Pages

Translate

Monday 30 September 2013

AKAMATWA NA MFUKO WA BANGI SOKONI

Kijana ambaye hakutambulika jina lake mara moja amenaswa na polisi akiwa na mfuko wa bangi. 

Sakata hilo limetokea maeneo ya Buguruni Sokoni jijini Dar es Salaam mara baada ya polisi kumshuku jamaa huyo ambaye alionekana kujificha chini ya matenga ya nyanya mara baada ya kuwaona polisi hao.
Polisi wakikagua mahali alipokuwa amejificha mtuhumiwa wa bangi.
Mfuko wa bangi aliokamatwa nao mtuhumiwa.
Mtuhumiwa akipelekwa kutuo cha polisi.

AKAMATWA NA MFUKO WA BANGI SOKONI

Kijana ambaye hakutambulika jina lake mara moja amenaswa na polisi akiwa na mfuko wa bangi. 

Sakata hilo limetokea maeneo ya Buguruni Sokoni jijini Dar es Salaam mara baada ya polisi kumshuku jamaa huyo ambaye alionekana kujificha chini ya matenga ya nyanya mara baada ya kuwaona polisi hao.
Polisi wakikagua mahali alipokuwa amejificha mtuhumiwa wa bangi.
Mfuko wa bangi aliokamatwa nao mtuhumiwa.
Mtuhumiwa akipelekwa kutuo cha polisi.

Sunday 29 September 2013

BIBI AMUUA MJUKUU WAKE KISA KACHELEWA KULETA MWIKO WA UGALI

Mtoto wa kike aliyetambulika kwa jina moja la Zuhura (6) mkazi wa mtaa wa Lulumba New Kiomboi mjini, wilayani Iramba,amefariki dunia baada ya kudaiwa kuuguzwa kwa maji ya moto na bibi yake Magreth Sombi (55).

Imedaiwa kwamba Zuhura alimwagiwa maji ya moto ambayo yalikuwa yatumike kupikia ugali,kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kitendo cha mtoto huyo kuchelewa kukabidhi mwiko aliotumwa na bibi yake.

Akisimulia mkasa huo wa aina yake,Mwenyekiti wa mtaa wa Lulumba,Abel Seit,amesema tukio hilo limetokea Septemba 24 mwaka huu majira ya jioni huko mtaa wa Lulumba katika mji wa New Kiomboi.

Amesema siku ya tukio,Zuhura alitumwa na bibi yake Magreth akalete mwiko wa kusoga ugali wa jioni na inadaiwa kwamba mtoto huyo alichelewa kuukabidhi mwiko huo.

Seit amesema baada ya kuleta mwiko huo,alimwagiwa mwilini maji yaliyokuwa yamechemka tayari kwa kutumika kupikia ugali wa jioni.

“Kama vile adhabu hiyo haikutosha,Magreth kwa ushirikiano na mtoto wake Naomi,walimkamata kwa nguvu Zuhura na kisha kuingiza viganja vyake vya mikono yote ndani ya sufuria iliyokuwa ina maji yaliyokuwa yamechemka kwa kiwango cha juu.Mtoto Zuhura aliweza kuugua na nyama zote kutoka na kubakia mifupa”amesema kwa masikitiko mwenyekiti huyo.

Seit amesema Zuhura alifariki dunia Septemba 25 akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya ya Iramba.

“Baada ya muda mrefu kupita baada ya Zuhura kufariki dunia,bibi yake Magreth alimtuma mtoto wake Naomi kuja nyumbani kwangu kunipa taarifa hiyo.Cha ajabu ni kwamba hawakupiga yowe wala kutoa taarifa kwa majirani zao”,amesema na kuongeza;

“Nilipomhoji ni kwa nini hajawajulisha majirani zao juu ya kifo hicho,kwanza alinionya kwamba nisije nikawaambia watu wala majirani kwa sababu hataki watu wajue au waje warundikane kwake na kwamba mwili wa Zuhura wakati wo wote utachukuliwa na wazazi wake kwenda kuzika Singida mjini”.


Kwa upande wake jirani wa karibu wa Magreth,Elieza Mgwali,amesema Zuhura ambaye ana miezi miwli toka aanze kuishi na bibi yake,aliishi kwa mateso makubwa.

“Mtoto huyu ameteseka mno toka aanze kuishi na bibi yake,alifanyishwa kazi ambazo ziko nje ya uwezo wake na mara nyingi alikuwa akinyimwa hata chakula.Mara nyingi tu tulikuwa tunashitukia anaingia kwetu na kwenda moja kwa moja jikoni na kujichukulia chakula bila hata kuomba.Kwa sababu tuliisha tambua mateso yake,tulikuwa tukimruhusu ale hadi ashibe”,alisema.

Majirani wa Magreth wamepigwa butwaa kutokana na kitendo hicho kufanywa na mama ambaye alikuwa hakosi kanisani na alikuwa mwimbaji mzuri wa kwaya.”Kumbe chui aliyekuwa amevaa ngozi ya kondoo”,alisikika mama mmoja ambaye alidai kuwa walikuwa wakisali na Magreth.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa mtaa,Magreth na mtoto wake Naomi,wanashikiliwa na polisi kuhusiana na mauaji hayo.

Juhudi kubwa zimefanywa na mwandishi wa habari hii kupata undani wa mauaji hayo,hazijaa matunda baada ya kumpigia Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida kupitia namba yake ya simu ya mkononi kuita bila kupokelewa na hata meseji ilipotumwa nayo haikuweza kujibiwa
Mwenyekiti wa mtaa wa Lulumba New Kiomboi mjini wilaya ya Iramba, Abel Seit akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya tukio la mtoto wa kike Zuhura (6) kumwagiwa maji ya moto na bibi yake Magreth Sombi (55) na kusababisha kifo chake.
Mwenyekiti wa mtaa wa Lulumba New Kiomboi mjini wilaya ya Iramba,Abel Seit akifungua mlango wa nyumba ya Magreth Sombi ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kumuuguza mjukuu wake Zuhura na kusababisha kifo chake.
Sehemu ya ndani ya nyumba ya mtuhumiwa Magreth Sombi anayedaiwa kumuuguza mjukuu wake maji ya moto na kusababisha kifo chake.
Picha na mtoto wa mtuhumiwa Magreth Sombi,Naomi ambaye hivi karibuni amehitimu mafunzo ya ualimu mkoani Tabora na alikuwa anasubiri kupangwa kazi.Kwa sasa Naomi na mama yake Magreth Sombi wanashikiliwa na jeshi la polisi wilaya ya Iramba kuhusiana na mauaji ya Zuhura.
Picha ya mtuhumiwa Magreth Sombi anayetuhumiwa kumuua mjukuu wake Zuhura kwa kumumwagia maji ya moto ambayo yaliyokuwa yatumike kupikia ugali wa jioni.(Picha zote na Nathaniel Limu).

Friday 27 September 2013

BINTI WA DARASA LA 5 ABAKWA NA BABA MZAZI KWA MIEZI 9


 Binti wa umri wa miaka 15 tunayemtambulisha kwa jina moja tu la Zaina, mkazi wa Kimara jijini Dar ameamua kufunguka na kusimulia jinsi alivyokuwa akibakwa na baba yake mzazi aliyemtaja kwa jina moja la Mohamed.
  
ANAANZA KWA KUANIKA HISTORIA YAKE FUPI!
Akisimulia kwa uchungu, Zaina alianza kwa kuanika historia yake kwa ufupi kwamba tangu atoke tumboni, hakuwahi kumuona mama yake zaidi ya kuoneshwa kwenye picha tu!
 

Akasema hiyo yote ilitokana na hadithi aliyowahi kusimuliwa kwamba, akiwa kichanga, baba huyo alimuiba kwa mama yake anayeishi Kigamboni, Dar na kwenda kumlea Kimara kwa ushirikiano na mama yake wa kufikia.
  
Lakini akasema: Hata huyo mama wa kambo mwaka jana aliachana na baba baada ya kutufumania chumbani mimi na baba, akakasirika na kuondoka zake.

SIKIA FILAMU KAMILI SASA
“Nakumbuka ilikuwa mwanzoni mwa mwaka jana, nikiwa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kimara ndipo baba alipoanza tabia ya kunilazimisha tufanye mapenzi. Alisema anataka tufanye kwa njia ya kawaida na ya kinyume na maumbile.
 
“Nilikataa lakini akawa ananilazimisha na vitisho juu. Tulianza kwa kufanya mchezo huo na baba lakini si kwa kupenda kwangu, nililazimika kwa sababu niliamini ni baba ambaye anaweza kunifanya lolote kama nitakataa, mbaya zaidi hakuwa akitumia kinga,” alisema na kuongeza:
 
“Kuanzia hapo, zoezi hilo liliendelea kila siku hadi mwishoni mwa mwaka jana nilipoamua kutoroka na kwenda kuwaeleza ndugu wa baba, kule Tanga.” 

Binti huyo alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa,  kilichomsukuma kutoroka ni mateso, ukatili na udhalilishwaji uliopitiliza kwani baba yake wakati akimwingilia alikuwa akimkaba kooni ili asipige kelele.
 

“Yeye alijua anafanya kosa, akawa akiniingilia huku ananikaba koo nisipige kelele. Nilikuwa nasikia maumivu makali balaa,” alisema binti huyo.

ALIWAAMBIA MAJIRANI LAKINI WALIOGOPA KUMVAA BABAKE
“Kingine kilichonifanya nitorokee Tanga kuwaambia ndugu zake ni kwamba, niliwahi kuwaambia majirani kuhusu mchezo wa baba lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza kwa vile wanamuogopa,” alisema.

MAMA MZAA BABA AAMBIWA KILA KITU
Zaina alizidi kusema kuwa, baada ya kufika Tanga  alimweleza kila kitu bibi yake (mama mzaa baba’ke). 


Bibi huyo kwa sababu ni mzazi alimwita mwanaye na kumkanya kisha akafanyiwa mambo ya kimila ili kuondoa balaa hilo la baba mtu kutembea na mwanaye wa kumzaa la sivyo kwa mila za kwao ukoo mzima ungesambaratika.

BABA MTU AONDOKA TANGA USO UMEMSHUKA, YEYE AGOMA
“Baada kufanyiwa mambo ya mila, baba aliniambia turudi Dar lakini nilikataa kwa sababu niliamini tutakapofika bado atataka kuniingilia tena. Nasema hivyo kwa sababu pia baba amewahi kufanya mapenzi na dada’angu anaitwa Hamida mpaka akampa mimba.
 

“Huo ukatili wote alikuwa akitufanyia kwa nyakati tofauti tofauti, dada alipopata mimba siku moja alimwibia fedha ili akaitoe, alifanikiwa na akakimbia nyumbani, sijui alipo,” alisema.

Akaendelea: Basi, niliamua kubaki kwa bibi, lakini kuna siku alikuja mtu aliyekuwa anatafuta msichana wa kazi ‘hausigeli’, mimi nikakubali, nikaenda Moshi ambako nilikaa kwa muda.

 

“Hivi karibuni nilirudi Dar na kufikia kwa jirani, sikutaka kwenda nyumbani kwa baba, namuogopa atataka tena. Huyu jirani niliyefikia kwake, mtoto wake ni rafiki yangu tulikuwa tunasoma naye. Hapa nilipo natafuta msaada wa kumpata mama yangu mzazi. Kama atabahatika kulisoma gazeti hili namuomba anifuate jirani na kwa baba atanipata,” alisema Zainab.

Zainab hakuishia kwenye kufikia kwa jirani tu, anasema akiwa hapo jirani huyo kesho yake alimpeleka serikali za mitaa ili kutoa taarifa kuwa amerudi kwa vile alitafutwa kwa muda mrefu kwenye shule aliyokuwa akisoma.

MWENYEKITI WA MTAA AKIRI ZAINAB KUBAKWA NA BABA’KE
Naye mwenyekiti wa mtaa wa eneo hilo, Demetrius alikiri kumpokea mtoto huyo na kumsimulia yote kuhusu baba yake ambapo aliambatana naye hadi Kituo cha Polisi Mbezi kwa Yusuf kwa lengo la kutoa taarifa ili mzee huyo achukuliwe hatua za kisheria. Alisema binti huyo alifunguliwa jalada la kesi KMR/RB/114/2013  UCHUNGUZI.

BABA ANASEMAJE?
Baada ya kumalizana na binti huyo aliyeungwa mkono na mwenyekiti huyo, mapaparazi wetu walizungumza na baba mtuhumiwa ambapo alikuwa na haya ya kusema:


“Si kweli, huyo mtoto ananisingizia tu, mimi siwezi kufanya kitu kama hicho na binti yangu wa kumzaa hata siku moja.

BABU WA KIKOMBE CHA LOLIONDO AWA KIJANA.


Sasa maisha ni mepesi baada ya kukusanya mamilioni ya pesa wakati wa kikimbe akichodai alioteshwa na Mungu


MWANAUME AMPIGA MKEWE BAADA YA KUMFUMANIA GESTI

Hapa akiwa amelala hajitambui baada ya kupata kipigo
Hapa wananchi wakiwa wanashudia jamaa akimpa kichapo mkewe baada ya kumfumania
    Picha hii jamaa amembeba mke wake baada ya kumfumania na kumpa kipigo kikali wakielekea nyumbani
Tukio hili limetokea leo asubuhi mida ya saa 8.00,katika mji wa Iringa maeneo ya mwangata paparazzi wetu alifanikiwa kulinasa hili tukio.Jamaa mmoja jina halikuweza kupatikana amemfumania mkewe gesti baada ya kumfumania alichokifanya ni kumruhusu yule mwanaume aliyemfuma na mke wake nakusema jamaa hana kosa mwenye kosa ni mke wake.Jamaa akazidi kufunguka nakusema mke wake alitakiwa kukataa alipotongozwa moja kwa moja mke wangu ndiye mwenye makosa huyu mgoni hana kosa kabisa.Kilichofuata baada ya hapo alimpa kichapo kikali kama unavyoona kwenye picha. Mwisho wa siku akambeba na kurudi naye nyumbani maeneo ya mwembetogwa ili kumfungashia mizigo yake na kumrudisha kwa wazazi wake.

WARIOBA AIUMBUA CCM KWA KUANIKA MAZITO


Warioba aiumbua CCM
• Asema muswada uliopitishwa bungeni unalenga kuifuta tume yake

na Irene Mark
Tanzania Daima

MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba, amesema Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013 uliopitishwa na Bunge hivi karibuni unalenga kuifuta tume hiyo kabla ya kumaliza muda wake.

Muswada huo ambao ulipitishwa na wabunge wa CCM pamoja na Augustine Mrema wa TLP (Vunjo), ulisusiwa na wabunge wa CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi kutokana na kuchakachuliwa baadhi ya vipengele huku Zanzibar ikiwa haijashirikishwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Jaji Warioba alisema miongoni mwa vipengele vilivyofanyiwa marekebisho kwenye sheria hiyo ni kile kinachotaka tume yake ivunjwe baada ya kuanza kwa Bunge la Katiba.
Hoja za Warioba ndizo hizo zinazopigiwa kelele na vyama hivyo vitatu pamoja na makundi ya asasi za kiraia huku viongozi wa serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakiwabeza na kudai muswada huo ulipitia taratibu zote.

Alisema marekebisho hayo yanakwenda kinyume cha sheria mama iliyounda tume hiyo ambayo inaweka wazi kwamba majukumu ya tume yatafika ukomo baada ya kupigwa kura ya maoni.
Kwa mujibu wa Jaji Warioba, uamuzi wa wabunge hao utaleta mkanganyiko endapo watashindwa kuelewana kwenye baadhi ya vipengele, kwani hapatakuwa na mtu wa kuwafafanulia, kwa kuwa tayari tume itakuwa imevunjwa.

“Sheria iliyounda tume hii inasema wazi kwamba ukomo wa tume ni baada ya wajumbe wa tume hiyo kutoa elimu kwa umma kuhusu kura ya maoni na mchakato wa kupiga kura hiyo utakapokamilika.
“Wao hawaoni sababu ya sisi kuendelea kuwapo hapa, nawaomba watafakari kipengele hicho,” alisema Warioba aliyepata kuwa waziri mkuu wa Tanzania.

Kabla ya kuhitimishwa kwa mkutano wa 12 wa Bunge mjini Dodoma, wabunge wa upinzani walitoka nje wakisusia kupitishwa kwa mabadiliko ya sheria hiyo, wakidai kufutwa kwa baadhi ya vipengele vilivyobadilishwa dakika za mwisho bila kuwahusisha.
Kususa huko wakati kikao kinaendelea kuliambatana na vurugu baada ya Naibu Spika, Job Ndugai, kuwataka askari wa Bunge kumtoa nje Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe, jambo lililowafanya wabunge wa vyama hivyo vitatu kutoka wote.

Pamoja na madai hayo, wabunge hao walilalamikia utendaji wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia Katiba na Sheria chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Viti Maalumu, Pindi Chana, kwa kubadili vipengele hivyo kabla ya kuupitisha bungeni.
Baada ya wabunge wa upinzani kususa, wabunge wachache wa CCM waliokuwapo ukumbini hapo na Mrema, walipitisha mabadiliko hayo na kuyapeleka kwa rais ili asaini na kuifanya kuwa sheria.

Nje ya Bunge
Moto uliowashwa nje ya Bunge na viongozi wa upinzani pamoja na makundi ya asasi za kiraia umebadili upepo kwani kelele za kumtaka Rais Jakaya Kikwete kutousaini muswada huo zimezidi kuongezeka.
Ni katika hatua hiyo, mawaziri kadhaa, William Lukuvi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Stephen Wasira na Mathias Chikawe wa Katiba na Sheria, wamekuwa wakiendelea kuwabeza wapinzani.

Hivi karibuni Waziri Chikawe alifikia hatua ya kumtisha Rais Kikwete akisema kuwa endapo hatausaini muswada huo kuwa sheria atakuwa ametangaza mgogoro na Bunge.
Pia Wasira naye amenukuriwa akisema kuwa wanaopinga muswada huo usisainiwe lazima wampe rais sababu za kutofanya hivyo, kwa vile hana, na kwamba milango ya Ikulu kwa wapinzani hao kujadiliana na mkuu wa nchi imefungwa.

Matamshi hayo ndiyo yamewaleta pamoja viongozi wa vyama hivyo na makundi mengine wakizunguka kwa wananchi kuwaeleza karoso zilizomo kwenye muswada huo ambao CCM inataka kutumia turufu hiyo kuhodhi mchakato wa Katiba mpya.

Angalizo la Warioba
Mwenyekiti huyo aliwataka wanasiasa kuacha malumbano katika mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya, huku akikanusha uvumi kwamba baadhi ya wajumbe wa tume hiyo wametishia kujiuzulu.
Badala yake aliwataka waketi pamoja na kukubaliana kuhusu vipengele wanavyotofautiana kwenye rasimu hiyo, kisha kuwaeleza wananchi manufaa ya kuwa na Katiba ya wote.

“Huu si wakati wa Tanzania kutengana, wanasiasa wanapaswa kutumia fursa walizonazo kukaa pamoja na kushirikiana ili tupate Katiba bora, hatuwezi kupata Katiba kwa maandamano, mikutano na mivutano baina ya vyama vya siasa,” alisema.
Kwa mujibu wa jaji huyo, kilichopo kwenye rasimu hiyo ni maoni ya wananchi, hivyo hakuna haja ya kubadili, bali kuboresha ili kila Mtanzania anufaike na uwepo wa Katiba hiyo.

Alifafanua kuwa kuna baadhi ya wajumbe wa mabaraza walidiriki kuwakashifu wajumbe wa tume yake, hasa kutokana na wanasiasa kutoa matamshi ya kuwalenga wajumbe hao wa tume.
“Hilo limetusikitisha, matamshi hayo yalitolewa kwa lengo la kuwadhalilisha wajumbe wa tume na kuishushia thamani kazi kubwa wanayoifanya ndani ya tume,” alisema.
Jaji Warioba alisema pamoja na changamoto hizo, tume ilifanikiwa kukamilisha mchakato huo ambapo kwa kupitia mikutano 179 ambayo ilihudhuriwa na wajumbe 19,337 wa mabaraza ya Katiba walipata maoni.
Mbali na hatua hiyo, Jaji Warioba alisema tume imepokea maoni kutoka kwa makundi, asasi na taasisi mbalimbali 600 kuhusiana na rasimu ya Katiba mpya.

Alisema baada ya kukusanya maoni hayo, tume inatarajia kuanza mchakato wa kuchambua ili kuandaa ripoti itakayokuwa na maboresho na kuikabidhi kwa rais kwa ajili ya kuendelea kwa mchakato mwingine.
“Tumewahoji wawakilishi wa wananchi kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania Bara na Visiwani, zaidi ya vikundi 176 vyenye uwakilishi wa watu tofauti tulikusanya maoni yao.
“Naamini Watanzania wanataka Katiba inayoheshimu utu wa mtu, umoja na kuvumiliana,” alisisitiza Jaji Warioba.

Thursday 26 September 2013

AJALI MBAYA YAJERUHI TABORA


Mwili wa kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Rashidi Seleman mkazi wa Isevya manispaa ya Tabora ambaye amepoteza maisha baada ya Lori walilokuwa wamepanda kuanguka eneo la Inala barabara ya kwenda Kigwa,Polisi wamesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva ambaye amekimbia huku watu wengine wanne wakiwa wamejeruhiwa vibaya ambao wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Kitete.
Tatizo la ukosefu la ukosefu wa vifaa vya kuokolea vilisababisha maiti ya mtu huyo kukaa muda mrefu akiwa amebanwa na Lori hilo ambalo ni mali ya kampuni ya mkandarasi JOSSAM
Awali jitihada za Polisi na wananchi ziligonga mwamba na kubaki wakiiangalia maiti hiyo pasipo msaada wowote ajali ambayo imetokea majira ya saa kumi jioni hapo jana.
Askari wa usalama barabarani wakiongozwa na kamanda wa Polisi kikosi cha usalama barabarani wilaya ya Tabora Bw.Swaleh Digega hatimaye wakafanikiwa kuutoa mwili wa marehemu huyo na kuupeleka hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete kwa ajili ya kuuhifadhi....Hata hivyo Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Sumatra wanakusudia kumfikisha mahakamani mmiliki wa Lori hilo kwa kitendo cha kusafirisha mizigo na wanadamu katika gari hilo lenye nambari za usajili T 702 ACR ambalo ni ISUZU TX

INASIKITISHA!!!!!!! BAADA YA KUZALIWA MAMA YAKE HAMTAKI KUTOKANA NAKUTOKUWA TAYARI KUMLEA

 

Ni katoto ka kike kenye afya teleee na ana siku tatu tu toka kuzaliwa.Bahati mbaya amezaliwa katika mazingira ambayo mama yake hayupo tayari kumlea na ilikuwa amtupe wasamaria wema wakaokoa jahazi.
Mama wa mtoto ndio huyu pichani anadai hana wazazi walifariki.Akawa analelewa na dada yake huko Sinza na akapata ujauzito.Baada ya kupata ujauzito dada akamfukuza nyumbani na aliyempa ujauzito akamkataa.
Kina mama pichani wakimwogesha mtoto baada ya kuzuia zoezi la mama kutupa mtoto
Inavyosemekana mama wa mtoto alienda dispensary kuchoma sindano mimba itoke.Bahati nzuri mtoto siku zilikuwa zimetimia akamzaa.Alipozaliwa na kuwa hai mama mtoto akawa hamtaki anataka kumtupa.Mama wa mtoto hamtaki kabisaaaa mwanae.
Kina mama baada ya kuzima zoezi la mtoto kutupwa wakakaa na binti kuelewa nini kinamsibu.Wakamuogesha mtoto na mama yake pia akaogeshwa.Akapewa maneno ya kumsaidia kisaikolojia lakini haikusaidia mama msimamo wake ukawa ule ule.Mama aliyekuwa akimuogesha mtoto yupo radhi kumchukua mtoto na kumlea kama wa kwake maana mama yake hamtaki.
Niliwahi kuona movie zamani inafanania na hili binti mdogo alipata ujauzito lakini hakuwa tayari kuwa mama na akamtoa mwanae kwa mtu na mkewe waliokuwa wanamatatizo ya kupata mtoto.Alimtoa kwasababu yeye asingeweza kulea na kumpa mahitaji yote.Yule baba na mkewe ndio walikuwa wakihitaji mtoto zaidi yake.

MFANYABIASHARA AFUMWA NA MKE WA MTU GESTI ALIA KAMA MTOTO

 Jamaa mmoja aliyetajwa kwa jina moja la Manfree,  Jamaa mmoja aliyetajwa kwa jina moja la Manfree,  mkazi wa Kimara Mwisho, Dar ambaye inadaiwa ni  mfanyabiashara wa baa iliyopo Mbezi Mwisho (Mbezi Shamba) anadaiwa kunaswa na mke wa mtu (jina tunalo).


Manfree baada ya kunaswa na mke wa mtu.

Kwa mujibu wa mashuhuda, tukio hilo lililoongeza faraja na furaha ya shetani kule kuzimu, lilijiri juzikati huko Kimara Mwisho ndani ya gesti moja (jina lipo kwenye droo zetu).

Akizungumza kwa uchungu mkubwa, mume wa mwanamke huyo ambaye hakupenda jina lake liupambe ukurasa huu, alisema siku nyingi Manfree amekuwa akimsumbua mke wake, hali iliyokuwa ikimpa wakati mgumu mwanamme huyo mwenye mke.

“Jamaa amekuwa akimsumbua sana mke wangu, nilipokuja kuzipata taarifa hizi nilishangaa sana lakini pia niliumia kama mwanamme,” alisema mwenye mke huyo.

Mwenye mke (kushoto) akiongea na mke wa mtuhumiwa.

Kwa mujibu wa mume huyo, kufahamiana kwa Manfree na mkewe kulikolea zaidi baada ya mwanamke huyo kuhitaji fremu kwa ajili ya biashara ya duka ambapo kwa kutumia uenyeji wa jamaa huyo, alionesha kutaka kumsaidia.

Mwanamme huyo aliendelea kusema kuwa sinema ya kunaswa kwa mwanamme huyo ilianza siku moja baada ya yeye kwenda kwenye baa ya jamaa huyo kuangalia mpira (hakuzitaja timu).

Alisema akiwa hapo baa, mara mke wake alitokea na kukaa kwenye kiti, meza nyingine. Jamaa huyo naye akaenda kukaa na mke wa jamaa na kuanza kuzungumza.

Nguo za Manfree zikiwa zimetundikwa chumbani.

“Mimi sikujua walichokuwa wakikizungumza na wala sikuwa na wasiwasi kwa vile jamaa ananifahamu, anafahamu yule ni mke wangu na anawafahamu hadi watoto wangu,” alisema mwanamme huyo.

Akaongeza: “Tulipofika nyumbani, mke wangu akasema amesikia mimi nina wanawake wengi nje, nimewafungulia biashara na mambo mengine kibao.

“Nilimuuliza ameambiwa na nani, akawa anagomagoma kunijibu lakini nilipombana sana mwisho akamtaja jamaa. Kumbe alipokaa naye pale baa ndiyo alikuwa akimwambia uongo huo.

“Mke wangu akaongeza kusema kuwa jamaa huyo kwa muda mrefu amekuwa akimtaka wakutane ‘praiveti’ lakini yeye amekuwa akimkatalia kwa sababu analinda heshima ya ndoa yake.

“Mke wangu alinionesha meseji ambazo jamaa alikuwa akimtumia, niliumia sana. Kwa kweli inauma sana jamani hasa kitendo hicho kufanywa na mtu ambaye mnafahamiana!”

Kwa mujibu wa mwanamme huyo, hali hiyo iliendelea kuisumbua ndoa yake huku maneno ya Manfree yakizidi kumvuruga kichwani.

Mume huyo alizidi kueleza kuwa baada ya mkewe kukiri kwamba Manfree amekuwa akimtaka wakutane chemba ndipo kwa pamoja walikubaliana kuandaa fumanizi.

“Nilimwambia mke wangu lazima tutege fumanizi, lengo ni kumfanya jamaa aachane na tabia hizi ambazo zinaweza kuharibu ndoa, watoto wakateseka na mambo menginemengine. Nilimruhusu amkubalie kukutana gesti,” alisema mume.

Mume anasema siku ya tukio, Manfree bila kujijua alimtumia meseji mwanamke huyo, akamuomba wakutane ndani ya gesti moja iliyopo Kimara Mwisho ambapo bila kupoteza muda mwanamke huyo alimtonya mumewe juu ya meseji hiyo.

“Baada ya kunionesha meseji hiyo nilitafuta baadhi ya marafiki zangu ili twende pamoja kwenye eneo la tukio wakawe mashahidi.”

Baada ya mke kufika ndani ya gesti hiyo, mume anadai alimtaarifu jamaa huyo ambaye alitokea na kumwambia mwanamke huyo kuwa amuongezee shilingi elfu kumi kwani chumba ni elfu ishirini.

Kwa mujibu wa mume huyo, baada ya wawili hao kuingia chumbani humo, jamaa huyo alivua nguo zote na kukimbilia bafuni. Nyuma, mwanamke huyo aliutumia mwanya huo kumtaarifu mumewe ambaye naye aliwashika masikio marafiki ili wakae mkao wa kumnasa jamaa huyo.

Muda mfupi baadaye, mume anasema Manfree alitoka bafuni na kufikia kitandani puu! Hana hili wala lile, mwanamme huyo akiwa na ‘skwadi’ yake walizama ndani, wakagonga mlango, Manfree akakaribisha, alijua ni mhudumu amemletea bia maana aliagiza.

Mume alizidi kusema kuwa jamaa alipigwa butwaa na kuonekana kuweweseka. Yeye akamuuliza imekuaje yuko na mke wake chumbani? Jamaa akawa hana la kujibu.

Katika maelezo yaliyomo kwenye video ya tukio zima Manfree anajieleza akimuomba msamaha mume huyo pamoja na wote waliokuwa chumbani humo.

Mwanaume huyo anadai kuwa kwa hasira aliamua kumpigia simu mke wa Manfree ili afike kwenye gesti hiyo kushuhudia mumewe alivyokutwa na mke wa mtu gesti.

Anasema: “Mke alifika, akamkuta mumewe hajavaa nguo, aliumia sana lakini hakuwa na la kufanya.”

Baada ya ‘mhangaikaji’ wetu kuzipata data hizo, juzi asubuhi alimtafuta Manfree kwa njia ya simu ya mkononi kupitia namba alizopewa na watu wa karibu. Mwanzoni jamaa huyo alionekana kugoma lakini baada ya kubanwa kwa vielelezo alikubali huku akisema japo alinaswa lakini pia jamaa hao walitumia njia za kumteka.

“Aa..! Ni kweli nilikutwa na zahama hiyo lakini jamaa waliniteka bwana. Hata hivyo, sitarudia tena kuwa na uhusiano na wake za watu na tulishamalizana na mwenye mke kwa kumuomba msamaha,” alisema Manfree.

Katika hali ya kushangaza, baada ya mkewe kupigiwa simu na mwandishi na kukiri kuwa ni kweli mumewe alinaswa chumba cha gesti akiwa na mke wa mtu, alisema bado anampenda na kwamba ndoa yao bado iko imara kama mizizi ya mti wa mbuyu!

“Ni kweli mume wangu alifumaniwa lakini bado nampenda sana na siwezi kumwacha, nitamvumilia maana ni mume wangu,” alisema mke wa Manfree aliyejitambulisha kwa jina moja la Sarah.

MAMA WA SHARO MILIONEA AMKANA MJUKUU WAKE


Stori: Hamida haasan na Gladness Mallya
MAMA wa aliyekuwa msanii maarufu Bongo, marehemu Hussein Mkiety ‘Sharo Millionea’, Zainab Mkiety amemkataa mtoto ambaye alipelekewa Tanga na mama yake anayetokea Geita akidai ni damu ya Sharo.

Mtu wa karibu na familia hiyo ameliambia gazeti hili kuwa baada ya msiba kupoa, mama wa mtoto huyo alifunga virago na mwanaye kwa ajili ya kwenda kutembelea kaburi la Sharo na kwenda kujitambulisha kwa bibi wa mtoto.
Chanzo hicho kilieleza kuwa mama mtoto huyo alipofika Muheza jijini Tanga, alipokelewa na watu wa bodaboda ambao walimsindikiza hadi nyumbani kwa mama Sharo.
“Alipofika alipokelewa lakini cha kushangaza mama Sharo alimkataa na kusema marehemu hakuwa na mtoto kwa sababu hakuwahi kumwambia,” alisema sosi huyo.

Ili kupata ukweli wa habari hiyo, paparazi wetu aliwasiliana na mama Sharo kwa simu ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli alikuja mwanamke akiwa amebeba mtoto ambaye alijitambulisha kwangu kuwa ametokea Geita.
“Alisema mtoto aliyekuwa amembeba ni wa Sharo lakini nilikataa nikamwambia kuwa mwanangu hakuwahi kuniambia kuwa ana mtoto na nilipowauliza marafiki zake walisema hawana taarifa hizo.
Nisingeweza kumpokea kwa sababu alishajitokeza mwingine na kudai kuwa ana mimba ya mwanangu, baada ya kumkataa mwanamke huyo aliondoka na mpaka leo sina mawasiliano naye.”
Sharo alifariki dunia kwa ajali ya gari Novemba 26, mwaka jana katika Kijiji cha Maguzoni-Soga, Wilaya ya Muheza jijini Tanga.

MASOGANGE KUFUNGA NDOA SIKU YA KUFIKA TZ


MCHUMBA wa ‘video queen’ maarufu Bongo, Agnes Jerald ‘Masogange ‘, Evance Komu amefungua kinywa chake na kusema; siku mchumba wake huyo atakapotia miguu nchini, wanafunga ndoa.
Masogange kwa sasa (juzi) yupo nchini Afrika Kusini alikokuwa akikabiliwa na kesi ya madawa ya kulevya ambapo alifanikiwa kuwa huru baada ya kulipia faini ya randi 30,000 (shilingi 4,800,000) aliyoamriwa na Mahakama ya Kempton.
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni mara baada ya Masogange kuachiwa, Evance alisema anamshukuru Mungu kwa kesi hiyo kumalizika na kinachofuata kwenye uchumba wao ni ndoa tu.
Evance aliweka bayana kuwa kinachomsukuma afanye uamuzi huo kwa sasa ni kutokana na jinsi alivyoguswa na changamoto kubwa alizopitia mchumba wake hivyo ameona kuna kila sababu ya kumuoa kabisa ili apate faraja ya milele.
“Mchumba wangu amepitia majaribu ya kutosha na mimi sioni muda wa kupoteza tena, akitua tu Bongo kinachofuata ni ndoa nina imani itakuwa ndiyo jambo kubwa la kumfariji na kumpa upendo wa hali ya juu,” alisema Evance pasipo kutaja siku ambayo mchumba wake atarejea.
Katika kesi hiyo iliyokuwa ikimkabili Masogange, alishikiliwa na mwenzake Melisa Edward ambaye naye aliachiwa huru kwa kukosekana na hatia.

BAADA YA KENYA SASA AL-SHABAAB YAIGEUKIA TANZANIA....WATISHIA KUIVAMIA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA


*Yajigamba kufanya mashambulio muda wowote
*Watanzania wapewa mafunzo ya ugaidi nje ya nchi
*Polisi nchini wasema vyombo vya ulinzi viko macho
*Mtanzania akamatwa Kenya akihofiwa gaidi

WAKATI wananchi wa Afrika Mashariki wakijawa na hofu ya mashambulio yanayopangwa kufanywa na vikundi vya ugaidi vya Al Qaeda na Al Shabab, imebainika kuna Watanzania waliopewa mafunzo ya ugaidi wanaojiandaa kufanya maovu.

Hayo yamebainika siku chache baada ya wanamgambo wa kundi la Al Shabab kufanya mashambulio katika Jengo la Biashara la Westgate mjini Nairobi na kuua watu zaidi ya 70 na kuacha mamia wengine wakiwa wamejeruhiwa.

Mkuu wa Interpol Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile aliyasema hayo jana katika mahojiano maalumu na MTANZANIA.

Alikuwa akizungumzia kauli ya hivi karibuni iliyotolewa na Msemaji wa Al Shabab, Sheikh Abdulaziz Abu Muscab aliyetoa tahadhari kwamba kundi lake linapanga mashambulio mengine Tanzania na Uganda.

Babile alisema taarifa zinaonyesha vijana wa Tanzania waliojiunga na mafunzo ya ugaidi yanayotolewa na vikundi vya Al Qaeda na Al Shabab, wamefanya hivyo baada ya kushawishiwa watapata utajiri wa haraka.

Alisema hali hiyo imevifanya vyombo vya ulinzi na usalama nchini kutoipuuza kauli hiyo ya Sheikh Abdulaziz Abu Muscab.

“Tunajua wapo Watanzania wanapewa dozi za ugaidi, na sisi siyo kisiwa, watu ni hao hao… tumejipanga kuyakabili haya na kuushirikisha umma katika ulinzi,” alisema.

Babile alisema kauli ya msemaji wa kundi la Al Shabab ya kuivamia Tanzania siyo ya kupuuza na kusisitiza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini viko tayari kukabiliana na lolote litakalotokea.

“Tumeisikia kauli yake kwenye mitandao ya jamii, imetufanya kuwa alert (macho) vya kutosha, imetuweka sawa na imetukumbusha kuwa tunaweza kuvamiwa wakati wowote.

“Hatuja-relax hata kidogo, tumejiweka sawa kwenye human resources zetu, materials resource na hata frontline officers wetu wako makini mno.

“Mfano kwenye viwanja vya ndege ambako ni muhimu, kuna mitambo inayoweza kugundua hati za kusafiria za washukiwa wa uhalifu wanaotafutwa kimataifa na tutawakamata tu.

“Lakini hata kwenye mipaka yetu yote hatuko peke yetu, tumepanua wigo wa kupata taarifa za kiintelijensia na katika kufanya kazi hii tunashirikiana na vyombo vyote vya ulinzi na usalama,” alisema.

Baada ya kufanya mashambulio mjini Nairobi Jumamosi iliyopita, Msemaji wa Al Shabab, Sheikh Abdulaziz Abu Muscab, aliripotiwa kwenye mitandao ya jamii akisema shambulio hilo lilikuwa ni la kulipiza kisasi baada ya majeshi ya Kenya kuvamia kundi hilo lenye makazi yake mjini Kismayu, Somalia.

Mitandao ya jamii pia ilimnukuu Sheikh Abu Muscab akijigamba kuwa wakati wowote mashambulio ya kikundi hicho yataelekezwa Uganda na Tanzania.

Wakati huohuo, Babile amesema Mtanzania mmoja alikamatwa Kenya akishukiwa kuwa ni mmoja magaidi waliovamia jengo la Westgate. 

Bila kumtaja jina, alisema mtu huyo ni mkazi wa Arusha na alikamatwa muda mfupi baada ya kuingia Kenya akitoa Tanzania, akitumia usafiri wa mabasi ya abiria.

“Walipomkamata wakatuletea taarifa sisi, tukatafuta kwenye database zetu na information za ndani zikatuonyesha hakuwa mtu hatari, tukamuachia.

“Kilichowatia hofu na kumshuku mtu huyu ni muda alioingia Kenya na muda wa tukio lilipotokea… lakini tumeangalia taarifa zote tukagundua hakuwa na shaka,” alisema Babile.

Thursday 19 September 2013

SITTA AWATETEA WAHAMIAJI HARAMU




Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samuel Sitta, akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa
habari (hawapo pichani) Dar es Salaam jana kuhusu kutengwa kwa Tanzania katika nchi za Afrika
Mashariki pamoja na ‘Operesheni Kimbunga’ inayoendelea hapa nchini. Kulia ni Katibu mkuu wa
wizara hiyo Joyce Mapunjo.


WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amekosoa utaratibu unaotumika kuwaondoa wahamiaji haramu nchini kupitia Operesheni Kimbunga, akisema ni kinyume cha haki za binadamu.Waziri Sitta amekuwa kiongozi wa kwanza nchini kukosoa utaratibu unaotumika kuondoa wahamiaji hao tangu Rais Jakaya Kikwete, aagize wawe wameondoka nchini ndani ya siku 14, vinginevyo wataondolewa kwa nguvu. Rais Kikwete alitoa agizo hilo akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Kagera.


Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Sitta aliwataka wakuu wa mikoa, wilaya, jeshi la polisi na uhamiaji kuwapa muda wa kutosha wahamiaji hao ili waweze kujiandaa kuondoka na mali zao ambazo walichuma kwa muda mrefu walioishi nchini kuliko kuwaswagaswaga.

"Haifai kwa hawa ndugu zetu ambao tumeishi nao kwa muda mrefu leo hii wanaswagwaswagwa jambo ambalo ni kinyume cha haki za binadamu pamoja na utawala bora," alisema na kuongeza;"Je, Watanzania waliopo nje ya nchi wakiondolewa kwa nguvu kama hawa wenzetu wanavyofanyiwa tutafurahi?" Alisema kwa jambo hili Tanzania isionekane ina nongwa na nchi fulani kwani hata Rais Kikwete, wakati anatoa agizo hilo hakusema utaratibu huo utumike.


Alitoa mfano kuwa kuna mwanamke ambaye amefukuzwa nchini ambaye ni raia wa Rwanda akisema aliishi kwa zaidi ya miaka 30 nchini Tanzania na mtoto wake amesomea nchini na kuajiriwa katika Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)."Mtu kama huyu hakutendewa haki...mtu unamfukuza anaondoka na begi lake moja wakati ana mali zake nyingi...huyo ni lazima arudishwe ili ahakiki mali zake," alisema.


Alisema walioondolewa na kuacha mali zao nyingi pamoja na watoto watarudishwa nchini kufanyiwa uhakiki kama inavyofanyika kwa raia wa Malawi. Alishauri wahamiaji hao watakaorudi kufuata mali zao wapewe makazi ya muda na mali zao zisiporwe kwani watu hao hawakuwa majambazi.

"Kama umemuacha mtu ameishi nchini kwako kwa muda wa miaka 30 halafu leo unamfukuza kwa kumswagaswaga nani mwenye kosa? Na muda wote ulikuwa wapi?" Alihoji Sitta na kusisitiza kuwa; "Ndiyo maana tunasema aondolewe kwa utaratibu."Aliongeza kuwa miongoni mwa wahamiaji haramu waliofukuzwa baadhi yao waliwahi kuwa viongozi wa Serikali za vijiji na mitaa katika maeneo waliyokutwa wakiishi.


Waziri Sitta alisema tayari amepokea barua kutoka nchi za Burundi na Rwanda zikilalamikia utaratibu unaotumika kuwaondoa wahamiaji haramu hao."Oktoba 1 mimi na Waziri wa Mambo ya Ndani tutakuwa mpakani mwa Burundi na Rwanda ili kuangalia jinsi operesheni hiyo inavyotekelezwa na kufanya mazungumzo na viongozi wa nchi hizo ili Tanzania isionekane ina malengo mabaya," alisema Sitta.


Alisema endapo utaratibu unaotumika wa kuwaondoa ukiendelea maadui wa Tanzania wataona njia hiyo inalenga kuwakomoa, jambo ambalo si la kweli.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imefuatilia taarifa kwenye vyombo vya habari mbalimbali hapa nchini, kuhusu kushiriki kwa Mheshimiwa Lu Younqing Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa nchini kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika huko Shinyanga, mwishoni mwa juma lililopita.

Taarifa hizo zimeambatana na picha zinazomuonyesha Mheshimiwa Lu akiwa amevaa kofia yenye nembo ya CCM. Habari zinaeleza kuwa Balozi alikwenda Shinyanga kuhudhuria uzinduzi wa mradi wa viwanda vya kuchambulia pamba vinavyojengwa na mwekezaji wa Kichina anayeitwa Tahong, na viwanda hivyo vita kuwa na uwezo wa kuchambua tani 120,000 za pamba kwa mwaka, vitakapokamilika mwakani.

Wizara inatambua mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Jamhuri ya watu wa China na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na vilevile inatambua kazi nzuri ambayo Balozi Lu Younqing amekuwa akifanya toka alipowasili nchini Tanzania. Kutokana na tukio hili, Wizara inapenda kuelekeza kwamba kitendo cha Balozi yeyote kuhudhuria mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa na kuvaa sare zenye nembo ya vyama vya siasa sio sahihi na kinakiuka Kifungu cha 41(1) cha Mkataba wa Vienna wa mwaka 1961, unaoongoza uhusiano wa kidiplomasia. Mkataba huo wa Vienna unazuia wawakilishi wa nchi za nje kujihusisha na masuala ya ndani ya nchi ikiwemo siasa wanapofanya kazi zao kwenye nchi za uwakilishi. Aidha, Sheria ya Diplomasia ya Tanzania ya Mwaka 1986 ambayo ni zao la Mkataba wa Vienna pia hairuhusu Balozi au mfanyakazi wa Ubalozi kujihusisha na masuala ya ndani ya nchi.

Itakumbukwa kwamba, katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2012 Wizara ilikumbana na vitendo vinavyofanana na kitendo hiki na ikachukua hatua stahiki. Na kwa tukio hili pia Wizara imechukua hatua za kidiplomasia zinazostahili ili kuzuia jambo hili lisitokee tena.

IMETOLEWA NA:
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
18 Septemba, 2013
Dar Es Salaam.

Chama legelege huzaa Serikali legelege. Mwl. J.K Nyerere

MTUHUMIWA AJINYEA MAHAKAMANI WAKATI AKISOMEWA KIFUNGO CHA MIEZI 6 JELA JIJINI DAR..!!



 
Mtu mmoja amehukumiwa kifungu cha miezi sita jela katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Sokoine Drive kwa kosa la kujisaidia haja kubwa ndani ya Mahakama wakati akisomewa mashitaka. 

Adhabu hiyo ilitolewa papo hapo baada ya mshitakiwa Hassan Omary (25) kufanya kitendo hicho aliposomewa mashitaka mengine tofauti.
  
Hakimu William Mutaki ndiye aliyetoa hukumu hiyo. Wakati akisomewa mashitaka sanjari na washitakiwa wengine watatu ya kubughudhi abiria maeneo ya Kariakoo, Omary inadaiwa alitokwa haja kubwa.
  
Mwandishi alishuhudia mshitakiwa huyo akisafisha eneo la mahakamani alikochafua kabla ya kupelekwa jela. Wengine anaoshitakiwa nao katika kesi hiyo ni Mohamedi Mussa (20),Hassani Ramadhani (18),Shukuru Adison (26) na Ally Omary (28).

Mwendesha mashitaka wa serikali John kijumbe alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi William Mutaki kuwa washitakiwa walitenda kosa la kuwanyanyasa na kuwabugudhi abiria ,Septemba 18 ,mwaka huu Kariakoo, jijini Dar es Salaam. Washitakiwa wengine walirudishwa rumande hadi Oktoba 2,mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
  
Katika kesi nyingine, mshitakiwa Jacob Sasita (28) amehukumiwa kifungo cha mwezi mmoja baada ya kukiri kuwanyanyasa abiria .
  
Sasita alikuwa miongoni mwa washitakiwa saba waliofikishwa mahakamani kwa kosa hilo. Washitakiwa wengine ni Ramadhani Juma (38),Abeid Ismail (25),Abuu Rajabu(25),Salimu Kijimbo (39),Ally Hassani (28),Josephb Chambo (29)na Fabiani Thomas (28) ambao walikana kutenda kosa baada ya kusomewa mashitaka.
  
Mbele ya Hakimu Mkazi Timoth Lyon, Mwendesha Mashitaka wa Serikari, Richard Magudi alidai watu hao walitenda kosa la kuwanyanyasa abiria katika kituo kikuu cha mabasai cha Ubungo ,kabla ya kukamatwa na askari polisi. Walirudishwa rumande hadi Oktoba 2 mwaka huu kesi itakapotajwa tena.