Dar es 
Salaam. Ofisa mmoja wa Usalama wa Marekani (FBI), akiwa na mbwa jana 
aliingia Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kufanya
 ukaguzi.
Tukio hilo lilitokea muda mfupi kabla ya msafara wa 
magari ya Marekani kupita yakitokea Ikulu kwenda Uwanja wa Ndege wa 
Julius Nyerere kumlaki Rais Barack Obama.
Polisi ambaye hakutaka kutajwa alisema ofisa huyo  aliingia na mbwa hadi maeneo ya mapokezi, lakini muda mfupi walitoka.
“Walikwenda
 moja kwa moja mapokezi wakafanya ukaguzi,  kisha wakatoka nje ya jengo 
na kama hiyo haitoshi, ofisa huyo akiwa na mbwa alikwenda sehemu ya 
kuegesha magari yenye kesi na yale ya kawaida na kuanza kufanya ukaguzi,
 baada ya hapo waliondoka,” alisema polisi huyo na kuongeza:
“Licha
 ya mimi kutokuwa na  cheo pale, lakini hili la kutukagua na mbwa, ni 
kama wametudhalilisha... sisi ndiyo tunaaminika kwa usalama, leo hii 
wanatukagua na mbwa. Tena Kituo Kikuu.”
Hata hivyo, usalama 
kwenye vituo vingi ikiwamo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juliusu 
Nyerere, vilikuwa chini ya usimamizi na uangalizi wa makachero wa 
Marekani.
 

 
No comments:
Post a Comment