Pages

Translate

Thursday 21 November 2013

HATMA NYINGINE YA BABU SEYA NA MWANAE NI LEO

MAHAKAMA ya Rufani leo inatarajia kutoa uamuzi wa ama kulikubali au kulikataa ombi la marejeo lililowasilishwa na mwanamuziki wa dansi nchini, Nguza Vicking ‘Babu Seya’ na mwanae, Papi Kocha ‘Mtoto wa Mfalme’, ambao waliomba mahakama hiyo ifanyie marejeo hukumu ya kifungo cha maisha iliyoitoa Februari 2010, kwa kuwa ina dosari za kisheria na kuwaachia huru.

Kwa mujibu wa hati ya wito wa mahakama iliyotolewa kwa mawakili wa pande zote mbili, mahakama imemtaka Babu Seya na mwanae pamoja na mawakili wa pande zote kufika leo mahakamani ili wapokee uamuzi wa maombi hayo.

Oktoba 30 mwaka huu, jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Nataria Kimaro, Salum Massati na Mbarouk Mbarouk, walisikiliza ombi hilo lililowasilishwa mahakamani hapo na wakili wa waomba rufani, Mabere Marando.

Wakili Marando alidai kwa mujibu wa kanuni ya 66 ya Mahakama ya Rufaa ya mwaka 2009  inatoa mamlaka kwa Mahakama ya Rufaa kufanya mapitio  ya hukumu inazozitoa,  hivyo wateja wake wamewasilisha ombi hilo kwa sababu wanaamini  mahakama ilikosea kisheria katika hukumu yake Februari 2010.

“Waheshimiwa majaji, kwa sababu jopo lenu katika hukumu yake lilikiri wazi wazi  kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilikosea kurekodi ushahidi wa watoto waliodai walitendewa vibaya na waomba rufaa (Babu Seya na Papii) na sheria za nchi zinasema endapo mahakama itabaini kuwa mahakama ya chini ilikiuka taratibu za kurekodi ushahidi wa watoto wadogo, basi ushahidi ule wa watoto wadogo uliotumika katika mahakama ya chini kuwatia hatiani washitakiwa unafutwa na waomba rufaa au washitakiwa wanaachiwa.

“Nafahamu ni kazi ngumu kuwashawishi nyie majaji kubadili uamuzi wenu mlioutoa katika hukumu ya Februari 2010, ambapo uliwatia hatiani wateja wangu, ila kwa utetezi huo wa kisheria niliouainisha unaonyesha katika hukumu yenu mlikubaliana na hoja yangu kuwa Mahakama ya Kisutu ilikosea kurekodi ushahidi wa watoto wadogo, naamini mtatumia busara zenu na kufuata sheria na leo naiomba mahakama iwaachie huru wateja wangu,” alidai Marando.

Mawakili wa upande wa mjibu maombi (DPP), Angaza Mwipopo, Jackson Mlati, Imaculata Banzi na Joseph Pande, waliomba mahakama itupilie mbali ombi hilo, kwa kuwa sababu zote alizozitoa alizieleza wakati wa usikilizwaji wa rufaa na ziliamuliwa katika hukumu iliyotolewa na mahakama hiyo Februari mwaka 2010.

Jackson alidai kama Marando anaona hukumu ya mwaka 2010 ilikuwa na dosari, angeomba mahakama hiyo impangie jopo la majaji watano wa kusikiliza ombi na si ombi lake kusikilizwa na jopo la maji watatu wale wale waliotoa hukumu hiyo ambayo anadai ina dosari.

Wednesday 20 November 2013

KAPUYA MAMBO SI SHWARI, HALI NI TETE.

  Azidi kumtishia kifo binti anayedaiwa kumbaka  

Fedha alizomtumia hadharani, amshambulia Sitta

     
 
 
 
 
 
 
 
 
 

KASHFA ya kumbaka na kutishia kumuua msichana wa miaka 16, inayomkabili Mbunge wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM), imeibua mambo mapya. Wakati serikali inakusudia kufungua mashtaka mawili ya kubaka na kutishia kuua dhidi ya Profesa Kapuya, waziri huyo wa zamani bila woga ameendelea kutuma ujumbe mfupi kupitia simu yake ya mkononi kwa binti huyo na kusisitiza kuwa lazima amuue. Mbali na kutishia kumuua binti huyo na ndugu yake na mtu mwingine yeyote atakayejitokeza kumsaidia, gazeti hili limenasa baadhi ya mawasilino ya simu za ujumbe mfupi wa kuhamisha fedha kutoka kwa Profesa Kapuya kwenda binti huyo ambaye juzi kupitia baadhi ya vyombo vya habari Kapuya alikana kumfahamu na kwamba hajawahi kukutana naye.
      Uchunguzi wetu umebaini kuwa mara baada ya taarifa ya gazeti hili jana kuandika mwendelezo wa kashfa hiyo, huku likimkariri Waziri wa Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Samuel Sitta, akihoji ukimya wa serikali katika kashfa hiyo, Profesa Kapuya alituma ujumbe mwingine wa kutishia kumuua binti huyo. Ujumbe huo kutoka simu namba 0784993930 inayomilikiwa na Kapuya kwenda kwa namba inayomilikiwa na binti huyo, unasomeka hivi: “Ni lazima nitakuua wewe na ndugu yako na atakaetaka kuwasaidia, huyo Sita asijiingize kwenu, yaani nitakuua tena sijui  leo mtalala wapi! We unadhani nani atakayenifunga? Ndo nishakupa ukimwi, sasa nakutaka uache mara moja kuongea na mtu, nitakuwinda popote tuone!” inasomeka sehemu ya ujumbe huo unaodaiwa kutoka kwa Kapuya. Ujumbe huo wa vitisho vya kuuawa, unafanana na ule uliokaririwa na gazeti hili ambao pia unadaiwa kutoka kwa Profesa Kapuya kwenda kwa binti huyo anayedai kubakwa na Kapuya.
       Sehemu ya ujumbe uliopita unasomeka: “Mkiuawa itakuwa vizuri….itawapunguzia gharama za kuishi; usitake kugombana na serikali mtoto mdogo kama wewe. “Sisi ndiyo wenye nchi yetu, mwenye hilo gazeti ni Mbowe sasa mwambieni nyumba ya kuishi si mmemuingizia hela leo? Mnatumika tu bure watu wanaingiza hela nyingi, ila mmenitibua lazima niwaue wiki hii haitaisha; nitapiga kambi kote. Jana si walikuficha? Tuone kama utalindwa milele; maana washatengeneza hela lazima mvae sanda  tu hilo sio ombi ni wajibu wenu. Mnajitia na nyie Mafia watoto siyo!!? “Watoto wetu wanauza unga nani anawakamata? Nani atapingana  nasi!?” Katika kuthibitisha kwamba Kapuya amekuwa na mawasiliano na binti huyo na kwamba anamjua tofauti na anavyodai kuwa hamjui, gazeti hili limenasa mawasiliano ya kutumiana fedha kutoka kwa Kapuya kwenda kwa binti huyo.
       Baadhi ya mawasiliano hayo ni pamoja na yale yaliyofanyika Agosti 31 mwaka huu kupitia simu ya Kapuya ambapo alituma sh 300,000 kwenda kwa binti huyo kama sehemu ya makubaliano ya kutuma pesa kila mwezi kwa ajili ya matunzo.
Mawasiliano hayo ni kama ifuatavyo:
R93NY448 Imethibitishwa
Umepokea Tsh505,000
kutoka kwa JUMA KAPUYA
Tarehe 21/6/13 saa 11:07 AM
Salio lako la M-PESA ni Tsh 505,000
U26UG365. Imethibitishwa Umepokea Tsh 300,000
kutoka kwa JUMA KAPUYA
Tarehe 31/8/13 saa 3:28 PM
Salio lako la M-PESA ni Tsh 300,000
V04EU470 Imethibitishwa Umepokea Tsh 400,000
kutoka kwa JUMA KAPUYA
Tarehe 24/9/13 saa 2:38 PM
Salio lako la M-PESA ni Tsh 400,040

       Tayari serikali kupitia jeshi lake la polisi, limesema linakusudia  kufungua mashtaka mawili dhidi ya mbunge huyo. Mashtaka yanayotajwa kumkabili mbunge huyo ambaye amepata kuwa waziri katika awamu tofauti za uongozi kuwa ni pamoja na ya ubakaji na kutishia kuua. Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, aliliambia gazeti hili juzi kuwa jeshi hilo halitakuwa na sababu ya kumuacha mbunge huyo kuendelea kutamba mitaani huku akituma ujumbe wa vitisho kwa binti wa miaka 16  anayedaiwa kumbaka. Wakati Kamanda Kova akisema hawatakuwa na ajizi na tuhuma za kubaka na kutishia kuua zinazomkabili Profesa Kapuya, Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete imekerwa na kauli ya mbunge huyo wa Urambo Magharibi kuwa serikali haiwezi kumfanya jambo lolote.
          Pia CCM ambayo baadhi ya maafisa wake walijitahidi kumtoa Kapuya kwenye kashfa hiyo, kimeamua kumtosa mbunge huyo aliyewahi kuongoza Wizara ya Elimu na Ulinzi kwa nyakati tofauti baada ya kumtaka aache kukihusisha chama na kashfa yake ya kubaka. Mbunge  huyo anadaiwa kumbaka binti huyo kwenye hoteli moja ya kitalii iliyoko jijini Dar es Salaam mwaka 2011, na kurudia tena kitendo ndani ya ofisi yake katika Jengo la Biashara Complex lililoko Mwananyamala Juni 3, 2012 alipoitwa kwenda kuchukua ada kwa mara ya pili. Kutokana na mfululizo wa habari hiyo ambayo imekuwa ikichapishwa na gazeti hili, Profesa Kapuya kupitia kwa wakili wake Yasin Memba, ametishia kuliburuza gazeti hili mahakamani endapo halitamwomba msamaha ndani ya siku saba. Mbali na kutishia kulipeleka gazeti hili na baadhi ya mitandao ya kijamii mahakamani pia Profesa Kapuya alikana kumfahamu binti anayedai alibakwa huku akikanusha  kumiliki simu namba 0784993930 ambayo imekuwa ikitumiwa kuwasiliana naye ikiwemo kumtumia ujumbe mfupi wa maneno (sms) wa vitisho

MCHUNGAJI KANISA LA PENTEKOSTE HOLLINESS ADAIWA KUBAKA WANAFUNZI



Nyumba anayoishi Mchungaji Mwaikambo ikiwa imepigwa kufuri huku mwenyewe akiwa ''amelala mbele!! baada ya kufanya unyama wake





MCHUNGAJI wa kanisa la Pentekostal aliyefahamika kwa jina la Bryson Mwaikambo(55) anadaiwa kuwabaka na kuwaambukiza ugonjwa wa zinaa wanafunzi wawili wa kike wanaosoma katika shule ya msingi ya Maendeleo wa  kata ya Nsalala wilaya ya Mbeya vijiji mkoani Mbeya.
Wanafunzi hao (majina yanahifadhiwa) wenye umri kati ya miaka 11 na 13 wanaosoma darasa la nne na darasa la sita walifanyiwa unyama huo kuanzia mwaka 2012 ambapo alianza kujenga mazoea na watoto hao wadogo kwa kuwapa peremende  pamoja  na fedha.
Imeelezwa kuwa mchungaji huyo ambaye anaendesha ibada katika kanisa hilo dogo lenye waumini wachache lililopo kitongoji cha kanani kijiji cha ‘Tunduma Road’alikuwa akiwavizia watoto hao kwa muda mrefu kila walipokuwa wanapita kuelekea shuleni.
Wazazi wa watoto wanaodaiwa kubakwa na Mchungaji wakiwa katika sura ya huzuni
 
Katika jitihada zake za kuwanasa watoto hao wa kike alimdanganya mmoja wa wazazi wa watoto aliyefahamika kwa jina la Bw.John Mussa(38) na kumuomba binti yake awe anamsaidia kazi za nyumbani nyakati za jioni kutokana na kuwa  mke wa mchungaji kuwepo safarini.
Kwa kuamini kuwa mchungaji huyo alikuwa ni mtumishi wa Mungu, Bw. Mussa aliridhia mwanaye aende kuishi na Mtumishi huyo wa Mungu bila kujua hatima ya kile ambacho kimemtokea binti yake kwa sasa.
Kwa mujibu wa maelezo kutoka kwa wazazi na walimu wa shule ya Msingi Maendeleo ni kwamba mabinti hao walikuwa wakifanya ngono na mchungaji huyo kwa zamu na kwamba walianza kujua tatizo hilo baada ya kutokea mgongano baina ya wasichana hao wawili .
‘’Tumejua tukio hili baada ya kutokea ugomvi baina yao wa kugombania maji na hivyo kuanza kurushiana maneno, mmoja wa watoto hao alikuja ofisini kushitaki kuhusu ugomvi wao ndipo mmoja akasema kuwa mwenzie anatembea na Mchungaji Mwaikambo’’alisema Mwalimu mkuu msaidizi Bi. Lucy Kamongile.
Alifafanua kuwa, baada ya tukio hilo walimu kwa pamoja walilazimika kuwauliza zaidi ndipo walipoanza kujieleza kuwa wamekuwa wakilala na Mchungaji huyo kwa muda mrefu na kwamba mwanzo alikuwa akiwapa peremende na baadaye akaanza kuwapa fedha.
Alisema kuwa walilazimika kuitisha kikao cha dharura baina ya wazazi wa watoto hao na walimu ambapo walieleza tukio zima la kuingiliwa kimwili na Mchungaji huyo tangu mwaka jana.
‘’Nililazimika kuwaita wazazi pamoja na wanafunzi tulikaa katika ofisi ya walimu, watoto walieleza tukio zima mbele ya wazazi wao juu ya vitendo walivyokuwa wakifanyiwa na Mchungaji huyo.
Alisema kuwa mara baada ya kikao hicho cha wazazi waliwapeleka watoto hao katika kituo kidogo cha Polisi kilichopo  katika mji  mdogo wa Mbalizi ambako walipewa Fomu ya Polisi Na. 3,(PF3) kwa ajili ya kuepelekwa hospitali ili wapatiwe matibabu.
Mwalimu Kamongile ambaye alikuwa na walimu wenzie katika ofisi ya Mwalimu mkuu wa shule hiyo wakati akitoa taarifa hizi mbele ya Ripota Wetu kuwa wanafunzi hao walipatiwa matibabu katika hospitali Teule ya Ifisi ambapo kwa mujibu wa taarifa za mganga aliyewachunguza  watoto hao ni kwamba mbali na kufanyiwa ubakaji wote wawili walikuwa wameambukizwa ugonjwa wa zinaa wa kaswende.
‘’Tukio hili limetufedhehesha sana tulikuwa tunatafakari wapi tutaenda,tunaomba kilio chetu kifike chama cha Waandishi wa Habari wanawake TAMWA kitoe taarifa hizi kwa undani waone namna ambavyo jamii ya pembezoni inavyokosa msaada na haki za kisheria,’’alisema Mwalimu Kamongile.  
 
Shule ya Msingi Maendeleo ambako wanasoma wasichana wanaodaiwa kubakwa na Mchungaji kwa zamu
Mwalimu huyo alisema kuwa wanatambua juhudi za chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA ambazo wamekuwa wakizifanya hivyo wanaimani chama hicho kikisikia suala kitalifanyia kazi kwa kina zaidi kuisaidia jamii ambayo aina mahali pa kusemea.
Kwa upande wa watoto hao ambao walikuwa wakizungumza kwa kupokezana juu ya kadhia iliyowakuta walisema kuwa Mchungaji huyo alianza kufanya nao vitendo vya ngono tangu mwaka 2012 kwa kuwadanganya kwa fedha na peremende na baadaye wakazoea kwenda kwa Mchungaji huyo mara kwa mara.
Mwanafunzi anayesoma darasa la nne alisema kuwa alianza kutembea na Mchungaji huyo wakati akimpitia mwenzie aliyekuwa akiishi nyumbani kwa mchungaji ambapo siku hiyo alimuita chumbani kwake na kumlazimisha kulala kitandani ambapo alianza kumuingiza vidole katika sehemu zake za siri.
“Siku ya kwanza nililia sana wakati mwenzangu yupo pembeni akishuhudia mchungaji akinifanya na ndipo mwenzangu alisema jikaze rafiki yangu”alisema Mtoto huyo.
Alisema kuwa mara baada ya kumuingiza vidole alivua nguo zake na kumbaka huku akilia wakati msichana mwenzie (alimtaja jina) akiwa amekaa pembeni ya kitanda akimweleza kuwa aache kulia kwa kuwa baada ya kumaliza watapewa fedha za kutumia shuleni.
Binti huyo aliendelea kusema kuwa alipata maumivu makali wakati Mchungaji huyo akitekeleza ubakaji wake ambapo mara baada ya kumaliza` alimpa sh.500 na peremende na baadaye alimwita mwenzie kitandani na kufanya naye ngono huku akishuhudia kwa macho yake.
Alisema mara baada ya kumaliza kufanya na mwenzie Mchungaji Mwaikambo aliwaonya wasiseme kwa wazazi wao kisha akawapa fedha na kuwaonya wasiseme jambo hilo kwa mtu yoyote.
Akizungumza sababu za kutosema kwa walimu au wazazi wake binti mwingine anayesoma darasa la sita alisema kuwa Mchungaji huyo aliwatishia kuwachinja na kuwafukia kwenye shimo iwapo atasikia wamesema tukio hilo kwa wazazi ama walimu wao.
Alisema kuwa Mchungaji aliwaomba wazazi wake ili aende kuishi nyumbani kwake kumsaidia kazi kutokana na mama Mchungaji ‘’Mke wa Mchungaji’’ kuwa safarini na kwamba katika siku hizo ndipo Mchungaji huyo alipoanza kulala naye mahusiano taratibu.
Alisema kwa siku za mwanzo alikuwa akimuingiza vidole katika sehemu zake za siri na baadaye akaanza kumbaka ambapo alijisikia maumivu makali lakini alimbembeleza kwa kumpa sh.1000 ambayo alikuwa akitumia shuleni kwa kununua chipsi.
‘’Alikuwa akiniingiza vidole huku chini(akionyesha sehemu za siri) akanibaka, sikuweza kumwambia baba niliogopa atanichinja..mwenzangu alipokuwa anakuja kunipitia kwenda shuleni naye alianza kumuingiza vidole akambaka!!, alilia sana, nikamwambia asilie atatupa hela,’’alisema.
Alisema kuwa wamebakwa na Mchungaji huyo zaidi ya mara nne na kila alipokuwa akiwabaka alikuwa anawapa hela za kutumia shuleni.
Kwa upande wazazi wa watoto hao Bw.Suveli Harrison na Bw. John Mussa walikiri kuitwa shuleni na kupata taarifa za kubakwa kwa watoto wao walipoitwa shuleni ambapo watoto walijieleza walichokuwa wakifanyiwa na Mchungaji Mwaikambo mbele ya walimu.
‘’Jambo hili lilitushitua sana, machozi yalitulenga, hatukutegemea kusikia Mchungaji anaweza kuwabaka watoto ambao ni sawa na wajukuu zake, tulienda polisi walitupa karatasi tukaenda Hospitali ya Ifisi, watoto walikutwa na maambukizi ya ugonjwa wa zinaa,’’alisema Bw. John Mussa.
Alisema kuwa yeye aliridhia mwanaye kuishi na Mchungaji huyo baada ya kuombwa kutokana na mchungaji huyo kuishi na mtoto mdogo wakati mkewe akiwa safarini.
Bw. Mussa alisema kuwa hakujua kuwa kama kuna siku mwanaye atadhurika kwa kufanyiwa kitendo cha unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kama walivyofanyiwa watoto hao na kwamba hata hivyo hadi sasa hakuna jitihada zozote za jeshi la polisi zilizofanikisha kumnasa Mchungaji huyo.
Alisema kuwa kwa sasa watoto hao wamekuwa wakitishiwa na Mchungaji kutokana na kufahamika kuwa yeye aliwabaka na kwamba anaomba msaada wa kisheria kusimamia haki ili sheria iifuatwe dhidi ya mtuhumiwa wa ubakaji.
Naye mzazi mwingine Bw.Suvile Harrison alisema kuwa hakujua chochote juu ya vitendo alivyofanyiwa mwanaye na Mchungaji huyo na  kwamba alifahamu tukio hilo baada ya kuitwa shuleni ambako walimu waliwaita watoto wao na kueleza tukio zima walilokuwa wakifanyiwa na Mchungaji.
Alisema kuwa hakubaini mabadiliko yoyote kwa mwanaye juu ya vitendo alivyofanyiwa na wala hajawahi kuhisi lolote hadi hapo alipoitwa shuleni na walimu.
Baada ya taarifa hizo waandishi wa habari wa gazeti hili walifunga safari hadi katika nyumba ambayo inasadikiwa kuwa ndipo anapoishi Mchungaji huyo na kukuta mlango ukiwa umefungwa lakini alijitokeza jamaa ambaye alijitambulisha kuwa ni mmiliki wa nyumba hiyo Bw. Zacharia Gambi.
Bw.Gambi alisema kuwa anamfahamu mpangaji wake kwa jina moja la Mchungaji Mwaikambo na kwamba mbali ya kuwa ni Mchungaji wa Kanisa la Kipentekoste ni Balozi wa nyumba kumi wa mtaa wa Kanani.
Bw.Gambi alisema kuwa Mchungaji huyo hajaonekana muda mrefu na kwamba mkewe amekuwa na desturi ya kuondoka alfajiri kuelekea shambani na kurudi usiku.
Kadhalika imeelezwa na baadhi ya watu ambao hawakupenda kutajwa majina yao gazetini kuwa  kitendo cha Mchungaji huyo kuwabaka mabinti wadogo kimetokana na imani za nguvu za giza kwamba kwa kufanya hivyo kitamuongezea waumini katika kanisa lake dogo lililopo katika mtaa wa Kanani.
Mama mzazi wa mmoja wa watoto waliobakwa aliyejitambulisha kwa jina la Jane John(35) alisema kuwa awali yeye alikuwa ni mmoja wa waumini katika kanisa hilo lakini baadaye walihamia kanisa jingine baada ya kuona mienendo ya mchungaji huyo kutofanana na kazi ya huduma za kiroho.
Alisema waumini wengi wamehama katika kanisa hilo wakiwemo watoto wake wakubwa wa kike ambao walieleza waziwazi tabia ya ukware ya Mchungaji huyo ya kuwafuatilia mabinti wadogo kwa ajili ya kufanya nao vitendo vya ngono.
Diwani wa Kata ya Nsalala iliyopo Mbeya vijijini Bw.Mashauri Mbembela alipozungumza na waandishi wa gazeti hili alisema kuwa anashangazwa tukio hilo kutoshughulikiwa kwa kipindi chote huku taarifa zikiwa zimefikishwa kituo cha polisi.
Alisema kuwa tukio hilo ni la unyanyasaji ambalo lilipaswa kushughulikiwa kwa nguvu zote na kwamba kuna haja ya kuweka sheria ngumu itakayokomesha vitendo vya ubakaji kwa watoto wa kike.
Bw.Mbembela alisema kuwa ili kukomesha tabia za ubakaji, itungwe sheria ya kuwahasi wabakaji badala ya kuwafunga jela miaka 30  ambako wanaenda kula chakula kinachotokana na kodi za wananchi.
‘’Wabakaji wanafungwa jela, wakimaliza vifungo vyao hurejea uraiani ambako wanaweza kuendeleza vitendo hivyo, njia pekee ya kukomesha ubakaji ni kuwahasi, wakirudi uraiani wataendeleza kujenga Taifa,’’alisema Bw. Mbembela.
Ripota wetu alifanya jitihada za kutafuta namba za simu za mchungaji huyo ambaye mara baada ya kupokea na kuulizwa juu ya tuhuma hizo alikanusha na kusema kuwa huu ni uzushi na uongo uliolenga kumpaka matope ili kuchafua huduma zake anazotoa kwa waumini .
Alidai kuwa kanisa lake la Pentecostal Holiness lenye  jumla waumini nane linatoa huduma za uhakika kijijini hapo hivyo baadhi ya wafuasi wa shetani wanalipiga vita ili lisiendelee kukua ili kuwafikia wanakondoo wengi.
“Wananipakazia tu unaweza kuingiwa na ibilisi na hivi ulivyonipigia nafikiria kuchukua maamuzi magumu na mwili wangu hamtauona kamwe bora uliwe na ndege  na wanyama wa porini  niende jehanamu kuliko kuchafuliwa huku”alisema Mchungaji huyo.
Alisema kuwa tuhuma hizo zimeelekezwa kwake baada ya kumdai fedha mmoja wa wazazi wa watoto hao ambaye alikuwa akifanya kibarua cha kujenga ofisi ya kata ambapo mama huyo alimkopesha fedha sh.5000 na alipoanza kudai ndipo akaanza kuzushiwa tuhuma hizo.
Hata hivyo alisema  Jumanne iliyopita alifuatwa na askari mgambo sita wenye virungu ambao walitaka kumkamata lakini kwa nguvu za yesu walishindwa na kuondoka zao.
“Mimi naishi kwa nguvu za Yesu mtu yeyote mwenye nia mbaya na mimi hawezi kunipata nataka niwe kama mfalme aliyejitoa mhanga nijiue mwili wangu usionekane duniani”alisisitiza na kukata simu.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Bw.Diwani Athumani alisema kuwa amepata taarifa hizo za ubakaji ambapo amemuagiza Ofisa Upelelezi wa Mkoa Bw.Mtatiro Nyamuhanga ambaye atalifuatilia kwa karibu tukio hilo na kwamba hata hivyo mtuhumiwa bado hajatiwa mbaroni.
 
Diwani wa Kata ya Nsalala Mashauri Mbembela akitoa msimamo wake juu ya vitendo vya kinyama walivyofanyiwa mabinti hao

MAREKANI YAITAJA TANZANIA KUWA KINARA WA BIASHARA YA KUSAFIRISHA BINADAMU...


Dar es Salaam. Marekani imetoa ripoti inayozungumzia usafirishaji wa binadamu ya mwaka 2013, huku ikiitaja Tanzania kuwa kinara wa kunyanyasa wasichana, kuwatumikisha katika ngono na usafirishaji wa binadamu.
 
Ripoti hiyo iliyotolewa na idara ya nchi hiyo inayohusika na diplomasia (US Department of State, Diplomacy in Action), pia inaitaja Tanzania kuwa ni kitovu cha njia ya kusafirisha wanawake, watoto na wanaume ambao hutumikishwa kwenye kazi za mashambani na biashara ya ngono.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa Julai mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Seneta John Kerry inaweka bayana kwamba biashara ya usafirishaji wa binadamu hufanywa na baadhi ya ndugu na marafiki ambao hutoa ahadi kwa wahusika kwamba wanakwenda kuwasomesha au kuwatafutia ajira nzuri mijini.

Unyonyaji wa wasichana wadogo na utumikishaji majumbani ndilo tatizo linaloongoza, ingawa kesi za watoto kusafirishwa kwa ajili ya biashara ya ngono katika mpaka wa Tanzania na Kenya zinaongezeka. Pia, wasichana wananyonywa kwenye maeneo ya utalii,” inasema sehemu ya ripoti hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, watoto kutoka Burundi na Kenya, watu wazima kutoka Bangladesh, Nepal, Yemen na India wanatumikishwa kufanya kazi kwenye sekta za kilimo, madini na majumbani nchini Tanzania.

Baadhi ya raia kutoka nchi jirani huingia Tanzania kwa hiari yao, lakini hulazimishwa kufanya kazi majumbani kabla ya kupelekwa kutumikishwa kwenye biashara ya ngono Afrika Kusini, Ulaya na Mashariki ya Kati,” inaeleza.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki alimtaka mwandishi kumtumia ripoti hiyo kwa njia ya baruapepe ili aweze kuisoma na kuitolea maelezo.

Alipotafutwa siku ya pili, alisema kuwa ameipokea na kuikabidhi ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) ili ifanyiwe kazi na baadaye kutoa majibu.

“Ripoti niliipata nikaikabidhi ofisi ya DPP kwa kuwa wao ndio wanaoweza kuitolea maelezo baada ya kuisoma. Maoni yangu lazima yawe ya kitaalamu siwezi kusema bila kupata taarifa kutoka kwao,” alisema.

Lawama kwa Serikali

Ripoti hiyo inaitupia lawama Tanzania kwa kutokuwa na sheria thabiti za kupambana na biashara haramu ya kusafirisha binadamu, huku ikitolea mfano namna ilivyoshindwa kuwasaidia raia wake waliokuwa wakinyanyaswa nje ya nchi.

Kamati ya Serikali ya kupambana na usafirishaji binadamu, haijachukua hatua za kutosha katika kutekeleza mpango mkakati wa kupambana na vitendo hivyo,” inaeleza na kuongeza:

“Serikali imeshindwa kutenga fedha kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa usafirishaji wa binadamu kama ambavyo inaelekezwa kwenye sheria ya kudhibiti biashara hiyo ya 2008.”

Taarifa hiyo inaitaka Tanzania kuongeza nguvu katika kutekeleza sheria ya kudhibiti biashara ya kusafirisha binadamu ya 2008 kwa kuwakamata na kuwashtaki wahusika wote, lakini ikaikosoa kwa kusema inatoa adhabu ndogo kwa mtu anayebainika kufanya makosa, ikiwa ni pamoja na kumhukumu kwenda jela miaka 10, kulipa faini au vyote viwili kwa pamoja.

Sheria hiyo haifanani na nyingine kama za mtu anayepatikana na kosa la kubaka au kufanya kosa jingine la jinai. Mamlaka imesema ina kesi nne inazozichunguza, saba zipo mahakamani toka mwaka jana, zikiwepo mbili mpya,” inasema ripoti.

Pia, Serikali ya Tanzania imelaumiwa kwa kushindwa kuripoti maendeleo ya uchunguzi wa maofisa wake waliotuhumiwa kujihusisha na biashara ya usafirishaji binadamu.

LHRC na TGNP

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema tatizo la usafirishaji wa binadamu pia linachangiwa na wasichana kuwa na tamaa ya maisha mazuri, hivyo kukubali ahadi ambazo hupewa kwamba wanapelekwa kusoma, wasifahamu wanarubuniwa.

“Wengi wanatamani kwenda ‘majuu’ wakidhani watapata elimu, lakini baadaye wanaingizwa kwenye vitendo vinavyowafedhehesha na kuwafanya wakate tamaa kabisa,” alisema.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Usu Mallya alisema katika siku za karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wasichana waliochukuliwa vijijini kwenda mijini kufanya kazi.

Alisema pamoja na tatizo hilo kuongezeka hapa nchini, hakuna tafiti za kutosha ambazo zimefanywa na wadau mbalimbali kuonyesha madhara yaliyopatikana hadi sasa.

Katika siku za usoni kumekuwa na ongezeko kubwa la vitendo vya kunyimwa chakula, kupigwa na kufukuzwa kazi huku wasichana wengine wakitumika kwenye biashara ya ngono,” alisema na kuongeza:

Ripoti hii isiishie kwenye makabrasha bali ifanyiwe kazi ili jamii yote ijue kuwa hili ni tatizo.

Ripoti hiyo inabainisha kuwa watu 47,000 pekee ndio walioweza kuokolewa mwaka jana kutoka kwenye mazingira ya utumikishwaji kati ya milioni 27 waliopo katika hali hiyo duniani.

Tanzania imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi 44 ambazo zinajaribu kupambana na biashara hiyo, lakini hali inazidi kuwa mbaya zaidi

Friday 15 November 2013

MBUNGE WA CCM( PROFESA JUMA KAPUYA )ATISHIA KUJIUA BAADA YA SIRI ZAKE ZA KUMBAKA MSICHANA NA KUMWAMBUKIZA UKIMWI KUVUJA....



MBUNGE wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM), ameingia katika matata. Katika kujaribu kudhibiti mtoto wa shule ambaye anadai alibakwa naye na kuambukiwa virusi vya ukimwi, mbunge huyo ametoa vitisho vya kuua mtoto huyo na kujiua kama njia ya kuepuka dhahama inayoelekea kumkabili.
 
Siku moja baada ya gazeti  la  Tanzania Daima  kuripoti habari za mbunge mmoja (bila kumtaja jina), jana asubuhi Profesa Kapuya ameibuka na kumtisha mwanafunzi huyo mwenye miaka 16 anayesoma Shule ya Sekondari Turiani iliyoko Magomeni jijini Dar es Salaam.
 
Baada ya kujua kuwa mtoto huyo ndiye alitoa habari za masahibu hayo, ambayo mbunge hakutaka yajulikane, alimpigia simu mtoto huyo, na baadaye kutuma meseji kadhaa za vitisho.
 
Jana Tanzania Daima ilishuhudia baadhi ya meseji za simu zilizotumwa na Profesa Kapuya kwenda kwa mtoto huyo.
 
Alfajiri saa 11:21 kupitia simu yake ya mkononi yenye namba 0784993***, Profesa Kapuya alituma ujumbe ufuatao kwa mtoto huyo:“chagueni kunisubiri tuje tuongee au mnataka kufa?”
 
Baadaye saa 1:07 asubuhi, alituma ujumbe mwingine kutoka simu hiyo hiyo kwenda kwa mtoto huyo, ukisema: “Mkiuawa, itakuwa nzuri, itawapunguzia gharama za kuishi. Usitake kugombana na serikali, mtoto mdogo kama wewe. Sisi ndo wenye nchi yetu.
 
“Mwambieni Mbowe mwenye hilo gazeti awape nyumba ya kuishi. Si mmemuingizia hela leo? Mnatumika bure watu wanaingiza hela nyingi, mmenitibua lazima niwauwe wiki hiii haitaisha, nitapanga kambi popote.
 
“Jana si wamekuficha? Tuone kama utalindwa milele. Kazi ya kulindwa imeisha, maana wameshatengeneza hela. Lazima mvae sanda. Hilo sio ombi, ni wajibu wenu. Mnajitia mafia watoto sio? Watoto wetu wanauza unga, nani anawakamata? Nani atapigana nasi?”
 
Hata hivyo, baada ya kuhisi kuwa watoto hao wamedhamiria kumchukulia hatua, na wamewasiliana na taasisi mbalimbali za kiraia na serikali zenye uwezo wa kumtia adabu, mbunge huyo alimtumia mtoto huyo ujumbe wa kuonyesha alikuwa anafikiria kunywa sumu..
 
Ujumbe huo uliotumwa kwa mtoto huyo saa 11:2 3 ulisema:“nimewakosea sana, acha nife mie nakunywa sumu nijiue, na nyie mje mnizike.”
 
Hasira za Profesa Kapuya dhidi ya mtoto hao zilitokana na hatua ya mtoto huyo na dada yake kufichua unyama wanaodai kutendewa na mbunge huyo, ambaye amewahi kushika nyadhifa kadhaa za uwaziri katika Serikali ya Awamu ya Nne.
 
Tangu alipogundua kuwa mtoto huyo alizungumza na gazeti hili juzi, saa 5:17 usiku wa kuamkia jana alituma ujumbe usemao: “Si mpo Bilz? Sasa tupo pamoja na nyie mpaka usiku.”
 
Baadaye saa 5:31 alituma ujumbe  huu: “Hivi hamkubali kushindwa? Leo ulifuata nini ofisi ya CCM?”
 
Ujumbe huo ulitokana na ukweli kwamba dada wa mtoto anayedaiwa kubakwa alifika Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) juzi asubuhi kuonana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana, ili kuomba chama kimsaidie kumbana Profesa Kapuya, ambaye alikuwa ameanza kuwatisha yeye na mdogo wake.
 
Hata hivyo, kwa mujibu wa mtoto huyo, Kinana alisema suala hilo si la chama bali la Profesa Kapuya binafsi.
 
Mtoto huyo alikataa ushauri wa kupeleka shauri hilo mbele ya vyombo vya sheria, akidai kuwa jitihada zake zimekuwa zinazimwa na mbunge huyo anayedai serikali haiwezi kumfanya lolote.
 
Alisisitiza kuwa hana imani na serikali, lakini akasema yupo tayari kuchukua hatua kali dhidi ya Profesa Kapuya iwapo atasimamiwa na watetezi wa haki za binadamu.
 
Baadhi ya mashirika yanayotetea makundi kadhaa yakiwamo Kituo cha Sheria na Haki za BInadamu (LHRC) na Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) yalijitokeza kumsaidia watoto hao, ambao ni yatima.
 
Mtoto huyo na dada yake, wakizungumza na gazeti hili kwa hofu mafichoni, walisema kwa sasa hawana imani tena kama kuna serikali nchini Tanzania kwa kuwa wamedhalilishwa, wametembezwa hadi Bungeni na wabunge bila hatua kuchukuliwa, licha ya kutoa taarifa katika kituo cha polisi Oysterbay tangu mwaka jana.
 
Hata hivyo, kabla ya tukio la watoto hao kuripoti, ofisi za gazeti hili juzi usiku kulikuwa na watu waliokuja wakiwatafuta watoto hao, huku wakiwatisha kwa simu na kuwatolea maneno ya kejeli, wakidai watawamwagia tindikali.
 
Mmoja wa watoto hao, alidai kuwa miongoni mwa vijana waliokuwa wanawatisha juzi walikuwa katika gari T170 BGY, Benz, Cream Metalic, ambayo inamilikiwa na mbaya wao.
 
Jana gazeti  hili lilichapisha habari kuwa  mwanafunzi huyo aliyesema kuwa waziri huyo  alimbaka kwenye hoteli moja ya kitalii iliyoko jijini Dar es Salaam mwaka 2011, na kurudia tena kitendo hicho katika Jengo la Biashara Complex lililoko Mwananyamala Juni 3, 2012 alipoitwa kwenda kuchua ada kwa mara ya pili. 
 
Akizungumza kwa uchungu, alisema mbunge huyo alifanya kitendo hicho kwenye Hoteli ya Giraffe, Jijini Dar es Salaam mwaka 2011.
 
Alisema kuwa yeye alikuwa na urafiki na mwanafunzi mwenzake Zuhura Mwaking’inda. Mwaking’inda amewahi kuwa Diwani wa Kata ya Sinza Jimbo la Ubungo, Jijini Dar es Salaam.
 
Kwa mujibu wa mwanafunzi huyo, rafiki yake (mtoto wa Mwaking’ida) alikuwa amepooza hivyo alikuwa analazimika kumhudumia hali iliyowaunganisha hadi huyo mtoto alipochukua jukumu la kumtambulisha kwa baba yake ambaye naye alimtambulisha kwa Kapuya ili aweze kumsaidia fedha kwa jili ada.
 
Mwanafunzi huyo alisema baada ya kutambulishwa aliitwa katika hoteli moja jijini Dar ambapo baada ya kufika mapokezi wafanyakazi wa  hoteli hiyo walimkataza kuingia chumbani katika maana kwamba umri wake alikuwa mdogo (mwaka 2011 alikuwa na miaka 14), lakini Kapuya aliamrisha aje chumbani pamoja na dereva na kumwingiza kwa nguvu.
 
Akiwa chumbani alimlazimisha kulala naye kisha kumpa sh laki saba, badala ya sh elfu sitini na saba kiasi ambacho kilikuwa ndio mahitaji halisi ya ada.
 
Mwanafunzi huyo amesema baada ya muhula mmoja aliitwa tena na mbunge huyo katika Jengo la Biashara Complex lililoko Mwananyamala tarehe 3 June 2012, ambapo pia alimlazimisha kulala naye kwenye zulia la ofisi yake, kisha kumpa sh 350,000/.
 
Alisimulia kwamba wakati anatoka kwa huzuni ofisini kwa mbunge huyo, mmoja wa wahudumu wa hapo alimuuliza kwanini anatoka kwa huzuni, alimweleza kisa hicho, na huyo mama aliangua kilio kwa kumwambia “mwanangu umekufa pole tu, huyu baba ni muathirika wa ukimwi”.
 
Aliongeza kuwa baada ya kuambiwa vile alilia na kufanya fujo hapo mapokezi hadi alipokamatwa na walinzi wa kisha kupelekwa kituo cha polisi kufunguliwa mashtaka, lakini akiwa polisi alipoeleza mkasa wote, Polisi walilazimika kumwita Kapuya na wakawasuluhisha kwa makubaliano kwamba Kapuya atakuwa anamlipia ada, na kumpa pesa za matumizi sh. laki tatu kila mwezi, jambo ambalo amekuwa akilitekeleza kupitia simu yake ya mkononi 0755993***.
 
Kwa mujibu wa mwanafunzi huyo, 24 Januari 2013, alifika mtu nyumbani kwao mtu mmoja (jina tunalihifadhi) na kujitambulisha kuwa yeye ni jambazi na kuwa alitumwa kwenda kuwaua kwa malipo ya sh. milioni 50, lakini alipokuta ni watoto wadogo aliwasamehe, na kusema yeye ni jambazi sugu hawezi kupoteza nguvu zake kuua vitoto.
 
Alienda akiwa na bastola, maji kwenye chupa yanayodhaniwa kuwa ni tindikali na bomba la sindano. Kwa mujibu wa mtoto huyo, jambazi huyo anasema kuwa tayari alilipwa milioni 15 za awali.
 
Mtoto huyo alisema jambazi huyo aliwambia kuwa yeye ni rafiki wa mtoto wa Kapuya na wanamfahamu vizuri, lakini hataweza kuaua baada ya kubaini kuwa wao ni yatima tu.
 
Hata hivyo kufikia mwezi Februari mwaka huu, mtu asiyefahamika alienda nyumbani na kutelekeza gari aina ya T.199 BGY Mercedes Benzi ya Blue wakati wanafunzi hao wakiwa shuleni, kisha kuacha ufunguo kwa jirani yao kwa maelekezo kuwa wakifika awapatie.
 
Na Kapuya aliwapigia simu kuwaarifu kuwa amempa zawadi ya gari kwa ajili ya matumizi ila yeye na dada yake wanaruhusiwa kuuza ili wapate pesa kwa ajili ya mahitaji yake siku zilizosalia, kwani muda sio mrefu baada ya uchguzi mkuu 2015, Kapuya atakuwa Waziri Mkuu, hivyo itakuwa ngumu yeye kumtumia huyo binti pesa kama alivyoelekezwa na jeshi la polisi kituo cha Oysterbay.
 
Baada ya mwanafunzi huyo na dada yake ambaye ana umri wa miaka 20, kupewa gari walishindwa kulitumia hivyo kutoa taarifa polisi kwani kwa kupokea gari hilo  ilikuwa ni kuwatelekeza kwani yeye hana hata hela ya kuweka mafuta ya gari, hivyo walienda polisi ili kesi ipelekwe mahakamani kumshtaki kapuya.
 
Polisi wa Oysterbay walikubali kulipeleka tatizo hilo kwa Katibu wa Bunge, ambaye alimwita mwanafunzi huyo na mdogo wake waende Dodoma kukutana na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ingawa walipofika Dodoma walikaa na kamati ya hiyo kwa maelezo kuwa Kapuya hakuwepo hadi Bunge lilipoisha walirejeshwa Dar es Salaam.
 
Mtoto huyo na dada yake alitoka ofisi za CCM lakini akiwa anaelekea kituo cha basi alithadharishwa na mwanafunzi mwingine kwa haraka kuwa akimbie kwa kuwa atamwagiwa tindikali na watu waliokuwa wanamfuata nyuma, alikimbilia katika mtaa wa Hoteli ya Star light kisha aliomba msaada baada ya kupotea njia na hivyo alisaidiwa na mama mmoja kufikishwa chumba cha habari cha Channel Ten.
 
Ni katika chumba hicho ndio mwandishi wa habari hizi alienda na kuwakuta watu wawili hao waliokuwa wanamhitaji binti huyo lakini walikatazwa kumchukua.

Chanzo:  Gazeti  la  Tanzania  Daima

MITIHANI KIDATO CHA NNE -2013 YAVUJISHWA



MTIHANI wa Taifa wa Kidato cha Nne, umeingia dosari baada ya walimu wawili akiwamo Mkuu wa Shule, kushikwa wakishiriki kutoa majibu kwa wanafunzi wao.
Tayari Polisi mkoani Singida, inashikilia walimu hao wa Sekondari ya Nkinto wilayani Mkalama kwa tuhuma ya kuvujisha mtihani huo unaoendelea kufanyika nchini kote hivi sasa.
 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, alitaja watuhumiwa hao kuwa ni Mkuu wa Shule, Monica Sebastian (30) na msimamizi wa mtihani huo, Agaloslo Otieno (32).
 
Alisema watuhumiwa hao walivujisha mtihani huo juzi kati ya saa 3 na 3:30 asubuhi katika shule hiyo iliyopo Kata ya Mwangeza Tarafa ya Kirumi.
 
Alidai kuwa Mwalimu Agaloslo aliyekuwa akisimamia mtihani katika shule nyingine ya Mwangeza, aliandika baadhi ya maswali ya Kiswahili na Uraia kwenye simu yake ya mkononi na kumtumia Mkuu wa Shule yake ya Nkinto, Monica aliyekuwa shuleni kwake.
 
Baada ya Monica kupata maswali hayo, inadaiwa alitafuta majibu akiwa chooni huku wanafunzi wakimfuata huko huko na kupewa majibu.
 
Kamanda Kamwela alisema lengo lao lilikuwa kusaidia wanafunzi, wafanye vizuri katika mtihani wao wa kidato cha nne mwaka huu. Alisema wanafunzi waliishaambiwa wadanganye wanakwenda chooni, ili wakapewe majibu na Mkuu wa Shule.
 
"Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa uvujishaji huo ulifanyika kwa nyakati tofauti kati ya Monica na Mwalimu Agaloslo akiwa anasimamia mtihani huo katika shule tofauti.
 
“Baada ya Mkuu wa Shule kutumiwa maswali, alijificha chooni na watahiniwa kwa nyakati tofauti waliomba ruhusa kwa wasimamizi kwenda kujisaidia na hapo walimkuta Mkuu wa Shule na kuwapa maelekezo ya namna ya kujibu maswali hayo," alisema Kamanda Kamwela.
 
Alisema baada ya Polisi kupata taarifa ya siri kutoka kwa wasamaria, iliweka mtego katika Sekondari ya Nkinto na kumkamata Mwalimu Monica huku simu yake ikiwa na baadhi ya maswali ya mtihani.
-Habari Leo

TPA NA TRA AIBU KWAO

SIMU moja baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamisi Kagasheki, kutangaza kwamba Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) inahusika katika ujangili, Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe pia ameibuka leo na kutangaza kwamba TRA pamoja na Mamlaka ya Bandari (TPA) kwa pamoja zinahusika katika biashara ya magendo nchini.
Balozi Kagasheki akiwa visiwani Zanzibar katika zoezi la kupakuwa shehena kubwa ya pembe za Tembo ikiwa na vipande 1,021 na uzito wa kilo 2,915  ambayo haijawahi kukamatwa nchini, alisema kwamba TRA wanahusika katika ujangili huo kwa sababu wao ndiyo wenye mamlaka ya kuhakikisha kwamba mizigo yote haramu haipiti katika bandari hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kagasheki (wa pili kushoto), akiwa ameshika pembe za ndovu zilizokatwa jana jijini Dar es Salaam toka kwa raia watatu wa China katika operesheni aliyoiongoza.PICHA NA MAKTABA
"Katika hili siwezi kumumunya maneno, lazima tu nisema ukweli hata kama wenzetu hawa watakasirika, lakini ukweli ni kwamba hawana pa kukwepea kwani wanahusika kwa asilimia 100 katika ujangili huu, kwa sababu kama watu wasingekuwa na maslahi katika hili kontena lisingekamatiwa hapa Zanzibar, hii ni ishara kwamba TRA wanahusika na kusaidia kulipitisha hadi huku"alisema Balozi Kagasheki.
Balozi alisema kwamba, shehena hiyo iliyokuwa tayari kusafirishwa kuelekea Philiphine ilikuwa katika magunia 98 yaliyochanganywa na magunia mengine ambayo yalikuwa yamefungwa pamoja na baadhi ya vitu vya baharini yalikuwa tayari yameshawekwa ndani ya kontena la futi 40 tayari kwa kusafirishwa kwenda Philiphne yakiwa katika hatua za mwisho za mamlaka husika za bandarini.
Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe akizungumza na Waandishi wa Habari
Katika hatua nyingine, Waziri wa Uchukuzi Dk Mwakyembe akiwa jijini  Tanga ametangaza vita rasmi na wafanyabiashara wanaoingiza bidhaa za magendo kupitia Bandari bubu Mkoani Tanga huku akidai kwamba maofisa wa vyombo vya Serikali waliopo kwenye mtandao huo watakiona cha moto. Dk Mwakyembe aliwataka watambue kuwa, kiama chao kimefika kwa sababu tayari Serikali inayo majina ya wafanyabiashara na baadhi ya maofisa wa Polisi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Bandari (TPA) wanaotumika kufanikisha upitishaji magendo.
Dk Mwakyembe ambaye aliwasili Tanga juzi na kufanya ziara ya ghafla kutembelea bandari bubu zilizoko mkoani hapa, alitangaza vita hiyo alipozungumza na maofisa wa TRA, Polisi, TPA na wafanyabiashara. Alisema baada ya Serikali kudhibiti Bandari ya Dar es Salaam, wafanyabiashara magwiji wa upitishaji bidhaa za magendo wamehamishia nguvu zao Tanga. “Natangaza rasmi vita dhidi ya walio katika mtandao huo, watambue hatuwezi kuruhusu Bandari ya Tanga, bandari bubu na mpaka wa Horohoro kuwa gulio la walanguzi, wapitishaji dawa za kulavya na wahamiaji haramu,” alisema.

MGANGA WA DIAMOND AFUNGUKA HADHARANI


 
Pennie na Diamond ambao wanadaiwa kumtumia Dk Kamdege kufanikisha mambo yao.


 
Dk Kamdege kutoka Tabora ambae inasemekana amekuwa kwenye  ukaribu na mwanamuziki Diamond pamoja na Pennieh hata kabla hawaanzisha mahusiano yako. 

Katika hali isiyotarajiwa habari zilizopatikana muda mchache baada ya kuvuja kwa siri ya undugu wa Pennie na Diamond kumbe chanzo chake inadaiwa mganga mashuhuri Tanzania toka Mkoani Tabora aliyefahamika kwa jina moja Dk Kamdege ambae anahusika kwenye mahusiano hayo. 

 Mganga huyo wa kienyeji ambae amekuwa maarufu sana tangu aanze huduma huyo kutokana na watu maarufu wengi kumfuata kwa ajili ya kutatuliwa mambo yao ikiwemo mafanikio kwenye biashara, kazi, muziki, sanaa, uongozi ngzi za juu pamoja na michezo.

 Habari zaidi zilisema miezi kadhaa iliyopita mganga huyo aliwahi kujitoa kwenye vyombo vha habari akimsihi Pennie aende kwake akamtafutie dawa ili Diamond atulie kwani inamfahamu viuzri mwanamuziki huyo na anajua kitu ambacho angefanya.

 Haikupta muda bila kufahamika kama Pennie alienda kwa Dk huyo au lakini hatimae Diamond alianza kurejea kwa Pennie na mambo yalimalizika kabisa kabla ya kuzuka kwa haya ya undugu na ndio maana watu wa karibu wamesema kuwa Dk huyu anahusika kwenye mahusiano hayo ya Diamond na Pennie kwa kuwa ni watu wake wa karibu sana. 

Blog hii ilimtafuta DK huyo na alipatikana kupitia namba yake ya simu 0788-844490 na 

alianza kusema" Mimi hao vijana nawafahamu sana lakini mimi ni Dk wa Watanzania wote sio Pennie na Wema tu hapana kazi zangu zinakubarika na watanzania wote na hata nje ya nchi kwani mimi nawatolea watu mikosi wanaotaka kuwa maarufu na wenye mafanikio pia nawanyooshea njia kwa hiyo naomba msiseme mimi ni Dk wa Pennie na Diamond hata viongozi wakubwa Serikalini nawapatia baraka zangu kisha wanaenda kufanikiwa huwa sipendi kujitangaza huko kwani mimi situmii uchawi kumpa mutu mfanikio hapana hapa ni miti shamba tu inafanyakazi yake" Alisema Kamdege 

 Aidha Mganga huyo anasemekana amekuwa akitumiwa sana na baadhi ya viongozi serikalini kwa ajili ya mafanikio kupata uongozi, kupandishwa vyeo kazini, kupewa dawa ya kumuona mbaya wako kwa macho tu huku mastaa wengi wa muziki, filamu, na biashara akiwa tegemeo lao...