Pages

Translate

Saturday 1 February 2014

CLAB YA WAKRISTO YAFUNGULIWA DAR, WATU WAHOFIA MAADILI YA KIKRISTO KUVUNJIKA


Klabu ya nyimbo za injili iliyofunguliwa jijini Dar es Salaam  

Mchungaji Harris Kapiga wa kanisa la Nchi ya Ahadi lililoko Sinza Kamanyola, ameamua kuanzisha klabu ya usiku kama zilivyo klabu nyingine za starehe.
Klabu hiyo iliyozinduliwa hivi karibuni maeneo ya Mbezi Tangibovu katika hoteli inayoitwa Mak Hotel, imeonekana kuvutia vijana wengi ambao walionekana wakifurahia mandhari na muziki uliokuwa ukipigwa ndani yake.


Tofauti na klabu nyinginezo, Mchungaji Kapiga anasema kutakuwa na udhibiti wa vishawishi vya dhambi ikiwa pamoja na ulevi, mavazi yasiyo na staha na aina ya muziki unaopigwa.
Anasema tangu alipoanzisha wazo hilo, watu wengi hasa wachungaji walikuwa na wasiwasi kuhusu vishawishi hivyo.
“Tangu nimeanza wazo langu hili nimekumbana na vikwazo vingi. Imeshtua watu wengi, japo wengi wamelikubali na kuna baadhi hawakubali ila hawawezi kusema wazi,” anasema na kuongeza:
“Wengine wanajiuliza nitawezaje kudhibiti vipi hali ya klabu kwa sababu maeneo haya kunakuwa na anasa, ulevi na masuala ya mavazi watu watavaaje, na mimi nawajibu.”
“Mtu akija hapa na mavazi mabaya hataingia, tutakuwa makini sana katika hili. Mtu avae nguo yenye staha, siyo mtu aje nusu uchi, tutamtoa kwa nia njema tu. Hata mtu aliyelewa tutamtoa labda tusimgundue.”
 
Mchungaji Kapiga anasema alianza kupata wazo hilo siku alipokuwa kwenye sherehe za kuadhimisha kuzaliwa kwa Clouds Media ambako pia ameajiriwa kama mtangazaji baada ya yeye kuitwa mbele kwa ajili ya utambulisho ndipo alipojongea mbele huku akiimba wimbo wa kumtukuza Mungu ndipo ukumbi wote uliposhangilia na kumsapoti kuimba wimbo huo na ndipo alipogundua ya kuwa wapo wakristo wapendao kutoka nyakati za usiku lakini wanakosa sehemu za kwenda.

Hata hivyo baadhi ya wakristo mitaani wanalalamika wakidai kuwa ukristo unapoteza muelekeo kwa kufanya mambo kama kwenda club. Lakini pia wapo wengine waliofananisha club hiyo na mikesha inayofanyika katika nyumba nyingi za ibada karibu kila ijumaa.

No comments:

Post a Comment