Mbakaji
 Erasto Mwakyomo (50) anayetuhumiwa kwa ubakaji akiwa akiwa katika ofisi ya mwenyekiti wa mtaa wa mapelele kabla ya kuchukuliwa na mwenyekiti wa dawati la watoto na ukatili wa kijinsia Bi. Mary Gumbo
 Mwenyekiti wa mtaa CHRISTOPHER MWAKIBETE 
 Baadhi ya ndugu na wazazi ya watoto wakiwa nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa
ERASTO
 MWAKYOMA mwenye umri wa miaka hamsini mkazi wa mtaa wa Mapelele Kata ya
 ILEMI jijini Mbeya anahojiwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za 
kuwadhalilisha watoto wawili wa kike wote wakazi wa Mapelele.
Wazazi
 wa watoto hao baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa watoto hao ambao 
mmoja ana umri wa miaka minne na mwingine mitano walitoa taarifa kwa 
Balozi wa mtaa Bwana CASIAN MWEZIMPYA ambapo baada ya kutafakari kwa 
kina aliamua kulipeleka suala hilo kwa Mwenyekiti wa Mtaa.
Mwenyekiti
 wa mtaa Bwana CHRISTOPHER MWAKIBETE Aliamua kuwaita wazazi na mtuhumiwa
 kuwahoji yaliyotukia ambapo nao watoto walipewa nafasi ya kueleza ambao
 walieza kuwa ERASTO Alikuwa akiwashika sehemu za siri na kuwapaka 
mafuta kabla ya kufanya nao mapenzi.
Baada
 ya kusikiliza kwa makini MWAKIBETE aliamuru kuwa suala hilo ni la 
kisheria na kitaalamu hivyo hawezi kuchukua hatua zozote bali suala hilo
 analazimika kulipeleka Polisi ambapo Mwenyekiti wa Dawati la watoto na 
jinsia MARY GUMBO Alimchukua mtuhumiwa hadi kituo cha Polisi kati.
Baada
 ya mahojiano ya awali GUMBO aliwachuchukua watoto hadi Hospitali ya 
Rufaa kwa uchunguzi na mtuhumiwa kubaki kituo cha kati kwa mahojiano 
zaidi,hata hivyo uchunguzi umebaini kuwa baadhi ya watoto mtaani hapo 
wamekuwa wakitendewa vitendo vya ukatili lakini vimekuwa vikifumbiwa 
macho na baadhi ya wazazi wakihisi ni aibu kwa watoto wao.
 

 
No comments:
Post a Comment