Pages

Translate

Thursday 15 August 2013

AWAPAKA MAFUTA WATOTO SEHEMU ZA SIRI NA KUWALAWITI


Mbakaji Erasto Mwakyomo (50) anayetuhumiwa kwa ubakaji akiwa akiwa katika ofisi ya mwenyekiti wa mtaa wa mapelele kabla ya kuchukuliwa na mwenyekiti wa dawati la watoto na ukatili wa kijinsia Bi. Mary Gumbo
WATOTO WALIOKUWA WAKIBAKWA WAKITOA MAELEZO JINSI WALIVYOKUWA WAKITENDEWA
 Mwenyekiti wa mtaa CHRISTOPHER MWAKIBETE
 Baadhi ya ndugu na wazazi ya watoto wakiwa nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa


ERASTO MWAKYOMA mwenye umri wa miaka hamsini mkazi wa mtaa wa Mapelele Kata ya ILEMI jijini Mbeya anahojiwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuwadhalilisha watoto wawili wa kike wote wakazi wa Mapelele.
Wazazi wa watoto hao baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa watoto hao ambao mmoja ana umri wa miaka minne na mwingine mitano walitoa taarifa kwa Balozi wa mtaa Bwana CASIAN MWEZIMPYA ambapo baada ya kutafakari kwa kina aliamua kulipeleka suala hilo kwa Mwenyekiti wa Mtaa.
Mwenyekiti wa mtaa Bwana CHRISTOPHER MWAKIBETE Aliamua kuwaita wazazi na mtuhumiwa kuwahoji yaliyotukia ambapo nao watoto walipewa nafasi ya kueleza ambao walieza kuwa ERASTO Alikuwa akiwashika sehemu za siri na kuwapaka mafuta kabla ya kufanya nao mapenzi.
Baada ya kusikiliza kwa makini MWAKIBETE aliamuru kuwa suala hilo ni la kisheria na kitaalamu hivyo hawezi kuchukua hatua zozote bali suala hilo analazimika kulipeleka Polisi ambapo Mwenyekiti wa Dawati la watoto na jinsia MARY GUMBO Alimchukua mtuhumiwa hadi kituo cha Polisi kati.
Baada ya mahojiano ya awali GUMBO aliwachuchukua watoto hadi Hospitali ya Rufaa kwa uchunguzi na mtuhumiwa kubaki kituo cha kati kwa mahojiano zaidi,hata hivyo uchunguzi umebaini kuwa baadhi ya watoto mtaani hapo wamekuwa wakitendewa vitendo vya ukatili lakini vimekuwa vikifumbiwa macho na baadhi ya wazazi wakihisi ni aibu kwa watoto wao.

No comments:

Post a Comment