiliwa ili upatikane mwafaka. Huku ni kukosa ukomavu wa kisiasa,” alisema.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mbowe alisema ni vema Rais Kikwete akaacha kuhangaika na wapinzani, badala yake awe tayari kuheshimu mawazo ya wananchi waliyotoa wakati wa kutoa maoni ya Katiba.

Mbowe alisema kuwa Rais Kikwete ni mwanasiasa na mtu anayejaribu kupotosha hoja, kwani CHADEMA waliposema watapambana, hawakumaanisha kupigana ngumi kama alivyosema kiongozi huyo.

Alisema kuwa viongozi wa CCM wamekuwa wakilazimisha ajenda ya Katiba mpya kuonekana kama sera yao, jambo ambalo CHADEMA haiwezi kuafiki.

“Katiba ni ya wananchi, si ya chama chochote cha siasa, ndiyo maana hatukubali kuona mawazo ya wananchi yakishindwa kuheshimiwa,” alisema.

Mwenyekiti huyo alisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba imefanya kazi nzuri ambapo Rais Kikwete na wabunge wake wanapaswa kuheshimu mchango huo.

Alisema kuwa CHADEMA itahakikisha inashindana kwa hoja katika Bunge la Katiba litakaloketi hivi karibuni na iwapo hilo litashindikana watarudi kwa wananchi ambao ndio wenye uamuzi wa mwisho juu ya suala hilo.

“Wajumbe watakaoshiriki Bunge la Katiba ni 640 ambao hao si waamuzi wa mwisho na kama tutaona kuna suala lolote linaloenda kinyume, sisi tutakachokifanya ni kurudi kwa wananchi kuwaeleza juu ya kilichotokea na hao ndio wenye maamuzi ya mwisho katika kura ya maoni,” alisema.

Mbowe alisema kuwa hata katika kushindana kwa hoja CCM wanapaswa wasiweke hila, maana wataweza kuchangia mchakato huo kushindwa kufanikiwa.

Alisema kuwa nia ya CHADEMA ni kuhakikisha Katiba nzuri, bora na iliyo ya wananchi inapatikana na si kusababisha vurugu kama ambavyo Rais Kikwete amejaribu kupotosha.

“Hila hiyo imeonekana wazi maana kuna hali ya kutaka kupuuza mawazo ya wananchi na CCM kulazimisha mawazo yao, hilo hatutalikubali na tutapambana…hiyo si mara ya kwanza kupambana katika suala hilo,” alisema.

Mbowe alisema kuwa kuhusu serikali tatu ni muhimu Rais Kikwete akaheshimu mawazo hayo na CHADEMA itashindana kwa hoja juu ya suala hilo ili kuhakikisha mawazo hayo yaliyowasilishwa na Jaji Warioba yanaheshimiwa.

Katika ziara ya mikutano ya hadhara ya CHADEMA iliyopewa jina la Operesheni M4C Pamoja Daima, Mbowe na viongozi wengine waliionya Serikali ya CCM kutochakachua mchakato wa Katiba, kwani Watanzania hawako tayari kurudi kwenye Katiba ya sasa ambayo alidai imekosa uhalali wa kuongoza nchi.

Alisema CCM kwa kutumia wabunge wake wakiamua kuhujumu mchakato huo bungeni, yeye na viongozi wenzake watapita nchi nzima kuwataka wananchi wasishiriki kura za maoni na yuko tayari kufunguliwa kesi kwa kudai Katiba

MTU MMOJA AJERUHIWA NA MAMBA HADI KUFA JIJINI TANGA




Baadhi ya wanakijiji wa Korogwe wakiushangaa mwili wa mtu huyo ambaye jina lake halikuweza kutambulika kwa haraka.


MCHUNGAJI MTIKILA ANUSULIKA KUUWAWA

 

Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila akionyesha picha za X-Ray alizopigwa baada ya kupewa kipigo na watu wanaodaiwa kuwa ni wakazi wa Kurasini alipokwenda kuwahamisha Ijumaa iliyopita.


Dar es Salaam. Kiongozi wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila amenusurika kifo na mtu mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Mikidadi, ambaye yupo mahututi katika Hospitali ya Temeke,  baada ya kushambuliwa na watu wanaodaiwa kuwa na mzozo wa ardhi eneo la Kurasini, jijini Dar es Salaam.
 
Mchungaji Mtikila alikumbwa na mkasa huo Ijumaa wiki iliyopita baada ya kufika katika eneo hilo kwa nia ya kutaka kuwaondoa watu hao wa familia tatu tofauti ambao wanaishi katika eneo hilo.
 
Kipigo hicho ambacho kimemsababishia majeraha ya kisogoni na hata kushonwa nyuzi tatu kichwani, kuvimba usoni na maumivu makali mwilini yalitokana na kipigo kutoka kwa familia mbili tofauti zinazoishi katika eneo hilo ambao wanapinga kuhama.
 
Pia katika sakata hilo, Mtikila anadai kupoteza simu mbili, pesa taslimu Sh400,000 na Dola za Marekani 2,000 na siku ya tukio na alifika hapo akiwa ameongozana na watendaji wa Dawati la Msaada wa Kisheria katika taasisi yake ya Liberty Fund International.
 
Kamanda wa Polisi Temeke, Engbert Kiondo alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa wanalifanyia uchunguzi na taarifa kamili itatolewa kesho Jumanne.
 
“Ni kweli suala hilo limeripotiwa hapa na tunalifanyia uchunguzi na kesho Jumanne nitatoa taarifa rasmi kwa waandishi wa habari,” alisema Kiondo.
 
Mtikila alisema, mara baada ya kufika eneo hilo, alikwenda katika nyumba ya kwanza  na kuwakuta walinzi ambao walikubali na kuondoka katika eneo hilo kwani tayari notisi walikuwa nayo na walikuwa wanatambua kuwa wanatakiwa kuondoka.Alisema baadaye walikwenda katika nyumba ya pili ambayo anaishi mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Rubein Sanga ambaye hata hivyo vitu vyake vingi akuwa amekwisha vihamisha.
 
Alisema wakiwa mbele ya nyumba hiyo gari la polisi lilifika na wakiwa hawana hili wala lile vijana ambao anawataja kuwa ni wa Sanga walianza kuwashambulia kwa kutumia nondo na kila aina ya silaha za jadi.
 
“Walinipiga sana hadi nikapoteza fahamu na wakawa wanasema huyo Mtikila bebeni na mumchome moto, walitaka kuniua kwani walinikwida tai hadi ikakatika,” alisema.
 
Na kuitaja pia familia ya Evelyne Mboya kuwa ilishiriki kuwashambulia. Alisema wakati vurugu zinaendelea, ndipo akatokea mmoja wa jirani wanaoishi katika eneo hilo aliyemtaja kwa jina la Mikidaki: “Yule bwana alipojaribu kunitetea kuwa nisiendelee kupigwa alipigwa nondo kichwani na akaanguka na alishambuliwa hadi kuzirai na hajapata fahamu hadi leo,” alisema.
 
Mchungaji Mtikila alisema alikuwa ameambatana pia na walinzi wawili (mabaunsa), wafanyakazi wa dawati lake la msaada wa kisheria lililopo chini ya taasisi yake ya Liberty Fund International na mmiliki halali wa eneo hilo, Omar Salum Muhsin ambaye pia alijeruhiwa mkononi kwa nondo.
 
Mtikila aliwataja wafanyakazi wake waliojeruhiwa kuwa ni Hemed Wendo na Gray Mhando na akiwa amezirai alibebwa na kupandishwa katika gari hadi Kituo cha Polisi Chang’ombe ambako yeye na wenzake walifunguliwa jalada kwa shtaka la kuingia isivyo halali katika eneo la watu wengine.

Sunday 2 February 2014

CCM YAAMUA KUSOMBA BONGO MOVIE WAKATI CHADEMA IKILA SHAVU KWA WANAMUZIKI

WASANII MAARUFU NCHINI   JB,IRENE UWOYA,BANANA ZORO,RICHIE,MBOTO,WASTARA NA JOHARI WAJIUNGA NA CCM WAPEWA KADI NA RAIS KIKWETE JIJINI MBEYA KWENYE SHEREHE ZA MIAKA 37 YA CCM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEieCQpy6l7t-skVrdKQKWOrzl7vj-IUUWfT568CW9bLbxBYk98lX7_tMhqiXfk0qlUTJMMD4Y5h14gVrjhdQB747cjaTKuYKJhzBVMcvik77XsV1aUklLQuXSEVTZzoW6ddKJh9gky92lNm/s1600/1Afande+Sele+Morogoro.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEieCQpy6l7t-skVrdKQKWOrzl7vj-IUUWfT568CW9bLbxBYk98lX7_tMhqiXfk0qlUTJMMD4Y5h14gVrjhdQB747cjaTKuYKJhzBVMcvik77XsV1aUklLQuXSEVTZzoW6ddKJh9gky92lNm/s1600/1Afande+Sele+Morogoro.jpg
WATOTO WA MJINI WANASEMA KAMA UMESHINDWA KUWA SHABIKI WA GAME NYINGINE HATA HUU NI MCHEZO MZURI WAWEZA KUSHABIKIA TUU HALAFU TUONE MWISHO WA GAMU NINI KINATOKEA

SLAA AZILILIA HELA ZA BENKI YA DUNIA

  Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amedai kuwa  baadhi ya viongozi wa Serikali wamegawana na kutafuna fedha zilitolewa na Benki ya Dunia, ili kugharimia miradi ya kuchimba visima 10  vya maji katika kila wilaya nchini.

Dk Slaa alitoa tuhuma hizo juzi jioni, alipokuwa akihutibia mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mkendo, mjini  Musoma.

Kiongozi huyo wa Chadema yuko katika Operesheni ya M4C Pamoja Daima.

Alisema kitendo hicho kinafanywa wakati Watanzania na hasa wanawake wakikabiliwa tatizo kubwa la kukosa huduma za maji kiasi cha kushinda hata kwa siku tatu bila kuoga.

“Ngoja niwaambie hivi sasa Serikali imekuwa ikiweka vikwazo vingi katika utekelezaji wa mradi wa maji kupitia Benki ya Dunia, ukweli ni kwamba fedha zote zilizotolewa zimeliwa sasa wameanza kuhaha wasijue cha kufanya,” alisema na kuongeza.

Wakati huohuo, Geofrey Nyang’oro na Raymond Kaminyonge wanaripoti kutoka Iringa kuwa viongozi wa Chadema Taifa wakiongozwa na mwenyekiti wake, Freeman Mbowe wamekamatwa na polisi mkoani hapa na kushikiliwa kwa muda wakituhumiwa kuzidisha muda katika mikutano waliyoifanya katika Jimbo la Kalenga wilayani hapa juzi.

Mbowe alikuwa ameambatana na viongozi wa chama hicho juzi, walifanya mikutano mbalimbali mkoani hapa, ambapo katika Jimbo la Kalenga walifanya mikutano katika Vijiji vya Wassa,Nzihi, Kidamali na kisha kushindwa kufanya mkutano mmoja uliotakiwa kufanyika katika Kijiji cha Mgama kwa madai muda ulikuwa umekishwa.

Mwenyekiti huyo pamoja na viongozi wawili wa Chadema, Mbunge Peter Msigwa na Halima Mdee walikamatwa saa tatu asubuhi wakati mwenyekiti huyo alipokuwa akijiaandaa kuondoka mkoani humo kwenda mkoani Pwani kuendelea na mikutano ya Operesheni M4C pamoja Daima inayoendelea kwa sasa kote nchini. Hii ni mara ya pili kwa kiongozi huyo kukamatwa na kuhojiwa  ambapo mara ya kwanza ilikuwa Agosti 25 mwaka jana.

KWA SUPOTI YAKO NDOTO YA TAJI LA MISS WORLD KUJA TANZANIA YAWEZEKANA


Hey guys. At Miss World, contestants usually need as much support as they  can get. I would therefore like to ask for your help in spreading the  word to your fellow fans, friends, family, acquaintances etc. about the  representative for Tanzania this year; Happiness Watimanywa.

People around the world can help me make an even bigger impact through social media and I would like you to be informed of my journey from as early as now.

Please follow: @misstanzania2013 on Instagram
@misstz2013 on twitter   And Like Miss World-Tanzania on Facebook
Thanks for the support. Happy

HILI NDILO GARI LILILOUA ASKALI WA 5 DODOMA JANA



Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma.

Askari polisi watano mkoani dodoma wafariki dunia papohapo katika ajali ya gari iliyotokea 31/01/2014 majira ya 23.45 hrs katika barabara kuu ya Dodoma – Morogoro eneo la Mtumba Center, Kata ya Mtumba Tarafa ya Kikombo Manispaa ya Dodoma, ambapo gari namba T.770 ABT Toyota Corolla lililokuwa likiendeshwa na Askari namba H. 3783 PC DEOGRATIUS wa Polisi Wilaya ya Kongwa likitokea Dodoma mjini likielekea Wilayani Kongwa liligongana uso kwa uso na gari namba T.997AVW Scania Bus mali ya Kampuni ya Mohamed Trans lililokuwa likiendeshwa na JUMA s/o MOHAMED, miaka 38, Mkazi wa Mwanza, likitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma na kusababisha vifo kwa askari watano papohapo. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME amewataja Askari hao waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni:-
1.          D.9084 D/CPL. ADOLF S/O MESHACK SILLA mwenye miaka 51, Mgogo.
2.          F.6459 D/C. EVARIST s/o MOSES BUKOMBE mwenye miaka 34, Muha.
3.          H.3783 PC. DEOGRATIUS s/o PATRICK MAHINYILA mwenyw miaka 29, Mgogo.
4.          WP.10337 PC. JACKLINE d/o AUGUSTINE TESHA mwenye miaka 22, Mchaga.
5.          WP.10382 PC. JEMA d/o JIMMY LUVINGA mwenye miaka 20, Mhehe. 
Wote ni askari Polisi Wilaya ya Kongwa na hakuna abiria aliyeumia katika basi.

Kamanda MISIME amesema chanzo cha ajali hiyo kulingana na uchunguzi wa awali ni mwendo kasi kutokana na uharibifu uliotokea kwa gari dogo walilokuwa wamepanda askari na jinsi lilivyoburuzwa na basi kwa umbali wa mita 56 kisha kwenda kusimama umbali wa mita 97, kwa hali hiyo umbali kutoka eneo walipogongana hadi basi liliipoenda kusimama ni mita 152. Dereva wa Bus alitoroka mara baada ya ajali hiyo kutokea, juhudi za kumtafuta zinaendelea. Miili ya maerehemu imehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya mkoa Dodoma.

Aidha Kamanda MISIME ametoawito kwa madereva kila mara wawe na udereva wa tahadhari na na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

KANISA LAUZA SAKRAMENTI SH 10,000, WAUMINI WALALAMIKA

WAUMINI wa Kanisa la Break Through Assemblies lililoko eneo la Boko Magengeni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam linadaiwa kuuza Sakramenti kwa Sh 100,000 kwa kila muumini.
Hatua hiyo inadaiwa kuwanyima wasio na fedha chakula hicho cha Bwana hivyo kusababisha malalamiko dhidi ya uongozi wa Kanisa hilo la Walokole.

Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili, zilisema tukio hilo lililoshangaza waumini lilitokea Januari 19. Kanisa hilo linaongozwa na Mchungaji Godfrey Simtomvu.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, na kwa masharti ya kutotajwa majina, waumini walisema kitendo hicho kiliwashangaza siku hiyo kanisani hapo walikokuwa wamekwenda kwa ajili ya Ibada kama siku zingine.

Akisimulia, mmoja wao alisema baada ya Mchungaji kuhubiri, vililetwa vikombe na mikate ambayo hutumiwa kanisani kama ishara ya kushiriki pamoja Chakula cha Bwana. Makanisa mengine hutambua ibada hiyo kama ya Sakramenti ya Chakula cha Bwana.

“Baada ya vifaa hivyo kufika kanisani hapo vilionekana kuwa vichache tofauti na waumini waliokuwa kanisani hapo…ndipo Mchungaji alipopaza sauti kuwa mwenye Sh 100,000 na zaidi ndiye atakayeshiriki,” alisema na kuongeza kuwa Januari 26, alishindwa kuabudu kutokana na kitendo hicho.

Alisema baada ya kutamka hivyo, waumini wengi walinywea wakashindwa kusogea na kupisha watu wapatao 10; lakini baada ya kuona idadi imekuwa ndogo zaidi ikatangazwa kuwa hata wenye Sh 50,000 wanaweza kusogea mbele kushiriki.

Aliongeza kuwa wakati wote huo waumini walikuwa wakitazamana, wakijiuliza juu ya utaratibu huo mpya, jambo ambalo ni kinyume na ilivyokuwa awali kanisani.

Alisema Mchungaji baada ya kuona idadi ya waumini inazidi kupungua, akawatangazia kuwa wasiokuwa na fedha wajiandikishe kisha wapokee chakula hicho kisha na kesho yake wapeleke kiwango hicho cha fedha. Muumini mwingine alisema jambo lililoshangaza wengi ni utaratibu huo mpya ambao awali haukuwapo kwani walikuwa wakitangaziwa wiki moja kabla na kutakiwa kujitayarisha kwa ajili ya ibada hiyo ya Chakula cha Bwana.

“Awali Mchungaji alikuwa akitupa taarifa wiki moja kabla, akiwataka waumini kujitayarisha na kusafisha nyoyo zao kabla ya kushiriki kitendo hicho ambacho tuliamini kuwa ni kitakatifu na chenye mafundisho makubwa kwa waumini,” alisema na kuongeza kuwa hilo la kununua chakula lilizuka ghafla na hakujua hatma yake.

Mwingine alisema mbali na kununua chakula hicho, pia jambo lililozusha mshangao kwa waumini ni Mchungaji huyo kuleta watu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuhubiri Neno la Mungu akidai kuwa ni wahubiri ambao nao husisitiza neno la kutoa tu.

“Waumini tunaamini kuwa Bwana Yesu alitoa chakula hicho bure…iweje leo waumini wauziwe tena kwa kupangiwa kiwango?” Alihoji.

Akizungumzia madai hayo, Mzee wa Kanisa hilo alisisitiza kuwa yeye si msemaji wa Kanisa hilo na kusema madai hayo hayana ukweli na kwamba siku hiyo, Mchungaji hakumaanisha kwamba utakuwa utaratibu, bali ilikuwa ni kuhamasisha utoaji kwa muumini mwenye nacho. Alisema kufanya hivyo halikuwa lengo la kutafuta fedha bali kupeleka Neno la Mungu mbele.

“Msemaji wa Kanisa ni Mchungaji mwenyewe, ukiniuliza sana mimi utakuwa unanionea, kama unamtafuta na ukamkosa atakuwa redioni katika kipindi,” alisema mzee huyo.

Akizungumzia malalamiko hayo, Mchungaji Simtomvu alisema kutokea kwa hali hiyo si imani ya Kanisa hilo bali ilitokana na mhubiri kutoka Kongo ambaye alifunuliwa na Mungu na kutaka waumini kuweka maagano yao na Mungu kwa mwaka huu.

Alisema hayo yalikuwa mafunuo ya mtu na si imani na ni kitu ambacho hutokea mara moja tu na kutolea mfano wa yai linapouzwa kwenye mnada kwa bei kubwa, ingawa bei yake halisi inajulikana.

“Laiti ningemfahamu aliyeleta taarifa hiyo ningemsaidia, kwani amekengeuka, mbona Mchungaji TB Joshua wa Nigeria huuza maji katika vichupa vidogo kwa gharama kubwa inayoweza kufikia Sh 75,000,” alisema Mchungaji Simtomvu.

Alisema tukio hilo ilikuwa ni kwa muumini anayetaka kuweka agano na Mungu wake, kwamba mwaka huu amtendee mambo gani na kuhoji kuwa zipo imani za ajabu ajabu lakini haziripotiwi.HABARILEO

Saturday 1 February 2014

KIKONGWE AFUMWA CHUMBANI KWA MTU AKIWA UCHI

Mashuhuda wa mwanzo wanadai walimkuta bibi huyo akitapatapa bila kujua nini la kufanya huku akiwa mtupu na nguo zake zikiwa pembeni kitendo kilichotafsiriwa kwamba pengine bibi huyo anaweza kuwa mchawi,huku wengine wakisubiri taarifa ya polisi na wengine wakisema huenda bibi huyo alipatwa na matamanio ya kimwili.
Hili ni tukio lilitokea huko Bukoba ambalo linamhusisha Kikongwe mmoja ambaye jina lake bado halijapatikana kukutwa chumbani kwa mtu huku akiwa mtupu chumbani kwa mtu.
25Mpaka sasa bado haijajulikana kama ni Kigarura au pengine alipata matamani ya mwili akaona pengine chumba kile kingemfaa kumpatia msaada wa mambo yake.
28Bibi Kizee huyo anakadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 70,ambapo amekamatwa alfajiri ya leo January 31 hata hivyo polisi wamefanikiwa kumnusuru na kifo baada ya kumchukua na kumpeleka kituo cha polisi.
30Mashuhuda wa mwanzo wanadai walimkuta bibi huyo akitapatapa bila kujua nini la kufanya huku akiwa mtupu na nguo zake zikiwa pembeni kitendo kilichotafsiriwa kwamba pengine bibi huyo anaweza kuwa mchawi,huku wengine wakisubiri taarifa ya polisi na wengine wakisema huenda bibi huyo alipatwa na matamanio ya kimwili.

UJUE UTAJIRI WA LOWASA

  Tokea enzi ya uhai wa Julius Kambarage Nyerere Faili la LOWASA kufahamika kuwa na utajiri wa kutosha linafahamika sana,na haijaanza leo kwa Lowasa kusemwa na kupewa shutuma kama hizo wala hazikuanza jana.

Zimeanza tokea kipindi Mwalimu Nyerere yuko hai,na hadi alishafikia hatua ya kuhoji utajiri wa Lowasa enz hizo akiwa kijana kama wa miaka 42 hivi,na kwa wakati huo miaka 42 huonekana kijana kweli kweli tofauti na sasa vijana katika umri kama huo washakuwa wazee tayari kutokana na ugumu wa maisha na frustuations zake.

Je,unafaham ni kwa nin MALECELA kwa kawaida tuh tokea hapo kale hampendi Edward Lowasa??

Hii vita haikuanza leo.,wanaccm hawa wawili na wenye ushawish kwenye chama hiko wameanza msuguano na malumbano tokea enzi hizo John Malecela akiwa Waziri Mkuu na Lowasa akiwa Waziri mwandamizi katika ofisi ya waziri ya waziri mkuu,kwa mantiki hiyo kwamba alikuwa chini ya malecela na kwa kumsaidia majukumu ya kazi ya siku zote za kuendesha serikali.

Enzi hizo wabunge wa jamhuri ya muungano wa tanzania walikuwa hawana magari ya kusafiria kama haya wanayokopeshwa kwa sasa,hali iliyokawa inawapa ugumu sana kuwatembelea wananchi wao majimboni hata wakati mwingine ugumu pia wa kuwahi bungeni kwa wakati kutokana na aina ya magari waliyokawa wanayatumia kipindi hiki kukosa stability ya kumudu safari na ukizingatia ubovu wa bara bara wa kipindi huko maeneo mbali mbali ya nchi hiyo.

Hili suala lilikua linaumiza sana serikali kipindi hiko chiniya utawala na usimamiz wake wazir mkuu wa kipindi hicho ndug john malecela.

Kutokana na kuwaza na kuwazua likaja wazo la kupeleka idea kwa serikali ya watu wa japan ili kuona ni kwa namna gani wanaweza kuwasaidia kihali na mali ili iweze kujikwamua katika tatizo hilo,

Mungu si Athumani,serikali ya japan enzi hizo wakakubali kuwaunganisha serikali ya tanzania na kiwanda cha toyota na kuwapa ushirikiano wa hali ya juu katika mazungumzo baina yao na kiwanda hicho hadi ikafikia tamati ya makubaliano kwamba serikali ya tanzania inaweza kukopeshwa magari hayo kisha wakawa wanalipa pole pole ili kusaidia kukizi na kuikubali changamoto hiyo.

Serikali baada ya kufanikisha plan hiyo ikaja kwa wabunge na kuwaeleza kwamba wanaweza kukopeshwa magari kwa mkopo,wabunge waliingia na wasi was kias flan na kusema wao wataweza kulipa vpi gharama hzo ukizingatia pesa waliyokawa wanachukua kipindi hiko isingetosha kulipa mkpo huo??

Serikali kupitia kw wazir mkuu malecele wakawaambia nyinyi chukuen tuh,sisi serikali tutajua tunawasaidia vipi,kwaiyo chukuen kwanza ili mukabiliane na changamoto ya usafiri kwanza.

Wabunge walikubali wazo lile na deal likafanyika,mambo yakafana kisawa sawa.

Sasa baada ya hapo mtu pekee ambae alikuwa anafuatilia mchakato mzima ni wazir wa nchi ofisi ya wazir mkuu enzi hizo akiwa ni edward lowasa,alikuwa anafuatilia suala hilo kwa ukaribu sana.


Wale wajapan walipolipwa chao,kumbe kuna makubaliano ambayo yakishafiikiwa baina yao na wazir mkuu malecela ya kumpatia kifuta jasho kwa kufanikisha deal ile kufanyika kwa ukamilifu wake.

Na yasemekana kifuta jasho hiko kilikuwa cha maana sana,cha maana sana sana,

Bahati mbaya sana wale wajapan walipofika ofcn kuleta kifuta jasho kile walianzia kwanza kwa ofisi ya wazir wa nchi ili wapate nafas ya kumuona wazir mkuu,sasa walipokutana na lowasa yasemekana akawauliza mnafuatia nin tena mheshimiwa ili hali deal ilishafanyika kikamilifu??kwan kuna tatizo??wale wajapan wakamwambia kwamba kuna kifuta jasho yapasa tumkabidh muheshimiwa wazir mkuu malecela.

Lowasa,,akastaajabu..!!akasema ,,"mnasema"???hicho kifuta jasho mnataka kumfikishia vipi mheshimiwa hamjui kuwa yule ni mtu mkubwa sana??kuna utaratibu wa kumfikishia kwa protokali ya serikali,sasa sikilizen bwana....

Hiyo pesa nipen mimi nitamfikishia,kwan kwa sasa hata hivyo yupo safarin hadi arudi,so nipeni mimi nitamkabidh,wale wajapan kwa kuwa wanafaham katika mchakato mzima wa ile deal lowasa nae alikuwa anaifuatilia kwa karibu hawakuwa na was was sana kumwachia amana kama ile.,,wakamwachia na kusign nae kisha wakageuza zao.

Kilichotokea hapo sasa mungu mwenyew ndie anaejua,

Lowasa akapiga kimya,kimya na yeye,yeye na kimyaa,muda ukawa unazid kwenda naskia ile pesa akaanza kuifanyia michakato ya kuizungusha na kuwekeza kwenye biashara ya real estate kwa haraka haraka na kuzikodisha kwa taasisi binafsi hata balozi mbali mbali za nchi mbali mbali,

Naskia ipo moja ambayo aliikodisha kwa ubaloz wa south afrika hapa hapa nchini,na hadi leo naskia iyo nyumba ni mali ya lowasa pamoja na vitu vingine vingi,kwa ufupi lowasa kawa DON tokea kitambo sana.

Sasa maskin mzee malecela akaona siku zinakwenda na kifuta jasho kutoka japan hakifiki,,akaamua kunyanyua simu na kuwavutia uzi jamaa na kuwauliza,ebwan vipi ile kitu yangu??mbona nyinyi wajapan wabaya kias hiko??ina maana baada ya deal kufanyika mnatupa jongoo na mti wake??

Wajapan wakasema Booossi,mbona kifuta jasho tulishaleta mda mrefu sana??tulimkabidh bwana Edward yule wazir wako wa nchi katka ofc yako na alisema atakukabidh kwan ulikuwa safarini..!!!

Malecela kikamshuka,kikampoa na asijue hata awajibu nini,

Ikabid sasa amwite edward na kumuuliza,wewe edward pesa yangu iko wapi??na nani alikuambia uichukue kwa niaba yangu??

Edward akasema Boooss,kwa kweli pesa nilichukua lakin sasa kwa kuwa ulikua safarini nikaona niiweke kwanza hadi urudi,,sasa kama unavyojua pesa tena mzee,kulitokea fursa za uwekezaji nikaamua kujikopesha ili niizungushe kisha nitakurejeshea lakin sasa mambo hayajaenda kama yalivyopangwa ndio kwa maana unaona kimya hiv sijakutafuta.

Sasa malecela presha ikampanda na kumshukaaa,atasema nini??na ile pesa ni chafu na ya deal ukizingatia yeye ni wazir mkuu??kumbuka nyerere yupo hai kipindi hicho na akifaham ishu kama hizo panakua hapatoshi..!!

Ikabid malecela ajikaze kisabun na kufa na tai yake shingoni huku lowasa akiendelea kupimp na kujitanua kwa raha zake.

Kwa kias kikubwa hapo ndipo LOWASA alipoanza kuwapiga GAPE LA KIPATO wenzake walio wengi,na kwa kias kikubwa wenyewe hao ambao wako ndan ya system wanalijua hilo.

Ndio kwa maana tokea zama hizo VITA baina ya LOWASA na MALECELA haiwez kuisha kamwe,kwan mambo waliyofanyiana wawili hao yanatishaa.

Hiyo ndiyo siasa ya bongo ilivyo,DO OR DIE.

CLAB YA WAKRISTO YAFUNGULIWA DAR, WATU WAHOFIA MAADILI YA KIKRISTO KUVUNJIKA


Klabu ya nyimbo za injili iliyofunguliwa jijini Dar es Salaam  

Mchungaji Harris Kapiga wa kanisa la Nchi ya Ahadi lililoko Sinza Kamanyola, ameamua kuanzisha klabu ya usiku kama zilivyo klabu nyingine za starehe.
Klabu hiyo iliyozinduliwa hivi karibuni maeneo ya Mbezi Tangibovu katika hoteli inayoitwa Mak Hotel, imeonekana kuvutia vijana wengi ambao walionekana wakifurahia mandhari na muziki uliokuwa ukipigwa ndani yake.


Tofauti na klabu nyinginezo, Mchungaji Kapiga anasema kutakuwa na udhibiti wa vishawishi vya dhambi ikiwa pamoja na ulevi, mavazi yasiyo na staha na aina ya muziki unaopigwa.
Anasema tangu alipoanzisha wazo hilo, watu wengi hasa wachungaji walikuwa na wasiwasi kuhusu vishawishi hivyo.
“Tangu nimeanza wazo langu hili nimekumbana na vikwazo vingi. Imeshtua watu wengi, japo wengi wamelikubali na kuna baadhi hawakubali ila hawawezi kusema wazi,” anasema na kuongeza:
“Wengine wanajiuliza nitawezaje kudhibiti vipi hali ya klabu kwa sababu maeneo haya kunakuwa na anasa, ulevi na masuala ya mavazi watu watavaaje, na mimi nawajibu.”
“Mtu akija hapa na mavazi mabaya hataingia, tutakuwa makini sana katika hili. Mtu avae nguo yenye staha, siyo mtu aje nusu uchi, tutamtoa kwa nia njema tu. Hata mtu aliyelewa tutamtoa labda tusimgundue.”
 
Mchungaji Kapiga anasema alianza kupata wazo hilo siku alipokuwa kwenye sherehe za kuadhimisha kuzaliwa kwa Clouds Media ambako pia ameajiriwa kama mtangazaji baada ya yeye kuitwa mbele kwa ajili ya utambulisho ndipo alipojongea mbele huku akiimba wimbo wa kumtukuza Mungu ndipo ukumbi wote uliposhangilia na kumsapoti kuimba wimbo huo na ndipo alipogundua ya kuwa wapo wakristo wapendao kutoka nyakati za usiku lakini wanakosa sehemu za kwenda.

Hata hivyo baadhi ya wakristo mitaani wanalalamika wakidai kuwa ukristo unapoteza muelekeo kwa kufanya mambo kama kwenda club. Lakini pia wapo wengine waliofananisha club hiyo na mikesha inayofanyika katika nyumba nyingi za ibada karibu kila ijumaa.

MBUNGE ALIYEOLEWA NA KIJANA AACHWA

www.newsaba24.blogspot.comMichael Christian (28) ambaye mwaka jana aliitikisa medani ya siasa Bongo kufuatia kufunga ndoa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Rukwa, Rose-Sweeter Kasikila (60) ameibuka na kuanika siri zilizomfanya aamue kuivunja ndoa hiyo na mheshimiwa huyo.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Rukwa, Rose-Sweeter Kasikila.

Akizungumza  jijini Dar, Michael alibainisha mambo hayo huku akisema anajuta kwa tukio lile ambalo bado halijamtoka kichwani hadi sasa.


Kijana Michael aliianika siri kwamba ni kuchekwa na marafiki zake wa Bagamoyo mara baada ya kugundua amefunga ndoa na mbunge huyo ‘mzee’.
“Marafiki zangu walianza kunicheka, walisema nimefunga ndoa na mbunge mzee, mama mtu mzima. Nikaanza kujisikia vibaya jambo ambalo sikulipenda hata kidogo,” alisema kijana huyo ambaye ni yatima.
Pia kutokuwepo kwa tangazo la ndoa la siku 21 kama sheria ya nchi inavyotaka ilikuwa ni sababu nyingine ya yeye kumuacha mama huyo. Kuna kifungu cha sheria kinachotaka wachumba wanapotaka kufunga ndoa kutolewa tangazo la siku 21 kwenye mamlaka za kufungisha ndoa hiyo ili kama mmoja wa wahusika ana ndoa inayoishi (halali) aweze kuwekewa pingamizi la kufungishwa ndoa.
Hata hivyo siku ya ndoa yetu hakukuwepo na mashahidi wa pande zote mbili (matroni na patroni) walioandaliwa zaidi ya kuitwa papohapo.
Alimtaja kwa jina moja Mchungaji Mtetumo wa Kanisa la Mikocheni ‘B’ Assemblies of God ‘Mlima wa Moto’ kuwa ndiye aliyesimamia kufungwa kwa ndoa hiyo, Septemba Mosi, 2011 ndani ya ofisi huku milango ikiwa imefungwa.
Alisema pia kwamba, suala la ndoa aliligundua siku hiyohiyo baada ya kufika kwenye kanisa hilo ambapo maandalizi mengine yote yalishafanyika akiwa hajui.
kisha akagundwa yeye ua kuwa katika ndoa yake huwenda hata bahatika kupata watoto na mama huyo kwaku mama huyo tayari anao watoto wakubwa zaidi yake na hata nilipomwambia tuzae alikataa
kitu kingine ni kwamba Alianza kunibana sana, kila hatua ya miguu yangu alitaka kujua inakwenda mpaka wapi! Hii hali nikaiona inanipiga pingu, nikagundua kuwa kumbe mimi sijaoa, bali nimeolewa. Yule mama alinioa mimi, si kwamba mimi nilimuoa yeye, nikasema ili niwe na amani ya moyo ni lazima

“Jambo jingine ambalo pia lilichangia kuamua kuivunja ndoa ile ni baada ya kukumbuka historia ya kukutana kwetu.
“Wakati nipo Hospitali ya Bagamoyo na yeye akiwa pale kama muuguzi mkuu, tulizoeana. Kuna siku aliniita kwake akasema anasafiri anaomba nimwangalizie nyumba, nilikuwa na rafiki yangu tukawa tunalala pale mpaka aliporudi.
“Kuzoeana kuliendelea, mwishowe tukawa wapenzi mpaka ndoa. Nilipokumbuka hivyo tu nikagundua kuwa aliniingiza mapenzini kwa hila au mbinu, hilo pia sikulipenda,” alisema Michael. 

Kijana Michael alisema kutokana na umri wake, ndani ya nyumba alijiona ni mtoto na si mume kama wanaume wengine walivyo.
“Hata uwezo wangu wa mawazo kwake haukuwa wa mume na mke, ni wa mtoto na mama. Kifupi haikuwa ndoa halali,” alisema.
 
Kijana huyo alisema ndoa yake na mheshimiwa huyo aliivunja mbele ya Mchungaji wa Kanisa la Mikocheni ‘B’ Assemblies of God, Dk. Getrude Rwakatare walipokwenda kusuluhishwa ili waende wakaishi kwa amani.
Alisema kabla ya usuluhishi alimfungukia mama Rwakatare kuhusu manyanyaso anayoyapata ndani ya ndoa hiyo ndipo aliposimama na kuivua pete kisha kuitupa chini huku akisema katu hawezi kurudi kwa mkewe huyo na ndoa imevunjika, akaondoka zake.

Kijana Michael alisema kilio chake kikubwa kwa sasa ambacho angependa kifike hadi kwa Rais Jakaya Kikwete ni kitendo cha mkewe huyo kuzuia vyeti vyake ambavyo vingemsaidia kutafutia kazi sehemu mbalimbali.

“Amezuia vyeti vyangu vyote, kila nikimwambia navitaka nikienda ananifanyia visa, nawaomba Watanzania wanisaidie kwa hili.
“Mimi kwa sasa nataka vyeti tu, sitaki cha ndoa wala nini? Lakini hataki kunipa,” alisema Michael.

Akijibu tuhuma hizo, Mheshimiwa Kasikila alikiri kuwa na vyeti vinavyolalamikiwa na mumewe huyo, lakini alikanusha kwa nguvu zote juu ya maneno kuwa yeye ameoana na mtoto mdogo, akirejea vifungu vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, vinavyomtaja mtoto kama ni mtu wa namna gani.
Mbunge: “Mwandishi, unafahamu mtoto kwa katiba yetu ni mtu wa namna gani?”
Mwandishi: “Ni mwenye umri wa chini ya miaka kumi na nane.”
Mbunge: “Sasa Michael ni mtoto? Ana miaka 28 unamuita mtoto?”

Alisema anajua suala hilo lina shinikizo la kisiasa, kwani hivi karibuni baadhi ya wanasiasa walikwenda jimboni kwake wakiwa na nakala ya gazeti moja lililoandika habari zake na kijana huyo na kuwaambia wapigakura wake kuwa mbunge wao ameoa kitoto, lakini wapigakura wake waliwapuuza kwa kuwaambia hilo haliwahusu kwani wanachojua anawawakilisha vizuri bungeni.
“Kama kweli ninyi mnampenda huyo Michael, muelekezeni sehemu sahihi ya kwenda kupeleka madai yake. Ngoja nikupe mfano, mimi nikiwa wizara ya afya, mtu akija na malalamiko kuhusu pembejeo za kilimo, kwa kumsaidia, nitamuelekeza aende wizara ya kilimo, kwa kuwa pale (afya) siyo sehemu yake, sasa nyinyi muelekezeni huyo sehemu sahihi ya kupata haki yake, siyo huko magazetini,” alisema mama huyo

Kwa upande wake, Mchungaji Rwakatare alipopigiwa simu kwa lengo la kumsikia chochote kuhusu ishu hiyo, alianza kulalamikia habari iliyoandikwa miezi miwili nyuma na kukata simu.