Pages

Translate

Friday 23 August 2013

HAYA SASA SIJUI TUWAFICHE WAPI WATOTO

Amnajisi mtoto kwa ngono ya mdomoni kwa hadaa ya kumpa mwanasesere

Fundi baiskeli  mmoja mkaazi wa mtaa wa Nsemlwa, wilaya ya Mpanda, mkoa wa Katavi,  Athumani  Mussa (54) amefikishwa jana katika  Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumlawiti (kunajisi)  mdomoni mtoto msichana (4) baada ya kumdanganya  kumpatia mdoli wa kuchezea.

Mtuhumiwa  alifikishwa  mahakamani hapo na kusomewa mashitaka na mwendesha mashitaka mkaguzi wa msaidizi wa polisi Razalo Masembo mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa.

Mwendesha mashitaka aliiambia  mahakama kuwa  mshitakiwa Athumani Musa alitenda kosa hilo Julai 24
mwaka huu majira ya saa 12 jioni nyumbani kwake katika mtaa wa Nsemlwa mjini hapa.

Mtuhumiwa anadaiwa kuwa siku hiyo ya tukio alimwona mtoto huyo akiwa na wenzake wakicheza barabarani karibu na nyumbani kwake ndipo alipomwita mtoto huyo na kumwambia amfuate nyumbani kwake ili akampe mdoli wa kuchezea. Mara baada ya mtoto huyo kuingia ndani, mtuhumiwa alianza kumnajisi mtoto huyo mdomoni huku akiwaamekaa kwenye kochi lake sebuleni.

Ilidaiwa kuwa licha ya mtoto huyo kupiga mayowe ya kuomba msaada, mtuhumiwa hakujali mayowe ya mtoto huyo bali aliendelea na shughuli yake hadi hapo alipomaliza haja yake.

Mwendesha mashitaka alidai kuwa mtoto huyo alipotoka nyumbani kwa mtuhumiwa alielekea nyumbani kwa mama yake huku akilia kwa sauti kubwa, hali iliyosababisha watoto wenzake wamfuate kwa nyuma.

Masembo alieleza mara baada ya kufika kwa mama yake na kuulizwa analia nini, mtoto huyo alitema mdomoni mbele ya mama yake shahawa akimweleza mama yake alichofanyiwa na fundi baiskeli, Musa.

Mama wa mtoto huyo aliangua kilio na kufanya majirani wakusaniyike na ndipo alipowasimulia mkasa huo.

Majirani hao walipochukua jukumu la kwenda kumkamata mtuhumiwa wakiwa wanaongozwa na mtoto huyo ambaye alikataa kuingia ndani ya nyumba ya mtuhumiwa kwa kudai  anaogopa kunajisiwa tena na mtuhumiwa.

Mtuhumiwa Athumani Musa alikana shitaka hilo na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Chiganga Ntengwa aliamuru mshitakiwa apelekwe rumande  hadi Septemba 2 kesi yake itakaposikilizwa.

KESI YA SHEHE PONDA; ULINZI MKALI MISIKITINI




                            Sheikh Ponda Issa Ponda
KATIKA kuhakikisha amani ya nchi haitetereki kutokana na vuguvugu la kesi inayomkabili Shehe Issa Ponda, ulinzi mkali umeonekana kuimarishwa katika maeneo mbalimbali jijini Dar hasa misikitini. 
Misikiti ambayo polisi wamekuwa hawakauki ni pamoja na Mtambani-Kinondoni, Kichangani-Magomeni, Palestina-Sinza, Idrisa-Kariakoo, Kwa Mnyamani-Buguruni, Mtoro-Kariakoo na misikiti mingine yenye wafuasi wengi wa kiongozi huyo.
Ijumaa ambalo limekuwa likipitapita maeneo hayo lilibaini kuwepo kwa mapolisi ambao wamekuwa wakirandaranda wakiwa kwenye pikipiki na magari, lengo likiwa ni kuhakikisha wafuasi wa kiongozi huyo wanakuwa kwenye utulivu.

Aidha, imebainika kuwa, watu wa usalama wa taifa pamoja na polisi waliovalia kiraia nao wamekuwa wakitinga misikitini na kufanya ibada na waumini wengine lakini wakiwa na jukumu lingine la kuhakikisha ibada zinaendelea bila kuwepo kwa uvunjifu wa amani.
Akizungumza na mwandishi wetu mmoja wa waumini katika Msikiti wa Mtambani aliyejitambulisha kwa jina la Hamad Juma, mkazi wa Makumbusho jijini Dar alisema anashangazwa na uwepo wa polisi katika maeneo hayo kwani wao hawana malengo ya kufanya vurugu ila pale itakapobidi watafuata sheria kwa kukusanyika au kuandamana.

“Hii kesi ya Ponda imetikisa nchi na inaendelea kutikisa, tumekuwa tukiona polisi wakirandaranda wakiwa na ‘yunifomu’ na wengine wakiwa wamevalia kiraia.
“Ninachoweza kusema ni kwamba sisi tutaandamana pale itakapobidi lakini nawashauri Waislam wenzangu tuwe na subira, tuache vurugu na kikubwa tumuombe Mungu awe nasi katika kipindi hiki kigumu ambacho kiongozi wetu anapitia.

“Tuwe watulivu, tuache sheria ichukue mkondo wake lakini tunaiomba serikali ijue Ponda ana watu wengi nyuma yake ambao hawatakubali kuona anatendewa kinyume na haki,” alisema muumini huyo.
Jumatatu iliyopita, Shehe Ponda alisomewa mashtaka matatu katika Mahakama ya Mkoa wa Morogoro na baadaye alirudishwa rumande katika Gereza la Segerea lililopo jijini Dar

RIPOTI MAALUM:UBAKAJI WA WAJANE NI UBAKAJI ULIOHALALISHWA UKEREWE


Bi. Arodia Gebasaki ambaye ni mjane akisimulia jinsi mila ya kutakasa wajane inavyofanyika kwa mwandishi wa makala haya (hayupo pichani) ambapo yeye alikataa kufanyiwa mila hiyo na hakuna madhara yoyote aliyopata tangu kufiwa na mume wake, miaka 14 iliyopita
 
Baadhi ya wajane wakiwa katika picha ya pamoja na mwandishi wa makala haya baada ya kufanya mahojiano kuhusu mila ya kutakasa wajane wilayani Ukerewe, Mwanza. Wajane hao wameipiga vita mila hiyo kutokana na kumdhalilisha mwanamke. 

"Udhalilishaji huu uliojificha katika mila inayoitwa Okusomboka kwa Wakerewe ni tendo ambalo hufanyika kwa maana ya kuhitimisha uhusiano wa ndoa kati ya mume na mke aliyefiwa. Mila hiyo huhitaji uhusiano huo uhitimiswe hivyo sababu ulianzishwa kwa tendo la ndoa.BIBI alibakwa,mama akabakwa, dada amebakwa na mke wangu atabakwa nitakapofariki.”


Huo ndiyo uhalifu mkubwa uliojificha kwenye mila ya Okusomboka (kutakasa) kwa wakazi wa Ukerewe hasa kwa Wakara na Wajita.Kwa Wakerewe ubakaji ni jambo la kawaida na unatukuzwa kwa mikono miwili kupitia mila ya Okusombaka.


Hayo ndiyo maisha ya kawaida kwa wakazi wa Ukerewe mkoani Mwanza wanaotukuza ubakaji, mbakaji anapomaliza tendo hilo, wakati mwingine anashangiliwa kwa kupigiwa vigelegele na akina mama akionekana shujaa wa kuondoa watu mikosi kupitia ubakaji, ingawa wao hutafsiri kuwa wanasomboka.


Ubakaji huo kupitia mila ya Okusomboka ni sehemu ya maisha ya kawaida kwa wakazi wa Ukerewe na unaheshimiwa kiasi kwamba wale wanaokataa kubakwa wanatengwa na kunyooshewa vidole kila wanapopita.


Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili wilayani Ukerewe Mkoa wa Mwanza juu ya mila ya Okusomboka (utakasaji) umebainisha vitendo vya ubakaji vimekuwa vikitendeka tangu enzi na enzi na kuingia katika karne hii ya sayansi na teknolojia.


Ambapo ubakaji huo, unalenga wanawake wajane na unafanyika siku ya nne ya matanga tangu kutokea kifo cha mwanaume ndani ya familia.Bila kujali uchungu anaokuwa nao mjane wa kupoteza mume wake, anatafutiwa mbakaji (Omwesya-yaani mtakasaji) ambaye anakodiwa na kulipwa ujira ili kutekeleza kitendo hicho cha kubaka mjane, ambacho kwa Ukerewe ni cha heshima, katika kuhitimisha uhusiano kati ya mume aliyekufa na mjane aliyebaki.


Ingawa sheria ya Makosa ya Kujamiiana ya Mwaka 1998 inatoa adhabu kali kwa watu wanaopatikana na hatia ya makosa ya ubakaji, kwa Ukerewe hawajui kama Okusomboka ni kubaka, hivyo kukiuka wazi wazi sheria hiyo inayotolewa kwa watu wanaofanya vitendo hivyo.


Ubakaji unafanyika kwa uwazi na wameenda mbele zaidi kwani kuna watu maalumu ambao wanalipwa fedha na wakati mwingine hata mifugo kwa ajili ya kuwabaka wanawake wanaofiwa na waume zao kwa hoja kwamba wanatimiza sharti la mila hiyo.


Mbakaji kabla ya kuanza kitendo hicho, huwa anaandaliwa chakula maalumu ikiwemo pombe ambayo huwa anakunywa na kuchangamka na hapo ndipo anaaza kubaka.


Kutokana na hali hiyo wanawake wengi walioolewa wilayani Ukerewe ni wabakwaji watarajiwa na wale watakao kataa kubakwa, basi wajiandae kutengwa na ndugu, kunyooshewa vidole na jamii inayowazunguka na mali za marehemu waume zao kutotolewa urithi.


Pia, mjane anayekataa kutakaswa ajiandae kutopata mwanaume wa kumuoa.


Vi kwa z o h i v y o , n d i v y o vinavyowashinikiza wakubali kubakwa na watu maalumu ambao hukodiwa kwa fedha au kulipwa mifungo kwa ajili ya kubaka wajane.


Katika mila hii, mwanamke analazimishwa kufanya tendo la ndoa bila ridhaa yake tena na mtu asiyemfahamu na haandaliwi kwa namna yoyote ile kwa ajili ya tendo hilo.


Wakati kwenye majumba ya utakasaji unafanyikwa kwa njia ya maombi, kwa Ukerewe unafanyika kwa njia ya ubakaji.


Okusomboka ni tendo la ndoa linalohusisha watu wawili, mjane ambaye amefiwa na mume au mke na mwingine ambaye yupo kwa ajili ya kazi hiyo.


Mfano leo hii ikitokea mwanamke akafiwa na mume wake, baada ya mazishi yanafanyika matanga ambapo siku ya nne ya matanga, anakodiwa mtu kutoka miongoni mwa watu wanaokodishwa kwa ajili ya kutakasa mjane na kufanya naye tendo la ndoa tena bila hiari ya mjane.


Ubakaji uliojificha kwenye mila ya Okusomboka (kutakasa) kwa Wakerewe ni tendo ambalo linafanyika kwa maana ya kuhitimisha uhusiano wa ndoa kati ya mume na mke ulioanzishwa kwa tendo la ndoa, hivyo ni lazima uhusiano huo uhitimishwe kwa tendo hilo kutokana na mmoja wa wanandoa kuwa amefariki.


Utakasaji huo unafanyika kwa pande zote yaani mwanake na kwa mwanaume, lakini unatofautiana mazingira unapofanyika.


Mfano, mwanamke anapofiwa na mume wake anakodishwa mtu maalumu wa kufanya naye tendo la ndoa na hapo kunakuwa hakuna maridhiano yoyote kati ya mtakaswaji na mtakasaji, bali maridhiano yanatokana na kile anacholipwa mtakasaji ndipo anafanya tendo hilo.


Lakini, mwanaume anapofiwa na mke wake anaenda mwenyewe mtaani kutafuta mwanamke wa kufanya naye tendo la ndoa wakati mwingine akisindikizwa na wapambe watakaothibitisha kwamba, alipata mwanamke na kufanya naye tendo la ndoa, hivyo anakuwa ametakasika.


Wanafanya hivyo, kwa kuamini kwamba, marehemu wakati anafikwa na mauti hakupata fursa ya mwisho ya kufanya tendo la ndoa hilo na mwenzi wake.


Kwa msingi huo, wanafanya hivyo kama ishara ya kuhitimisha uhusiano wa wanandoa hao, yaani marehemu na yule aliyebaki hai.


Wakerewe wanaamini kuwa, mjane au mgane akishatakaswa ile mikosi yote iliyosababisha kifo cha marehemu inakuwa imeondolewa yote.


Pia wanafanya hivyo kwa kuamini kwamba, marehemu wakati anafikwa na mauti hakupata fursa ya mwisho ya kufanya tendo hilo na mwenzi wake.


Hiyo inakuwa ni ishara ya kumalizika kwa uhusiano wa wanandoa hao, yaani marehemu na yule aliyebaki hai.


UBAKAJI WENYEWE


Mmoja wa wazee anayefahamu mila hiyo ambaye pia aliwahi kufanyiwa mila hiyo, Juma Mtallo (83) mkazi wa Nkilizi katika Kijiji cha Mmakeke wilayani Ukerewe, anasema pindi mwanamke anapofiwa na mumewe, kama kawaida yanafanyika matanga kwa siku kati ya tano na saba kulingana na uwezo wa wafiwa.


Katika kipindi hicho, mjane huyo anatakiwa kuhudumiwa na kuandaliwa chakula na mtu aliyewahi kufiwa na mwenzi wake.


“Anakuwa ndani ya nyumba amefunikwa nguo na wanaoenda kumsalimia na kumhudumia ikiwa ni pamoja na kumpikia chakula ni wale waliowahi kufiwa,” anasema Mtallo.


Anasema, kwa kipindi hicho anakuwa hajaoga. “Siku ya nne ndipo wanaanza taratibu za kumuogesha na akishamaliza ndipo anapelekwa kwa mbakaji (mtakasaji).”


Anaongeza kwamba baada ya mtakasaji kumaliza kazi hiyo, anaondoka kwa majigambo na wakati mwingine akiimba; “Wanaume wafe wanawake wabaki…wanaume wafe wanawake wabaki,” anasema huku akiongeza huwa anaimba hivyo ili wanaume wazidi kufa na yeye azidi kupata kazi ya kubaka wajane.


SIKU YA UBAKAJI


Kwa mujibu wa mila hiyo, siku ya kubaka, mbakaji huwa anaandaliwa chakula kizuri pamoja na vinywaji hasa pombe kwa gharama za familia inayotakaswa.


Mmoja wa wanawake waliowahi kutakaswa, Anna Sebastiane mkazi wa Tarafa ya Ukara Kata ya Bukungu, wilayani Ukerewe anasema, siku mtakasaji anapoenda kutakasa mjane, anapokelewa kwa heshima kubwa.


Anaeleza kwamba wakati mwingine anaweza kumwambia mtakaswaji; “Hebu cheza nione kama unaweza,” anasema yaani aoneshe umahiri wa kutikisa nyonga wakati wa tendo la ndoa.


Anafafanua kwamba, endapo ataona mjane hawezi kutikisa nyonga, anaongeza gharama. Mfano endapo aliwatoza fedha basi atapenda aongezewe kiasi atakachoona kinamfaa au kama ni mifugo kama vile mbuzi, atataka aongezewe mwingine kwa jinsi atakavyoona inafaa.


Hata pale asipovutiwa sura ya mtakaswaji, mtakasaji anapandisha gharama kwa jinsi atakavyoona inafaa.


Anasema, endapo utakasaji utafanyika nyumbani kwa marehemu basi ndani ya nyumba inabidi wawepo watoto wake ambao hawajaolewa.


“Wakati utakasaji unafanyika (ubakaji) watoto wanakuwa wanasikia jinsi Omwezya (mtakasaji) anavyonguruma (akitoa maelekezo kwa sauti nene akimwelekeza mjane jinsi anavyotaka alale au namna ambavyo anataka atingishe nyonga yake) na hapo kitanda kinachokuwa kinatumika ni cha marehemu,” anasema Sebastiane.


Anapoulizwa kama watoto wanasikia hiyo sauti? Sebastiane anacheka kwanza huku akivuta pumzi, kisha anasema;


“Sio watoto peke yake, hata wanaokuwa nje wanafahamu kinachoendelea …si unaona hali ya nyumba zetu (mbovu kiasi kwamba nyingi hazina faragha). Anasema anakuwa anahimiza mtakaswaji atingishe nyonga ili apate raha.


“Watakasaji wengine, hawakuwa na staha na tendo la ndoa, kwani walipokaribia mshindo (kutoa mbegu za uzazi) walipiga kelele kwa kunogewa na uhondo wakati huo huo akiashiria kwamba kazi aliyopewa amehitimisha,” anasema na kuongeza kuwa akishamaliza anavaa nguo na kutoka nje ya nyumba kwa mbwe mbwe kisha kulipwa chake.


Anasema, watakasaji wengine waliondoka wakiimba; “wanaume wafe wanawake wabaki..wanaume wa f e wa n awa k e wa b a k i . ” Anasema hiyo kwa kufurahia kile walicholipwa. “Wakati anaondoka anapigiwa vigelegele na akina mama kwa kufurahia kuhitimisha mila hiyo…mila hii unaweza kuiona ni mbaya, lakini yakishakufika utaona umuhimu wake,” anasema Sebastiane.


Hata hivyo, anasema: “ Mila hii (Okusomboka) ni aibu kwa watoto wanaokuwa ndani ya nyumba wakisikiliza mama yao akitakaswa, huku akihimizwa atingishe nyonga… tendo la ndoa linahitaji faragha, lakini utakasaji hauna faragha na unamdhalilisha mwanamke,” anasema na kuongeza kuwa ni jambo la aibu ndiyo maana tendo la ndoa linahitaji faragha.


Sebastiane anapoulizwa kama mtakasaji anatumia kondomu ili kujikinga na magonjwa, anasema jambo hilo halipo.


Pia anasema, mtakasaji na mtakaswaji wanatakiwa wafanye tendo moja la ndoa (yaani mshindo mmoja) na wasifanye tena tendo hilo maishani mwao, endapo wakirudia watakuwa wamekiuka sharti la mila hiyo hivyo mikosi inaweza kurudia familia ya mjane.


“Kwa hiyo atalazimika atakaswe (abakwe) upya na mtakasaji mwingine, vinginevyo wanaamini kuwa familia yake itaendelea kuandamwa na mikosi,” anasema .


Anataja mikosi hiyo kuwa ni pamoja na familia kuandamwa na vifo na kuugua mara kwa mara.


MASHAHIDI


Mashahidi wanaoshuhudia tukio hilo, wanasema wanakuwepo kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tendo hilo limefanyika, ili kuondoa wasiwasi wa wajane kudanganya.


Mjane mwingine, Arodia Gabaseki (64) mkazi wa Kata ya Ulagala, Tarafa ya Masonga wilayani Ukerewe anasema mashuhuda wanakuwa nje katika mazingira ambayo watakuwa na uhakika kuwa tendo hilo linafanyika.


Anasema kwamba, kutokana na wajane kuogopa mikosi, lazima wakubali na kwamba mgurumo wa mtakasaji nao kwa wakati mwingine ni ishara nzuri kwao.


Anaeleza kwamba, mara baada ya kutakaswa anarejea nyumbani akiwa ameinamisha kichwa chini na kupokewa kwa furaha na wanandugu waliopo kwenye matanga, kwa kuwa wanaamini kuwa uhusiano kati ya mjane na marehemu umehitimishwa na hakuna matatizo yoyote yanayoweza kuwapata.


SIFA YA MTAKASAJI


Ofisa wa Taasisi ya Kuboresha Mila na Desturi katika Jamii ya Ukerewe (KUMIDEU), taasisi ambayo inajihusisha kutoa elimu ya kutokomeza mila ya kutakasa wajane, Musiba Kakulu anasema mtakasaji ni mtu anayeonekana hakubaliki ndani ya jamii kutokana na matendo hayo.


Anasema, watakasaji wengi ni walevi, wachafu, wasiokuwa na wanawake na mara nyingi walitegemea kuendesha maisha yao kwa kutegemea malipo wanayopata kwa njia ya utakasaji.


“Kutokana na umuhimu wa mila ya kutakasa, mtakasaji (Omwezya) anakuwa hana umuhimu ndani ya jamii,” anasema Kakulu. Sifa nyingine anasema ni mtu anayejua dawa na anayependa kusimamia mila na desturi.


Pamoja na kuwa na hali hiyo, lakini thamani yao inaonekana pale walipohitajika kutakasa, kwani watu wenye heshima zao ndani ya jamii hawakubali kabisa kutakasa watu ambao tena haijulikani wenzi wao wamefariki kwa magonjwa gani.


“Mtakaswaji kama ni bibi kikongwe, anapata shida kwani mtakasaji anatoza gharama kubwa kama vile ng’ombe wakati uwezo anakuwa hana, lakini ndugu lazima wachangishane ili wampate ng’ombe huyo,” anasema.


Anasema, wakati mwingine mtakasaji anapotakiwa kwenda kwa mtakaswaji na ni mzee sana analazimika atafutiwe usafiri hadi nyumbani kwa mjane

DIAMOND APATA MWANMKE MPYA

 


MWANAMUZIKI Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amegeuka gumzo nchini Kenya baada ya mrembo mmoja aliyejipatia jina kupitia Runinga ya KTN, Angel Maggy kutangaza penzi lao upya kwa mara nyingine.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari za burudani vya Kenya, mara baada ya Diamond kufanya shoo mbili katika Miji ya Nairobi na Mombasa nchini humo, alipogeuza kisogo kurejea Bongo ndipo ukaibuka mlipuko wa habari zilizomhusu na mrembo huyo.

Ukiachilia mbali gumzo la vurugu zilizotokea baada ya Diamond kucheleweshwa kupanda stejini na kusababisha watu kupigwa chupa huko Mombasa, kilichofuata ni skendo ya mapenzi na mrembo aliyepata jina kupitia kipindi cha Tujuane cha KTN.

Habari hizo zilieleza kuwa mara tu baada ya kutua nchini humo, Diamond alipokelewa kwa bashasha na mrembo huyo akiwa na wenzake wanne.

Ilielezwa kuwa tofauti na warembo wengine, Angel alimganda Diamond kila kona kuanzia akiwa jijini Nairobi katika shoo yake ya kwanza na siku ya pili aliambatana naye hadi Mombasa kwenye shoo ya pili.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz' akiwa naAngel.

Ilisemekana kuwa alipokuwa akifanya shoo kwenye Ukumbi wa KICC, Nairobi siku ya kwanza, Diamond aliimba wimbo wake wa Ukimuona maalum (dedication) kwa ajili ya Angel, jambo lililomfanya mrembo huyo kuonekana ‘spesho’ miongoni mwa maelfu waliohudhuria onesho hilo.

Imeripotiwa kuwa baada ya shoo hiyo kumalizika ‘naiti’ kali, Angel alionekana ‘beneti’ na Diamond wakielekea katika hoteli aliyofikia staa huyo Nairobi.

Hata hivyo, hakuna mahali palipoelezwa kama walilala wote usiku huo.

Habari zilizidi kutonya kuwa kesho yake mrembo huyo alionekana kila kona aliyokatiza Diamond mjini na baadaye kwenye shoo ya Mombasa ambako huko ndiko kulipotawaliwa na vituko vya kufa mtu.

Ilidaiwa kuwa kwenye shoo hiyo ndiko Angel alipokuwa akiahidi kumpa Diamond mahaba mazito kupitiliza yale aliyokuwa akipewa na zilipendwa wake, Wema Isaac Sepetu kwa kuwa wanamjua.

Ikasemekana kuwa wakati Mkenya huyo akitamba kwa mara nyingine kuwa ndiye demu wa Diamond na kupewa jina hilo (Demu wa Diamond), warembo wenzake walikuwa wakimuonea wivu kwa kuwa mwanamuziki huyo ni gumzo kwa wanawake nchini humo.

Ilidaiwa kuwa wakati Angel akijitapa kuwa ndiye malkia mbele ya mfalme Diamond, mashosti zake waliojiita mashemeji, nao walikiri kumkubali mwanamuziki huyo.

Ilisemekana kuwa Angel na wenzake walimbatiza Diamond jina la Mfalme wa Afrika Mashariki hasa alipofanya shoo iliyowaacha watu hoi kwa namna alivyokonga nyoyo zao.

Baada ya shoo kuliibuka madai mazito kuwa Angel alipata nafasi adimu ya kwenda kulala na Diamond katika hoteli aliyofikia huko Mombasa Beach.

Iliendelea kufahamika kuwa wawili hao hawakuonesha ugeni wa kuonana kwani walionekana ni watu waliozoeana kwani mara kadhaa Angel wa Diamond alinukuliwa akisema yeye ndiye malkia wa staa huyo wa Wimbo wa Kesho.

“Wanaonekana kuzoeana kwa sababu mwaka jana walikutana Mombasa ‘so’ siyo mara yao ya kwanza, wanakumbushia, sema tu safari hii imekuwa ‘too much’,” ilisomeka sehemu ya habari hiyo.

Katika kuonesha kuwa kuna kitu kati ya wawili hao, Angel amejichora ‘tattoo’ ya jina la Diamond na alama za ‘malavu’ kwenye mkono wa kushoto huku rafiki zake wakidai kuwa ana nyingine ya mwanamuziki huyo aliyojichora sehemu nyeti.

Baada ya kuwepo kwa habari hizo ambazo hakuna mahali Diamond alipopewa nafasi ili kupata mzani wake, gazeti hili lilimtafuta Diamond na kumpa A-Z ambapo alikiri kumfahamu Angel na kufunguka anachokijua.

“Namjua (anatajiwa Angel), kila nikienda huko huwa anapenda kuwa na mimi. Nilipofika kule (Nairobi) niliandaliwa mamodo ambao nilikwenda nao Mombasa na huyo mrembo alikuwa mmoja wao.

“Alinionesha hata hiyo tattoo akaniambia ananipenda sana na ndiyo maana kajichora jina langu.

“Kweli kuna picha tulipiga, huwa huyo mrembo anajitangazia huko Kenya kuwa anatoka na mimi kimapenzi ila si kweli namjua tu kawaida,” alisema Diamond kwa makubaliano kuwa akimaliza shoo ya Fiesta leo mkoani Tabora atatafuta chansi kulizungumzia sula hilo kwa kina.


Hata hivyo Penny alipotafutwa kupitia simu ya kuganjani hakupatikana hewani lakini kwa mujibu wa rafiki yake wa karibu, mrembo huyo hajui chochote kinachoendelea.

Septemba mwaka jana,kunataarifa zilienea baada ya Angel kujitapa kulala na staa huyo alipokwenda nchini humo kwa ziara ya shoo ambapo Diamond alisikitishwa na kitendo hicho hivyo habari hii ni mwendelezo wa madai ya mrembo huyo kuwa penzi lao limeibuka upya.

27 WAUAWA, 350 WAKIJERUHIWA KATIKA MILIPUKO NCHINI LEBANON



Wananchi wakiwa wamekusanyika eneo la mlipuko nje ya msikiti wa Sunni uliopo jijini Tripoli, Lebanon.
Wananchi wakiangalia uhalibifu uliotokea baada ya mlipuko.
Magari yaliyohabiriwa katika mlipuko huo.
Mwananchi huyu akchukua picha katika simu yake ya mkononi.
(PICHA ZOTE NA AP)
MILIPUKO mikubwa miwili imetokea leo nje ya misikiti katika jiji la Tripoli lililopo Kaskazini mwa Lebanon jirani na Syria. Katika milipuko hiyo, watu 27 wanadaiwa kupoteza maisha, wakati 350 wakijeruhiwa. Milipuko hii imeongeza mvutano nchini Lebanon ikiwa ni matokeo ya vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea nchini Syria kati ya wafuasi na wapinzani wa utawala wa Rais wa Syria, Bashar Assad.

TFF: YANGA WAMEONGEZA ADHABU YA MRISHO NGASSA



Mrisho Ngassa.
Na Khatimu Naheka
IMEFAHAMIKA kuwa Klabu ya Yanga, ndiyo iliyochangia ukubwa wa adhabu aliyopewa kiungo wake mshambuliaji Mrisho Ngassa, Championi Ijumaa limebaini.
Taarifa hiyo inakuja wakati ambao Ngassa amefungiwa kucheza mechi sita za mashindano pamoja na kuilipa Simba jumla ya shilingi milioni 45, sababu kubwa ikiwa ni kusaini mikataba miwili, ule wa Yanga na ule wa Simba.
Boniface Wambura ambaye ni Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ameliambia Championi Ijumaa kuwa, adhabu ya kufungiwa michezo sita kwa Ngassa imewekwa maalum, kutokana na Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji kutaka mchezaji huyo apate uchungu wa makosa aliyoyafanya na siyo kutegemea kulipiwa na klabu.
Wambura alisema adhabu hiyo imetokana na kasumba ya klabu mbalimbali ambazo zimekuwa zikiamua kulipa faini wanazokatwa wachezaji wao kwa makosa mbalimbali, maamuzi ambayo yanasababisha wachezaji kurudia makosa hayo.
“Adhabu kama hii ni maalum kuweza kumfanya mchezaji aone makali ya kosa alilofanya ili asiweze kurudia wakati mwingine, kamati imebaini kuwa makosa kama haya kila wakati yanakuwa yakijirudia kwa kuwa klabu ndizo zinazosababisha hilo,” alisema Wambura na kuongeza:
“Hata huku TFF, tunaona jinsi klabu zinavyofanya, endapo mchezaji fulani anapofanya makosa na kuhukumiwa utaiona klabu ndiyo inakuja na kuilipa faini husika, maamuzi kama hayo yanasababisha mchezaji asijue makali ya makosa anayofanya, ndiyo maana adhabu hii ikawa kali zaidi.”

BODI YA UKAGUZI YAIPIGA STOP FILAMU YA FOOLISH AGE YA LULU

 
 
 
 
 
Bodi ya ukaguzi wa filamu na michezo ya kuigiza nchini imeipiga stop filamu ya Foolish age ya msanii wa kike mwenye mvuto Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ baada ya kukuta picha zilizo nje ya maadili ya Kitanzania katika filamu hiyo, filamu hiyo ambayo ilipanga kuzinduliwa mwezi huu tarehe 30 katika ukumbi wa Mlimani City inahitaji marekebisho.
 
Kikwazo kilichoikumba filamu hiyo ni nguo fupi zilizotumika katika waigizaji walioshiriki katika filamu hiyo ambayo inatabiriwa kufanya vizuri katika soko la filamu Bongo kama itafanikiwa kuzinduliwa na kuingia sokoni, juhudi zinafanyika kuhakikisha kuwa marekebisho yanafanyika ili kwenda na ratiba kama ilivyopangwa.

Hivi sasa baada ya urasimishaji wa filamu mamlaka na taasisi zinazohusika na masuala ya filamu zimekuwa makini na kuhakikisha kuwa filamu zinazoingia sokoni na zile zinazozinduliwa kukaguliwa kabla ya kufanyika kwa matukio hayo kama ilivyokuwa awali, kama filamu hiyo ya Foolish age itashindwa vigezo vya madaraja yanayotolewa na Bodi hiyo haitaonyeshwa.

Lulu ndio mwigizaji bora wa kike kwa mwaka 2013 kupitia tamasha la filamu la kimataifa la ZIFF katika kipengere cha tuzo za Bongo movie kilichopewa jina la Zuku Bongo movie Awards zilizotolewa katika ukumbi wa Ngome Kongwe.

Soma zaidi: http://mwanahabariuswazi.blogspot.com/2013/08/bodi-ya-ukaguzi-yaipiga-stop-filamu-ya.html#ixzz2cotm3ptI

SHAHIDI KESI YA WEMA AGEUKA ‘BUBU’ GHAFLA


KESI inayomkabili staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ya kudaiwa kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga vibao meneja wa hoteli, Goodluck Kayumbu ilizua kituko baada ya shahidi kugeuka ‘bubu’ ghafla.
Kituko hicho kilijiri Agosti 20, mwaka huu katika Mahakama ya Mwanzo Kawe jijini Dar ambako kesi hiyo inaunguruma.
Mmoja wa makarani wa mahakama hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, alisema kitu kilichoonekana kituko ni pale shahidi wa mwisho aliposhindwa kutoa ushahidi baada ya sauti kukauka ghafla.
 “Mlalamikaji alifika hapa na mashahidi wake watatu, Boniface Mati, Taito Osa na Melao  ambapo wawili walitoa ushahidi lakini Taito alishindwa kutoa ushahidi wake kwani sauti ilikata ghafla na ndipo hakimu Bernice akamuamuru anyamaze na kupanga tarehe nyingine ya kuwasikiliza mashahidi hao,” alisema karani huyo.
Mlalamikaji wa kesi hiyo, alipoombwa na paparazi wetu azungumzie ‘ ishu’ ya shahidi wake kushindwa kuzungumza alisema amekubaliana na uamuzi wa mahakama  na anasubiri tarehe ya kurudi mahakamani ambayo ni Septemba 30, mwaka huu.

WANAUME WANATUPENDA SISI MABONGE



MAKUBWA! Madogo yana nafuu! Wanawake wenye maumbile makubwa wanaofanya biashara haramu ya kuuza miili yao jijini Dar, wamefunguka kwamba wanaume wamekuwa wakiwapenda kwa sababu ya ubonge wao.
Baadhi ya wanawake wenye maumbile makubwa wanaofanya biashara ya kuuza miili yao jijini Dar wanaodai kupendwa zaidi na wanaume.

Mijimama hiyo ilitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati ikizungumza na paparazi wetu aliyekuwa katika oparesheni maalum ya kuhojiana nao ili kujua kinachowafanya wajihusishe na biashara hiyo inayohatarisha maisha yao.
Akizungumza na mwandishi wetu, mmoja wa wanawake hao aliyejitambulisha kwa jina moja la Zainabu anayefanya biashara hiyo maeneo ya Sinza Afrika Sana, alisema umbo lake limekuwa likiwadatisha wanaume kibao.
“Kaka si unaiona hii shepu yangu, hapa kuna mwanaume anayeweza kunipita na kwenda kwa wale vimbaumbau,” alisema Zainabu huku akimuonesha paparazi wetu wasichana wembamba waliokuwa mbele yao.
  Wanawake wanaofanya biashara ya kuuza miili yao  wakiwa kazini.
Mwanamke mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Sara Mashauzi, aliyekuwa katika mawindo ya wanaume wakware na Zainabu alisema: “Mimi nilianza haya mambo baada ya kuachana na mume wangu, sasa kila ninakopita wanaume wakiniona tu huanza kunipigia miluzi na wengine kuniita, sista… sista… hongera…, nikaamua kujiuza ili nipate kipato kwani maisha yalibana sana.”
Sara aliongeza kuwa, wanaume wengi anaotoka nao wamekuwa wakimsifia kwa umbo lake ‘pana’ na kudai kwa siku huwa hakosi shilingi 50,000 na siku nyingine anapata hadi 80,000.
Karibu wanawake wote mabonge waliozungumza na paparazi wetu maeneo ya Kinondoni, Buguruni, Manzese na Oysterbay ambako biashara hiyo imeshamiri walidai maumbo yao yamekuwa yakipendwa sana na wanaume hususan waume za watu.
Paparazi wetu alipomuuliza Sara, Zainabu na mwenzao aliyejitambulisha kwa jina la Sikitu kwamba hawaoni kama wanaharibu soko la wenzao wembamba, kama vile waliambiana jibu wakasema watajiju!
 ...Huyu naye akiwa lindoni.

Baadhi ya madadapoa wembamba waliozungumza na paparazi wetu, waliwafungukia majimama hao na kudai wamewaharibia soko lao na kusababisha wajiuze kwa promosheni.
Gazeti hili linakemea tabia hiyo chafu na isiyofaa katika jamii na kuviomba vyombo husika kupambana na kuwasambaratisha wasichana hao. Mhariri.

CRAZY GK ANAJIANDAA KURUDI RASMI KWENYE GAME

 
Mwanzilishi wa kundi la East Coast Team (ECT) “Crazy Gk” aliyetamba na nyimbo kama sauti ya Manka, miko kumi ya rap, sister sister na simba wa afrika anamipango ya kurudi kwenye game la bongo flava.

Msanii huyo aliyepotea kwa muda mwingi akiwa masomoni sasa anataka kurudi tena kwenye game na atazindua wimbo wake mpya wiki ijayo kupitia radio station tofauti tofauti hapa Tz.

KAULI YA MWASITI KUHUSU ALICHOKISEMA NEY WA MITEGO KWAMBA KIGOMA ALL STARS IMEKUFA



Leo hii msanii na muhasibu wa Kigoma All Stars,  Mwasit Almasi a.ka Mwasiti amezungumza juu ya tuhuma za rapper Ney wa mitego kupitia wimbo wake "nasema nao" kuwa Kigoma All Stars imekufa.
  

  mwasitiamesema"Hahahaaa jamani, unajua mi siendi kujibu hizi mambo, mi sipendi hizo maneno maneno
kurushiana,lakini mi nataka watanzania wajue kitu kimoja, safari hii simjibu Ney, najibu watanzania kwasababu wao ndio wamepelekewa ujumbe, nawaambia watanzania kwamba Kigoma All Stars ni kampuni sio group ya mziki, kigoma all stars ni kampuni ya wanamziki, ingekuwa ni group wangekuwa wanatuona tunafanya kazi wote kila sehem sasa hivi, ile ni kampuni ya wanamziki ambao wanashughuli zao, huwezi kukuta hiyo group nzima iko kwenye  mkoa mmoja inafanya show mfano Fiesta, ni ngumu, ile mtu akipelekwa ni kazi yake binafsi , lakini tukimuhitaji kwenye kazi ya kampuni tutampata, kwahiyo hakuna kitu kinachoitwa kufa kwa kigoma all Stars, kigoma all stars ni kampuni ambayo kila mwana mziki ana share katika ile kampuni, kwahiyo ni ngumu kufa, kila mwanamziki amewekeza pale, kila mwanamziki anajua hapa nina changu kwahiyo ni yake"

MADAWA YA KULEVYA YAWA SABABU YA WATANZANIA 3 KUPIGWA RISASI SOUTH AFRICA

Watanzania watatu wameuawa hivi karibuni jijini Cape Town, Afrika ya Kusini kwa tuhuma za kujihusisha na dawa za kulevya. Watanzania hao walipigwa risasi na kundi la watu waliokuwa wameficha nyuso zao nje ya duka lijulikano kama Maisha Tuck Shop jumanne iliyopita katika barabara ya Veld, Athlone, Cape Town.
 
Watanzania wawili walifariki papo hapo na mmoja kufia hosipitali. Mtu mwingine, raia wa Afrika Kusini, alijeruhiwa vibaya katika shambulio hilo. Mmiliki wa duka la Maisha Tuck, Ashim Nassoro, alisema kuwa aliona kundi la watu wakiwa na bunduki za aina ya AK-47 na pistols wakipiga risasi nje ya duka lake.
Bw. Nassoro alidai waliouawa walikuwa marafiki zake, alisema yeye alikuwa nyumbani na mke wake na mtoto wake, ambapo ni karibu na duka hilo aliposikia milio ya risasi.
 
 “Nilikuwa ndani na nilimwambia mke na mtoto wangu walale chini mpaka milio ya risasi iishe” alisema Nassoro na kuongeza “waliwapiga risasi watu waliokuwa ndani ya nyumba halafu wakaenda kwenye duka. Walipiga risasi watu wawili dukani, mmoja aliyekuwa kwenye geti na mwanamke mmoja aliyekuwa kwenye nyumba.”
Nasroro aliongeza kuwa alikuwa anawajuwa Watanzania hao kwa sababu wote wanatoka Tanzania na wamekuwa wakiishi pamoja tokea walipowasili Cape Town miaka mitano iliyopita. Mtu mwingine aliyeshughudia tukio hilo alisema kuwa waliowauwa Watanzania hao walikuwa hawana wasiwasi na walirudi kwenye gari yao taratibu na kuondoka eneo la tukio.
Kufuatia tukio hilo, polisi ilimkamata Abdus Salaam Ebrahim ambaye ni kiongozi wa kikundi kinachopiga vita dhidi ya uhalifu na madawa ya kulevya nchini humo kinachojulikana kama People Against Gangsterism and Drugs (Pagad). Abdus Salaam Ebrahim amefikishwa mahakami leo kwa mashtaka ya mauaji.
Hata hivyo, mahakama imeyaondoa mashtaka hayo kwa muda kufuatia ombi la mwendesha mashtaka ili kuruhusu uchunguzi zaidi kufanyika. Wakati hakimu akiyandoa mashtaka hayo, wafuasi wa kikundi hicho cha Pagad waliokuwa wamejazana mahakamani hapo walishangilia huku wakisema “Allahu Akbar”. Majina ya Watanzania waliouawa hayakuwekwa kwenye charge sheet.
Pagad ni kikundi kilichoanziswa mwaka 1995 kupambana na uhalifu na madawa ya kulevya kwenye jiji la Cape Town baada baada ya juhudi za serikali kulegalega. Kampeni ya kikundi hiki ilianza mwaka 1996 baada kumkamata, kumpiga na kumchoma moto hadi kufa Rashaad Staggie ambaye alikuwa kiongozi wa kikundi cha uhalifu jijini Cape Town. Serikali ya Afrika Kusini ilishawahi kudai huko nyuma kuwa Pagad ni kikundi cha kigaidi baada ya kudaiwa kulipua kwa bomu hoteli ya Planet Hollywood mwaka 1998. Hata hivyo, Pagad ilipinga kuhusika kwenye shambulio hilo.
Kikundi hiki kilipotea lakini kikaja kuibuka tena kuanzia mwaka 2011 na kampeni yake ya kuchukua mitaa inayotawaliwa na uhalifu na biashara ya madawa ya kulevya. Wadadisi wa mambo wanadai kuwa kurudi tena kwa Pagad kwa gia ya kupambana na uhalifu, hasa madawa ya kulevya, itafanya hali kuwa mbaya hasa kwenye jimbo la Western Cape.
Hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la milipuko ya mabomu kwenye sehemu zinazouza magari na pia kwenye nyumba za makazi ya watu zilizopo Athlone na maeneo mengine jijini Cape Town. Matukio haya yamekuwa yakitokea zaidi kwenye nyuma za makazi zinazotuhumiwa kutumika kufanyia biashara ya madawa ya kulevya. Kikundi cha Pagad kimekanusha kujihusisha na matukio hayo.

MSANII MANAIKI SANGA ALIYEPIGA PICHA ZA UCHI ATIWA MBARONI, ASKARI WAMKAMATA KIMAFIA HUENDA IKWA NDIO MWISHO WAKE ....................DUUUUUU

PICHA ZA UCHI ZIMPONZA

Tunaomba radhi kwa picha zilizopo katika habari hii huwenda zisikufurahishe
 
 




















Pacha wa Lulu Diana Kimario " Mikogo" huyu







Huyu bint inasemekana ni mwanafunzi wa chuo ambae ni raia wa Kenya anaesoma nchini pia ilidaiwa ni mtoto wa Waziri mmoja nchini humo



Huyu nae amewahi kupangiwa chumba na Manaiki maeneo ya Sinza na wakaishi zaidi ya mwaka mmoja kama mume na mke!

Msichana ambae inasemekana aliwahi kunusurika kunywa sumu kwa ajili ya penzi la Manaiki mmh.









Ushahidi hadharani na sijui kama walikuwa wanaigiza kweli? na kama walikuwa wanaigiza ni filamu gani ya utupu?


Irine Kanka Miss Temeke mwaka juzi akiwa kwenye himaya ya Manaiki kama wanavyoonekana sijui walikuwa wanaigiza au laa!

Huyu mwingine hakufahamika jina lakini nae kesha pitiwa na Manaiki.




Msanii Skaina ambae inadaiwa amewahi kuishi kinyumba na Manaiki kabla ya kuolewa na kuachika tena!

Mrembo wa Facebook na Manaiki

Msanii chipukizi kwenye kiwanda cha filamu Bongo aliyefahamika kwa jina la Suzy akichezea .....

Picha hizi hazina mafunzo kwetu bali Mmh haya yetu macho sisi.

Manaiki na Dida wakifurahia maisha

Huyu nae hakufahamika jina lake mara moja lakini yuo kwenye mnyororo wa Manaiki.

Mrembo ambae sio staa aliyejulikana kwa jina la Zachia akiwa chumbani muda mfupi baada ya kuduu na Manaiki.

Msanii Skaina katikati ambae nae amingizwa kwenye orodha ya wachumba wa Manaiki Sanga.


Msanii Manaiki Sanga akiwa na mwanamuziki maarufu toka Zanzibar Dida wakila bata za ufukweni kama wanavyoonekana!


Jeshi la polisi kanda ya Dar es Salaam linadaiwa kumtia mbaroni msanii anaetuhumiwa kupiga picha chafu na wanawake mchanganyiko wakiwema mamiss maarufu na baadae kusambaza kwenye mitandao yote ya kijamii pamoja na kuripotiwa kwenye magazeti pendwa.

Gazeti hili katika upekenyuaji wake limenasa picha hizi kwenye mtandao mmoja maarufu wa kijamii ukimuonesha Manaiki akiwa kwenye kibano kikali cha polisi huku akiwa amevishwa pingu na kurukishwa kichurachura.

Habari za uhakika  zinasema kuwa msanii huyo aliyeshiriki kwenye filamu za Tikisa, Love Position, Last Coin na Sory my Soni alikamatwa siku chache baada kuvuja kwa picha zake za aibu zikimuonesha akiwa na wanawake tofauti tofauti.

Aidha picha zaidi za tukio hilo la kukamatwa kwa Manaiki na haikufahamika kama alikamatwa kwa kosa jingine tofauti na kosa la kudhalilisha wanawake ambapo hali hiyo iliwalazimu waandishi wetu kufatilia kwa ukaribu tukio hilo la kukamtwa kwa msanii huyo aliyejitapia usataa kwa matukio ya picha za uchi .

Timu ya waandishi wetu ilifika kituo cha Polisi Buguruni kwa ajili ya kufahamu kama msanii huyo alikuwa ameswekwa kituoni hapo lakini kwa bahati mbaya hakuwepo. Ambapo gari la mapapalazi weti ilielekezwa kituo cha Polisi Oysterbay kwa ajili ya kuonana na RPC wa Kanda ya Kinondoni Wambura lakini pia kwa bahati mbaya mara baada ya kufika ofisini kwake sekritali wake alisema kamanda hakuwepo kwa muda huo.


Alipotafutwa msanii huyo kupitia simu yake ya kiganjani ili kujuwa nini kilimsibu lakini hakuweza kupatikana kwani simu yake ilikuwa haipatikani kabisa licha kupigwa zaidi ya mara sita.

Aidha kukamatwa kwa Manaiki kumeleta tafsiri tofauti kuwa huenda Rais wa Miss Utalii Tanzania Gidion Chipungahelo anahusika kufuatia kauri yake aliyoitoa kwenye la Kiu la wiki iliyopita kuwa lazima ataanza kumshughulikia Manaiki ili iwe fundisho kwa wale wote wanaosubiri kuwafanyia skendo chafu warembo wake. Hata hivyo licha waandishi wetu kufatilia habari hiyo karibu siku nzima lakini hapakuwa na taarifa sahihi za wapi alipo Manaiki na kituo gani cha Polisi alichoswekwa ambapo  juhudi nyingine za kufika nyumbani kwa msanii huyo na baadae tutawaletea taarifa kamili. 

WAZAZI WATOA KAURI NZITO: 
Baada ya wiki iliyopita tumepokea maoni mbalimbali ya wananchi hasa wazazi wenye uchungu na wa watoto wao na walifunguka mengi sana fuatilia ujue kauri zao.

Mama Amina wa Mbezi Beach alisema “ Jamani hivi huyo msanii ana wazazi kweli? Hapana binafsi siamini kama anao kwani udhalilishaji anaoufanya kwa watoto wa watu kama angekuwa na wazazi hakika wangemkanya na angeachana na huo upuuzi nasema hii haikubariki kabisa tunamuomba Kamanda Kova amshughulikie kijana huyo ili iwe fundisho kwa wengine” Alisema mama huyo kwa uchungu

Nae Mama Mud wa Sinza Jijini Dar alifunguka hivi “ Unajua huyu Manaiki mimi ni mmoja wa mashabiki wake kwenye muziki wa bongo flava sasa nashindwa kuelewa kwa nini amejidhalilisha kwa picha chafu kama hizo? Sio bure mi nadhani anahitaji ushauri nasahaa kwani huenda sio akili yake haki ya Mungu” Alisema

Aidha nae msanii mkongwe wa tasinia ya filamu nchini Mzee Magali alitoa ushauri kwa Manaiki na kusema“ Huyu motto ana kipaji kizuri sana kwenye kuimba kuigiza sasa ni nini kinachomfanya ajidhalilishe kiasi hiki dar kweli imeuma sana kuona kijana wangu anavyopotea, Kwani sasa hivi tunahitaji kudhalisha akina mzee Chilo wapya. Akina mzee Magali wapya sasa kwa mtindo huu hakika hawa vijana hawatofika mbali na sanaa” Alisema sema kwa uchungu

Aidha nae Hemed Kavu meneja wa Club Maisha ya Dar alikuwa na haya “ Mimi nimepiga simu hapo kuwaeleza kuwa nimesikitishwa sana na tabia ya Manaiki ambapo kwenye hizo picha pia yupo mpwa wangu ambae anasema alishawishiwa na Manaiki kupiga hizo picha hivyo kama familia tutakaa chini kuangalia namna ya kumshitaki ili amradi ushahidi toka kwa muhusika upo kuwa kulikuwa na ushawishwaji wakati wa kupiga picha hizo toka kwa Manaiki ambae alimrubuni kumpa laki mbili akishapiga picha hizo” Alisema Hk

Nae mwalimu wa wasanii wengi nchini n director wa filamu Tanzania aliyejitambulisha kwa jina moja la Bakari alilonga “ Hapo mimi ninachokiona hao wote wana makosa kwani hapo hakuna mtoto mdogo hao mabint nao viherehere vyao viliwaponza hivyo kama Manaiki alifanya kwa kuwafunga kamba hapo sawa ana haki ya kuhukumiwa jamani lakini hao wanawake walijitakia wenyewe basi walaumiwe wote” Alisema