HAWA NDIYO MASTAA WA BONGO WALIONASA MIMBA ZIKACHOLOPOKA PASIPO SABABU KUWEKWA WAZI..!!
DHAMIRA
 ya watu wengi ni kutunza mimba hadi kufikia hatua ya kujifungua lakini 
wakati mwingine ujauzito unaweza kuchoropoka kutokana na sababu tofauti,
 iwe kwa kukusudia au bahati mbaya.Kwenye maisha ya mastaa wetu wa Bongo, wapo waliowahi kupata mimba lakini kutokana na sababu tofauti, zilichoropoka.Amani linakumegea baadhi ya mastaa hao ambao wengine walianika sababu za mimba hizo kuchoropoka huku wengine wakifanya siri:
|  | 
| AUNT EZEKIEL | 
Februari,
 2011 aliripotiwa kuwa na ujuzito wa mwanaume ambaye mwenyewe hakumtaja 
lakini haikupita muda mrefu, mimba hiyo ilichoropoka pasipo kuweka wazi 
sababu.
|  | 
| JINI KABULA | 
Mwaka
 jana alijinadi kuwa na ujauzito wa Mbongo Fleva, Maximiliam Bushoke. 
Mimba hiyo ikadumu kwa miezi kadhaa, ghafla ikachoropoka yenyewe kwa 
bahati mbaya.
|  | 
| WEMA SEPETU | 
Kwa
 upande wake alitundikwa kibendi na aliyekuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul 
‘Diamond’ lakini miezi kadhaa mbele ikatoka yenyewe kutokana na sababu 
za kitaalam.
|  | 
| LULU | 
Mwaka
 jana aliripoti kwenye vyombo vya habari kuwa na mimba ya muigizaji 
mwenzake, marehemu Steven Kanumba. Wakati mapaparazi wakiendelea kufanya
 uchunguzi, ghafla ikadaiwa ‘kuyeyuka’ pasipo kujulikana chanzo.
|  | 
| LADY JAYDEE | 
Huyu
 ni mke halali wa Mtangazaji, Gardner Habash. Mwaka 2011 mitandao ya 
kijamii iliripoti kuwa ni mjamzito na kudaiwa kuwa habari hiyo ilimpa 
faraja mumewe lakini furaha hiyo iliyeyuka ghafla wakati Lady Jaydee 
akionekana na tumbo kubwa, ikadaiwa mimba imechoropoka bila sababu 
kutajwa.
|  | 
| Baby Madaha | 
Mwaka
 2010 mkali huyo wa filamu na muziki Bongo, alidaiwa kuwa na mimba 
ingawa mwenyewe hakutaka kuweka wazi lakini baadaye ilidaiwa kuwa 
alikwenda kuichoropoa nchini Kenya.
|  | 
| 
JACK WA CHUZ | 
Mapema
 mwaka huu aliripotiwa kuwa ni mjamzito lakini mwenyewe hakupenda kuweka
 mambo yake hadharani. Hata hivyo, vyanzo makini vilidai kuwa mimba hiyo
 ilikuwa ya mfanyabiashara mmoja jijini Dar lakini baadaye aliichoropoa 
pasipo kufahamika sababu. 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment