Ni mwanajeshi kutoka Marekani,miaka ya hivi karibuni alikua vitani
ambapo alipoteza miguu yake miwili katika shambulio la bomu la kurushwa
kwa mkono,aliporudishwa nyumbani kwa matibabu akilini alishajua
amepoteza vingi maishani,akiwemo mkewe wa ndoa,ila tofauti na
alivyotarajia mkewe ndio alikua mstari wa mbele kuhakikisha mumewe
anapata matibabu stahiki na huduma zote muhimu,mpaka sasa mwanadada huyo
amekua ni gumzo na shujaa katika jamii inayomzunguka,je ni wangapi
mnaweza kufanya huu ushujaa pindi linapotokea tatizo kama hili?je
tunajifunza kutoka kwa wenzetu wanaotuzunguka? Wanandoa inatubidi kumaanisha wakati wakuoana na kutoa kiapo kama hiki kwani kiuhalisia katika maisha ya mwanadamu kuna kupanda na kushuka hivyo wakati wote tuwe tayari kupokea matokeo yoyote yatakayokuja mbele yetu. CHUKUA SOMO
No comments:
Post a Comment