 
 
MKANDA mzima wa askari bandia wa Kikosi cha Usalama Barabarani 
(trafiki), James Juma Hussein (45)  aliyekamatwa saa 1:30 asubuhi ya 
Agosti, 14, 2013 maeneo ya Tabata Kinyerezi Mnara wa Voda, jijini Dar es
 Salaam akiwa ndani ya sare zake za kazi, umepatikana....
Kwa nini James alikamatwa? Asubuhi hiyo, afisa mmoja wa trafiki mwenye 
cheo cha ukaguzi alikuwa akipita eneo hilo kwenda kazini, alipomwona 
James alisimamisha gari, akashuka kwenda kumsalimia.  
Lakini alishangaa kuviona vifungo vya shati lake ni vya kawaida (vya 
polisi vinatakiwa kuandikwa police force yaani ‘jeshi la polisi’), 
akamtilia shaka.  
Afisa huyo Alimkamata ‘askari feki’ huyo  mkazi wa Kimara Matangini, Dar
 na kumfikisha kwenye Kituo cha Polisi Stakishari, wilayani Ilala, Dar 
akafunguliwa jalada namba STK/RB/15305/2013 KUJIFANYA ASKARI ili 
taratibu za kisheria zichukuliwe juu yake. 
Trafiki huyo alisema kuwa yeye ni mnyamwezi wa Tabora na ana wiki moja tangu ajifanye yeye ni trafiki. 
Nguo nyeupe juu ya kofia niliitengeneza kienyeji, krauni, tepe za
 usajenti na mkanda ni za shemeji yangu alikuwa polisi Tabora, ni 
marehemu, alikuwa akiitwa Shaban. 
James aliwaambia polisi kuwa suruali nyeupe ya kitrafiki aliishona 
mtaani lakini kamba ya filimbi na kizibao cha kung’ara vilikuwa vya 
polisi. 
Askari: Uliwahi kuwa polisi?
James: Niliwahi kupata mafunzo ya upolisi katika Chuo cha Polisi Moshi 
(CCP) mwaka 1990-91 lakini nilifukuzwa kazi kwa sababu nilikwenda 
muziki vitu ambavyo havitakiwi kufanywa na polisi. Nilirudi Tabora nikawa mkulima na mke wangu na mtoto mmoja ambao
 wote sasa ni marehemu. 
Ndani ya nguo za kitrafiki alizokuwa amevaa James, alikutwa na suruali ya bluu na fulana ya kijani.
James alisema njaa ndiyo iliyomfanya ajifanye trafiki na ‘kuwapiga 
mikono’ madereva, hasa wa daladala ili anapowakuta na makosa kwenye 
magari yao ajipatie chochote. 
Kamishina wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Suleiman Kova amethibitisha kukamatwa kwa polisi huyo feki
 
 
No comments:
Post a Comment