Pages

Translate

Wednesday 24 July 2013

CHADEMA YAWAONYA LOWASA NA SITTA 2015



      CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewaonya makada wawili wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kuwa wasipoteze muda kuusaka urais 2015 kwa njia ya harambee makanisani na misikitini. Onyo hilo limetolewa na wabunge wa CHADEMA Kanda ya Ziwa wakati wakihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kituo cha mabasi Igoma jijini Mwanza, wakisema kuwa pamoja na makada hao kutumia nyumba za ibada kujijenga kisiasa wasipoteze muda wao kuwania nafasi hiyo kwani hawawezi kuipata.

       Akizungumza kwa niaba ya wabunge wenzake, mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje, alisema kuwa Lowassa ambaye alijiuzulu wadhifa wa uwaziri mkuu mwaka 2008 kwa kashfa ya kampuni tata ya kufua umeme ya Richmond kwa sasa anaonekana kuhaha kuchangisha fedha makanisani, misikitini na Wamachinga akitaka aungwe mkono katika harakati zake za kisiasa. Wenje aliwasihi wananchi kuchukuwa fedha zinazotolewa na Lowassa, lakini akawataka wafanye uamuzi wa kuiangamiza CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2014 uchaguzi mkuu wa 2015. “Lowassa ambaye ni mbunge wa Mondoli na mjumbe wa NEC, amekuwa kinara wa kuhudhuria harambee akilenga kujiimarisha kisiasa. Nasikia majuzi alikuja hapa Mwanza kuchangisha fedha kwa Machinga. Na huyu Sitta eti na yeye anausaka urais...jamani Tanzania imekuwa nchi ya kuchezewa hivi?”

     “Sasa fedha wanazotoa zipokeeni lakini maamuzi yenu ya kuiondoa CCM madarakani na kuipa madaraka hayo CHADEMA mwaka 2015 yapo pale pale,” alisema Wenje kisha kushangiliwa na wananchi waliofurika mkutanoni hapo. Aliongeza kuwa ili kuthibitisha kwamba serikali haiwajali wananchi wake, imetoa misamaha kwenye mafuta yanayotumika katika migodi ya madini nchini, lakini wananchi walalahoi wanatozwa kodi ya sh 1,000 kwenye laini ya simu, wanja na vipodozi vingine vya wanawake. Wenje alisema kuwa suluhisho pekee la Watanzania kujinasua na janga la umaskini ni kuiondoa madarakani serikali ya CCM pamoja na kuwa na Katiba nzuri inayojali ustawi wao.

       Alisema kuwa CHADEMA kimedhamiria kukusanya saini za Watanzania milioni 10 kwa lengo la kutaka Katiba mpya iamuru Spika wa Bunge, mawaziri wasitokane na wabunge ili kujenga uwajibikaji. Mambo mengine muhimu ndani ya Katiba mpya yatakayowekewa saini na wananchi ni pamoja na kuundiwa mabaraza ya Katiba ambayo yatawashirikisha, kuwepo mawaziri saba katika baraza la mawaziri, dira ya maendeleo ya taifa, haki za binadamu, Bunge kuwa na wabunge 75 na mihula mitatu ya ukomo wa ubunge. Naye mbunge wa Bukombe, Profesa Kulikoyela Kahigi, aliwataka wananchi kutambua jinsi serikali ya CCM ilivyoshindwa kuwapelekea maendeleo kinyume cha Katiba ya nchi.

     Alisema kuwa serikali imevunja ibara ya 8 ya Katiba inayowapa mamlaka wananchi, huku ikitakiwa kuboresha ustawi wa raia wake kwani kwa sasa mamlaka hayo yameporwa. “Lakini serikali hii ya CCM imeshindwa kuwasaidia kuyafahamu, maana mtaelimika muikatae. Sasa sisi CHADEMA tunataka lazima mamlaka ya wananchi yaheshimiwe maana ndio wenye nchi,” alisema. Wabunge wengine walio kwenye ziara hiyo ya kuimarisha chama Kanda ya Ziwa ni Dk. Anthony Mbassa (Biharamulo Magharibi), Conchesta Rwamlaza (Viti Maalumu Kagera) na viongozi wa kanda hiyo

No comments:

Post a Comment