Pages

Translate

Wednesday 24 July 2013

SUMAYE AWAONYA WAUZA UNGA

 
Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye amewatahadharisha Watanzania kuwa makini na watu wanaotaka madaraka kwa kugawa fedha katika sehemu mbalimbali za nchi au majimbo akionya wanaweza kujikuta wakimweka madarakani kiongozi anayejihusisha na biashara ya dawa za kulevya.
“Hivi kama mtu anaweza kuhonga sehemu kubwa ya wapigakura katika jimbo la uchaguzi au hata katika nchi kama nafasi anayosaka ni urais; tumeshajiuliza hizo fedha nyingi hivyo anapata wapi? Kama anajihusisha na biashara hizo chafu akipata nafasi hiyo watoto wetu watapona?” alisema Sumaye jana na kuongeza:
“Haya ni maswali muhimu ya kujiuliza tunapoelekea mwaka kesho kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na mwaka 2015 wakati wa Uchaguzi Mkuu.”
Alisema hayo mjini Morogoro kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (Mviwata).
Akizungumza kwa tahadhari alisema haizungumzii Serikali yake iliyoko madarakani wala mtu yeyote, bali tabia mbaya, Sumaye alisema biashara ya dawa za kulevya inahusisha fedha nyingi na mitandao mipana ambayo isipodhibitiwa inaweza kulitumbukiza taifa katika janga.
Alisema Katiba Mpya siyo mwarobaini wa matatizo yanayolikabili taifa bali, utekelezaji na usimamizi wa sheria na kwamba jambo muhimu ni kuwa na Serikali itakayosimamia na kutekeleza sheria ili kulinda yale yaliyoelekezwa katika Katiba.
“Katiba haiwezi kumzuia mwizi kwenda kuiba na sheria haitamzuia mwizi kwenda kuiba ila itatamka adhabu ya kupewa huyo mwizi. Kwa hiyo ili vyote hivi viwe na maana ni lazima awepo mtu au chombo cha kumkamata huyo mwizi na kumfikisha katika mikono ya sheria na chombo hicho ni Serikali. Kama haiwezi kufanya hiyo kazi kwa ukamilifu tutaishia kulalamika tu na maonevu na maumivu yataendelea kuumiza jamii.”
“Kwa hiyo hata Katiba iwe nzuri namna gani na ikatamka kuwa rushwa ni adui wa haki na hata ikatoa adhabu kali sana kwa kosa hilo; kama tutaweka viongozi madarakani kwa rushwa, hiyo Katiba wala haitatusaidia. Hivyo Katiba nzuri mpya lazima iambatane na Serikali safi yenye kusimamia masilahi ya umma. Huwezi kumweka madarakani mwenyekiti wa kijiji au diwani au mbunge au hata Rais kwa rushwa ya kuwanunua wapigakura halafu utegemee Katiba Mpya itajibu matatizo ya jamii.”
Azungumzia Mviwata
Sumaye alisema Mtandao huo wa Wakulima Wadogo Tanzania ndiyo unaojua tatizo la kilimo na shida zao na ndiyo unaotakiwa kuulizwa cha kufanya ili kilimo chetu kibadilike na mkulima afaidike...
“Kama hatuwahusishi na kuwashirikisha katika sera, mipango na programu za kilimo, basi tujue kuwa sera, mipango na programu hizo zitashindwa.”
Alisema Tanzania ni nchi ambayo wananchi wake wengi wanategemea kilimo kwa maisha yao na uchumi wa taifa pia kwa kiasi kikubwa hutegemea sekta hiyo, lakini bado ni duni na hakijamkomboa mkulima mwenyewe wala uchumi wa taifa... “Nchi na watu wake bado ni maskini pamoja na kuwa watu wachapakazi wapo na ardhi kubwa na nzuri yenye rutuba ipo

Mtoto wa Mkulima PINDA Hovyooo!!! Rais Kikwete Amuumbua




Naam, Tanzania yetu imewahi kuwa na viongozi mbalimbali wabovu, lakini linapokuja suala la mawaziri wakuu, basi Mizengo Kayanda Pinda, anaweza kabisa kuingia kwenye kumbukumbu kama WAZIRI MKUU MBOVU KULIKO WOTE KATIKA HISTORIA YA NCHI YETU.
Ndio, Kuna Edward Lowassa, aliyeng'oka kwa kashfa ya Richmond, lakini angalau yeye hakuwa m-babaishaji katika kauli zake. N apengine kilichmosaidia Lowassa ni kutambua busara kuwa mdomo sharti ushirikiane na ubongo kabla ya kutoa kauli yoyote ile.
Pinda, anayeitwa Mtoto wa Mkulima, amekuwa maarufu zaidi kwa kauli zake za kipuuzi kuliko utendaji kazi.Mbabaishaji huyo aliwahi kuzua sokomoko huko nyuma alipohalalisha MAUAJI: kwa uzembe tu wa kufikiri, Pinda alidai kuwa anaguswa sana na mauaji ya maalbino,kwahiyo ni ruksa kwa wananchi kuwauwa WATUHUMIWA wa mauaji hayo. Japo kitaaluma  mwanasheria, lakini Pinda hakuona tatizo katika kauli yake hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inahamisha nguvu za polisi na mahakama na kuzikabidhi kwa umma.Kwa lugha nyingine, mzembe huyo alikuwa anahalalisha mob justice.
Badala ya ku-behave kama mtu mzima, Pinda akenda bungeni na kujitetea kwa KULIA KAMA MTOTO.Lakini kwa bahati nzuri, wengi wa wabunge wetu wapo bize zaidi na posho zao kuliko kuwatendea haki wananchi wanaowawakilisha, na machozi hayo ya kinafiki ya Pinda yakamnusuru.
Katika kuonyesha kuwa Tanzania kwa sasa ni kama haina Waziri Mkuu kwani Pinda anayeshikilia nafasi hiyo ni so useless kiasi kwamba uwepo au kutokuwepo kwake hakuna tofauti, majuzi akakurupuka tena na kauli nyingine ya kibabaishaji.Akatangaza kuwa ni ruksa kwa polisi kupiga raia ZAIDI...Yaani kana kwamba unyanyasaji unaofanywa na polisi hautoshi, na sasa wanahamasishwa kutoa vipigo zaidi.
Watu tumesema weee kuhusu kauli hiyo ya kihuni lakini kwa vile aliyemteua Pinda kushika nafasi hiyo hana tofauti sana na Pinda, Waziri Mkuu huyo bado yupo madarakani hadi dakika hii.
Na uwepo wake huo umepelekea ujinga mwingine. Majuzi kumezuka sokomoko la kodi mpya ya SIM kadi.Badala ya kusikia kilio cha mamilioni ya Watanzania wanaopinga kodi hiyo, mropokaji Pinda akadai eti "wanaopinga kodi hiyo hawaitakii mema nchi yetu..." COMPLETELY USELESS!
Bahati nzuri, safari hii Rais Kikwete kaamua kutumia busara, na kwa namna flani, amemudu KUMUUMBUA PINDA. Rais amezitaka mamlaka husika kukaa pamoja kutafuta ufumbuzi wa haraka kuhusu kodi hiyo inayolalamikiwa na wananchi wengi. Rais aliyasema hayo alipokutana na viongozi wa Wizara ya Fedha, na wale wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia, na Mamlaka ya Mawasiliano TCRA.
- See more at: http://www.chahali.com/2013/07/mtoto-wa-mkulima-pinda-hovyooo-rais.html#sthash.XSd2iJnG.dpuf

Mtoto wa Mkulima PINDA Hovyooo!!! Rais Kikwete Amuumbua




Naam, Tanzania yetu imewahi kuwa na viongozi mbalimbali wabovu, lakini linapokuja suala la mawaziri wakuu, basi Mizengo Kayanda Pinda, anaweza kabisa kuingia kwenye kumbukumbu kama WAZIRI MKUU MBOVU KULIKO WOTE KATIKA HISTORIA YA NCHI YETU.
Ndio, Kuna Edward Lowassa, aliyeng'oka kwa kashfa ya Richmond, lakini angalau yeye hakuwa m-babaishaji katika kauli zake. N apengine kilichmosaidia Lowassa ni kutambua busara kuwa mdomo sharti ushirikiane na ubongo kabla ya kutoa kauli yoyote ile.
Pinda, anayeitwa Mtoto wa Mkulima, amekuwa maarufu zaidi kwa kauli zake za kipuuzi kuliko utendaji kazi.Mbabaishaji huyo aliwahi kuzua sokomoko huko nyuma alipohalalisha MAUAJI: kwa uzembe tu wa kufikiri, Pinda alidai kuwa anaguswa sana na mauaji ya maalbino,kwahiyo ni ruksa kwa wananchi kuwauwa WATUHUMIWA wa mauaji hayo. Japo kitaaluma  mwanasheria, lakini Pinda hakuona tatizo katika kauli yake hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inahamisha nguvu za polisi na mahakama na kuzikabidhi kwa umma.Kwa lugha nyingine, mzembe huyo alikuwa anahalalisha mob justice.
Badala ya ku-behave kama mtu mzima, Pinda akenda bungeni na kujitetea kwa KULIA KAMA MTOTO.Lakini kwa bahati nzuri, wengi wa wabunge wetu wapo bize zaidi na posho zao kuliko kuwatendea haki wananchi wanaowawakilisha, na machozi hayo ya kinafiki ya Pinda yakamnusuru.
Katika kuonyesha kuwa Tanzania kwa sasa ni kama haina Waziri Mkuu kwani Pinda anayeshikilia nafasi hiyo ni so useless kiasi kwamba uwepo au kutokuwepo kwake hakuna tofauti, majuzi akakurupuka tena na kauli nyingine ya kibabaishaji.Akatangaza kuwa ni ruksa kwa polisi kupiga raia ZAIDI...Yaani kana kwamba unyanyasaji unaofanywa na polisi hautoshi, na sasa wanahamasishwa kutoa vipigo zaidi.
Watu tumesema weee kuhusu kauli hiyo ya kihuni lakini kwa vile aliyemteua Pinda kushika nafasi hiyo hana tofauti sana na Pinda, Waziri Mkuu huyo bado yupo madarakani hadi dakika hii.
Na uwepo wake huo umepelekea ujinga mwingine. Majuzi kumezuka sokomoko la kodi mpya ya SIM kadi.Badala ya kusikia kilio cha mamilioni ya Watanzania wanaopinga kodi hiyo, mropokaji Pinda akadai eti "wanaopinga kodi hiyo hawaitakii mema nchi yetu..." COMPLETELY USELESS!
Bahati nzuri, safari hii Rais Kikwete kaamua kutumia busara, na kwa namna flani, amemudu KUMUUMBUA PINDA. Rais amezitaka mamlaka husika kukaa pamoja kutafuta ufumbuzi wa haraka kuhusu kodi hiyo inayolalamikiwa na wananchi wengi. Rais aliyasema hayo alipokutana na viongozi wa Wizara ya Fedha, na wale wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia, na Mamlaka ya Mawasiliano TCRA.
- See more at: http://www.chahali.com/2013/07/mtoto-wa-mkulima-pinda-hovyooo-rais.html#sthash.XSd2iJnG.dpuf

No comments:

Post a Comment