 
Kufuatia kuongezwa 
kwa kodi katika huduma za simu za mkononi , gharama za huduma hizo zinatajiwa 
pia kuongezeka kuanzia Julai Mosi mwaka huu.
Taarifa ya pamoja 
iliyotolewa jijini Dar es salaam na Umoja wa Makampuni ya Simu za Mkononi 
Tanzania – MOAT imesema pendekezo la serikali la kuweka kodi ya 14.5 kwenye 
huduma za simu za mkononi hazotoweza kukwepesha kupanda kwa gharama za simu kwa 
watumiaji.
MOAT inasema awali kodi 
ilikuwa ikitozwa asilimia 12.5 katika huduma ya mawasiliano ya simu na kwmaba 
ongezeko la kufiikia asilimia 14.5 tofauti na nchi za jirani Kenya na Uganda 
ambazo zimeendelea kutoza viwango vya ushuru vya asilimia 10 na 12.5 tu ni mzigo 
kwa watumiaji wa huduma za simu za mkononi.
Muswada 
wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2013 unaainisha, huduma za mawasiliano kuwa ni; 
“huduma yoyote ya maelezo inayotolewa na makampuni ya mawasiliano ya simu kwa 
njia ya mawasiliano kwa kutoa au kupokea sauti, maandishi, na picha au taarifa 
ya aina yoyote kupitia mfumo wa kielektronikia.
”Imesema taarifa hiyo 
iliyosainiwa na Vodacom, Airtel, Tigo na Zantel MOAT imesema eneo mojawapo 
litakaloathirika ni huduma za Intaneti eneo amablo linahitaji kuwekewa mikakati 
ya kulikuza kutokana na umuhimu wake katika maisha ya sasa kiuchumi na kijamii 
na wala sio kulizorotesha kwa kusababisha ongezeko la gharama na hivyo kuendelea 
kuwa na kiwango cha cha matumizi kilinganishwa na baadhi ya nchi nyengine 
zikiwemo za Afrika Mashariki.
 “Hatua hii ya 
kuongeza kodi itakwenda kinyume na mipango iliyopo yenye lengo la kuibadili 
jamii kwa kuipatia maarifa ya msingi kupitia huduma ya intaneti sambamba na 
mawasiliano ya simu.”
Kwa mujibu wa MOAT, 
Tanzania ni kati ya nchi zenye kiwango cha chini ya matumizi ya huduma ya 
mtandao wa intaneti katika bara la Afrika ambapo watumiaji wa huduma hiyo ni 
asilimia 10 pekee ikilinganishwa na nchi jirani ya Kenya ambayo ina zaidi ya 
watumiaji asilimia 40.
Aidha, 
MOAT imeongeza kuwa, “mawasiliano ya simu si anasa bali ni huduma muhimu katika 
Tanzania ya leo, sasa tunawezaaje kuwatozakodi mara kwa mara watu hao hao ambao 
wanaitegemea huduma hiyo ili kuboresha maisha yao? Ilihoji taarifa hiyo ya 
MOAT. 
Taarifa hiyo 
imeendelea kusema kuwa kwa tozo la kodi ya mapato ya asilimia 35 kwenye sekta 
hiyo ya mawasiliano ya simu linatosha kiasi ya kwamba sekta hiyo isngeweza 
kubeba mzigo zaidi wa ongezeko jingine.
Hivi sasa, upanuzi wa 
mawasiliano na miundombinu vijijini ndiyo kipaumbele cha sekta nzima. Tunaamini 
hapa ndipo ukuaji wa sekta ya mawasiliano ya simu itakapoonekana katika miaka 
ijayo. Ongezeko lolote la kodi litazorotesha uwezo wetu wa kutanua huduma zetu 
za mawasiliano na miundombinu maeneo ya vijijini, imesema MOAT.
“Tunaelewa kuwa serikali 
inayafanya haya yote ili kuweza kupata fedha kwa ajili ya kusaidia kwenye huduma 
za jamii katika maeneo muhimu. Ni bahati mbaya kwamba sekta ya huduma ya 
mawasiliano ya simu inaendelea kubeba mzigo mkubwa wa ongezeko hili ambapo 
wateja watalazimika kuelemewa na mzigo huo.
 

 
No comments:
Post a Comment