Pages

Translate

Saturday 15 June 2013

DKT. SHEIN AZINDUA TAMASHA LA MANGAPWANI



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Moh’d
Shein  amewataka wananchi wa  Mangapwani  kulinda, kuenzi na 
kuendeleza  Utamaduni wa asili wa Zanzibar ili kuweka historia kwa 
kizazi cha baadae.
 Dk. Shein  ameyase mahayo leo huko Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Wilaya   
ya kaskazini B Unguja, wakati alipokuwa  akizinduwa  Tamasha la Urithi  
la  wana kijiji cha Mangapwani linalohamasisha kuinua hali za maisha 
ya kijiji na kutunza historia ya kijiji hicho.
Amesema historia ni kitu muhimu sana kwa mwanadamu kufahamu yale 
yaliopita  ambayo yalikuwa muhimu na kutoa mchango mkubwa kwa wana
kijiji hivyo kuitunza historia ya watu wa Mangapwani ni jambo muhimu kwao
na Taifa kwani litapelekea kupata kipato kutokana na wageni (watalii )
wanaoingia kijijini hapo .
“Mambo ya asili yasitupwe yaendelezwe, leo vijana wanapoteza muelekeo kwa
kusahau ya zamamani walio kuwa wakiyafanya wazee  ambayo yaliwaongezea
afya kujenga miili yao kwa kula vya kula vya asili lakini leo chipsi  
zimetawala na vijana kuwa na matatizo ya kiafya kwa kula mafuta kuzidi  
kipimo.” alisema Dkt Ali Mohamed Shein.
Aidha Dkt. Shein alisema njia nzuri ya kuutunza na kuendeleza
utamaduni ni kutunga vitabu na kuviuza vitakavyoelezea Historia,
Tamaduni na Silka za  kijiji hicho ili wakija wageni kutoka nchi
mbalimbali wavikute na kujisomea.
 
Aidha Rais wa Zanzibar na Mwenyeki wa Baraza la Mapindunzi Dkt Ali
Muhamed Shein alisema kua matamasha kama hayo ni mazuri na ni muhimu
sana  kufanyika katika maeneo ya historia kwani hueleza hali halisi ya
sehemu kama hizo ambazo zilikaliwa na wakoloni kwa kufanya shughulizao
mbalimbali kama vile ulinzi na usalama.
 
“ Ngome sehemu ya Mangapwani ilitumika katika masuala kama vile ulinzi
na usalama kwa kujenga ghala la silaha ili kujilinda na
maaduwi”alisema Dkt Shein.
 
Hata hivyo Dkt Shein alimpongeza Rais mstaafu  Mzee Ali Hsani Mwinyi
kuwa mlezi wa tamasha hilo na kusema kua anamshukuru kwa ujasiri wake  kukubali kuwa mstari wa mbele na kuona tamasha hilo linafanikiwa .
 
Akijibu risala ya wana kijiji wa hapo juu ya kupatiwa eneo la ujenzi
wa chuo cha uvuvi na utengenezaji wa magari alisema jambo hilo ni zuri
na atamuagiza Waziri wa Ardhi Ramadhali Abdalla Shabani kuangalia
uwezekano wa kuwapatia wana kijijihicho eneo la kutimiza azma yao .
Nae Rais Mstahafu Ali Hassani Mwinyi alisema kuwa kuna haja ya kurejesha
hadhi ya Mangapwani  pamoja na mambo ya asili ambayo yamepotea kwa
siku nyingi .   Amesema mangapwani ya zamani si ile yaleo ambayo vivutio vyake vina   potea jambo ambalo kuna haja kubwa kutunzwa na wannchi kufaidika navyo.
"Irudishwe hadhi ya mangapwani kwani  mcheza kwao hutuzwa,” alisema Mzee Ali.   
 Aidha alisema  kua tamasha hilo ni kutafuta nia ya kuwawezesha
wanakijiji wa ukunda huo wa mangapwani na jirani zao kuwawezesha
kiutalii na utamaduni pamoja na kuwakumbuka wasanii marufu wataarabu
hapa Zanzibar.
Nae mwenyekiti wa Tamasha hilo  Mwinyi Jamal Nasib akisoma Risala
kwa niaba ya wanakijiji cha mangapwani kwenyetamasha hilo  alisema
malengo makuu ya Tamasha ni kurejesha utamaduni ulio potea
,asilizawatu wa hapo,kutafuta dawa ya kujikwamua na umasikini,
kuendeleza utalii na kujenga chuo cha kumuenzi Rais Mstaafu  Mzee Ali
Hssan Mwinyi ambae ni mlenzi wa Chuo hicho.

 
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment