Pages

Translate

Friday 15 November 2013

TPA NA TRA AIBU KWAO

SIMU moja baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamisi Kagasheki, kutangaza kwamba Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) inahusika katika ujangili, Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe pia ameibuka leo na kutangaza kwamba TRA pamoja na Mamlaka ya Bandari (TPA) kwa pamoja zinahusika katika biashara ya magendo nchini.
Balozi Kagasheki akiwa visiwani Zanzibar katika zoezi la kupakuwa shehena kubwa ya pembe za Tembo ikiwa na vipande 1,021 na uzito wa kilo 2,915  ambayo haijawahi kukamatwa nchini, alisema kwamba TRA wanahusika katika ujangili huo kwa sababu wao ndiyo wenye mamlaka ya kuhakikisha kwamba mizigo yote haramu haipiti katika bandari hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kagasheki (wa pili kushoto), akiwa ameshika pembe za ndovu zilizokatwa jana jijini Dar es Salaam toka kwa raia watatu wa China katika operesheni aliyoiongoza.PICHA NA MAKTABA
"Katika hili siwezi kumumunya maneno, lazima tu nisema ukweli hata kama wenzetu hawa watakasirika, lakini ukweli ni kwamba hawana pa kukwepea kwani wanahusika kwa asilimia 100 katika ujangili huu, kwa sababu kama watu wasingekuwa na maslahi katika hili kontena lisingekamatiwa hapa Zanzibar, hii ni ishara kwamba TRA wanahusika na kusaidia kulipitisha hadi huku"alisema Balozi Kagasheki.
Balozi alisema kwamba, shehena hiyo iliyokuwa tayari kusafirishwa kuelekea Philiphine ilikuwa katika magunia 98 yaliyochanganywa na magunia mengine ambayo yalikuwa yamefungwa pamoja na baadhi ya vitu vya baharini yalikuwa tayari yameshawekwa ndani ya kontena la futi 40 tayari kwa kusafirishwa kwenda Philiphne yakiwa katika hatua za mwisho za mamlaka husika za bandarini.
Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe akizungumza na Waandishi wa Habari
Katika hatua nyingine, Waziri wa Uchukuzi Dk Mwakyembe akiwa jijini  Tanga ametangaza vita rasmi na wafanyabiashara wanaoingiza bidhaa za magendo kupitia Bandari bubu Mkoani Tanga huku akidai kwamba maofisa wa vyombo vya Serikali waliopo kwenye mtandao huo watakiona cha moto. Dk Mwakyembe aliwataka watambue kuwa, kiama chao kimefika kwa sababu tayari Serikali inayo majina ya wafanyabiashara na baadhi ya maofisa wa Polisi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Bandari (TPA) wanaotumika kufanikisha upitishaji magendo.
Dk Mwakyembe ambaye aliwasili Tanga juzi na kufanya ziara ya ghafla kutembelea bandari bubu zilizoko mkoani hapa, alitangaza vita hiyo alipozungumza na maofisa wa TRA, Polisi, TPA na wafanyabiashara. Alisema baada ya Serikali kudhibiti Bandari ya Dar es Salaam, wafanyabiashara magwiji wa upitishaji bidhaa za magendo wamehamishia nguvu zao Tanga. “Natangaza rasmi vita dhidi ya walio katika mtandao huo, watambue hatuwezi kuruhusu Bandari ya Tanga, bandari bubu na mpaka wa Horohoro kuwa gulio la walanguzi, wapitishaji dawa za kulavya na wahamiaji haramu,” alisema.

No comments:

Post a Comment