CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewaonya makada 
wawili wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward 
Lowassa, na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, 
kuwa wasipoteze muda kuusaka urais 2015 kwa njia ya harambee makanisani 
na misikitini. Onyo
 hilo limetolewa na wabunge wa CHADEMA Kanda ya Ziwa wakati wakihutubia 
mkutano wa hadhara uliofanyika kituo cha mabasi Igoma jijini Mwanza, 
wakisema kuwa pamoja na makada hao kutumia nyumba za ibada kujijenga 
kisiasa wasipoteze muda wao kuwania nafasi hiyo kwani hawawezi kuipata.
 
      Akizungumza kwa niaba ya wabunge wenzake, mbunge wa Nyamagana, 
Ezekiel Wenje, alisema kuwa Lowassa ambaye alijiuzulu wadhifa wa uwaziri
 mkuu mwaka 2008 kwa kashfa ya kampuni tata ya kufua umeme ya Richmond 
kwa sasa anaonekana kuhaha kuchangisha fedha makanisani, misikitini na 
Wamachinga akitaka aungwe mkono katika harakati zake za kisiasa. Wenje
 aliwasihi wananchi kuchukuwa fedha zinazotolewa na Lowassa, lakini 
akawataka wafanye uamuzi wa kuiangamiza CCM katika uchaguzi wa serikali 
za mitaa mwaka 2014 uchaguzi mkuu wa 2015. “Lowassa
 ambaye ni mbunge wa Mondoli na mjumbe wa NEC, amekuwa kinara wa 
kuhudhuria harambee akilenga kujiimarisha kisiasa. Nasikia majuzi 
alikuja hapa Mwanza kuchangisha fedha kwa Machinga. Na huyu Sitta eti na
 yeye anausaka urais...jamani Tanzania imekuwa nchi ya kuchezewa hivi?”
 
    “Sasa fedha wanazotoa zipokeeni lakini maamuzi yenu ya kuiondoa CCM 
madarakani na kuipa madaraka hayo CHADEMA mwaka 2015 yapo pale pale,” 
alisema Wenje kisha kushangiliwa na wananchi waliofurika mkutanoni 
hapo. Aliongeza
 kuwa ili kuthibitisha kwamba serikali haiwajali wananchi wake, imetoa 
misamaha kwenye mafuta yanayotumika katika migodi ya madini nchini, 
lakini wananchi walalahoi wanatozwa kodi ya sh 1,000 kwenye laini ya 
simu, wanja na vipodozi vingine vya wanawake. Wenje
 alisema kuwa suluhisho pekee la Watanzania kujinasua na janga la 
umaskini ni kuiondoa madarakani serikali ya CCM pamoja na kuwa na Katiba
 nzuri inayojali ustawi wao.
 
      Alisema kuwa CHADEMA kimedhamiria kukusanya saini za Watanzania 
milioni 10 kwa lengo la kutaka Katiba mpya iamuru Spika wa Bunge, 
mawaziri wasitokane na wabunge ili kujenga uwajibikaji. Mambo
 mengine muhimu ndani ya Katiba mpya yatakayowekewa saini na wananchi ni
 pamoja na kuundiwa mabaraza ya Katiba ambayo yatawashirikisha, kuwepo 
mawaziri saba katika baraza la mawaziri, dira ya maendeleo ya taifa, 
haki za binadamu, Bunge kuwa na wabunge 75 na mihula mitatu ya ukomo wa 
ubunge. Naye
 mbunge wa Bukombe, Profesa Kulikoyela Kahigi, aliwataka wananchi 
kutambua jinsi serikali ya CCM ilivyoshindwa kuwapelekea maendeleo 
kinyume cha Katiba ya nchi.
 
 
No comments:
Post a Comment