Moshi.
 Mashahidi wawili wa upande wa mashtaka, wameieleza mahakama namna 
wanyamahai, wakiwamo twiga wanne, walivyosafirishwa kwenda Doha nchini 
Qatar kwa kutumia ndege ya jeshi.
Mashahidi
 hao, akiwamo mmoja wa madereva wa lori, walitoa ushahidi wao juzi 
wakiongozwa na jopo la mawakili watatu wa Serikali, Evetha Mushi, Pius 
Hilla na Stella Majaliwa.
Shahidi
 wa sita, Davis Kimei aliyekuwa dereva wa lori aina ya Mitsubish Fusso, 
alieleza namna alivyosafirisha wanyama hao toka Arusha hadi Uwanja wa 
Ndege wa Kilimanjaro (Kia).
Mbele
 ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Simon Kobelo shahidi huyo alidai Novemba 25, 
2010 alikodishwa kubeba wanyama hao na watu watatu, wakiwemo wawili 
wenye asili ya kiasia hadi uwanja wa Kia kwa ujira wa Sh150,000.
“Baada
 ya kuelewana tulikwenda hadi kwenye nyumba moja eneo la Kwamrefu, 
Arusha na humo ndani nilikuta vijana wengi ambao walikuwa wakitengeneza 
mabox yaliyokuwa na Twiga na Swala,” alisema.
Shahidi
 huyo alidai baada ya kuwapakia wanyama hao, msafara wa malori manne 
ulielekea Kia na kufika saa 8:00 usiku na kuelekea moja kwa moja 
uwanjani ambapo walikuta ndege kubwa ya jeshi imeegeshwa.
“Maboksi yale yalishushwa na kupakiwa katika ndege hiyo usiku ule wa manane,” alisema.
Shahidi
 wa saba, alidai siku ya tukio saa 4:00 usiku aliwasikia wafanyakazi 
wawili uwanjani hapo, wakisema kuna wanyama wangesafirishwa usiku huo.
“Nilimdokeza
 mkuu wa upelelezi… Nilipokuwa nyumbani bosi wangu alinipigia simu na 
kuniambia ile taarifa niliyompa ilikuwa ni ya kweli kuna ndege ya 
Serikali inasafirisha wanyamapori,” alisema.
Shahidi
 huyo alidai kuwa saa 6:00 usiku alirudi kazini na ilipofika saa 8:30 
usiku lilikuja basi aina ya Toyota Coaster ambapo walishuka watu wenye 
sare za jeshi wenye asili ya kiarabu.
Washtakiwa
 katika kesi hiyo inayovuta hisia za Watanzania wengi ni Kamran Ahmed, 
Hawa Mang’unyuka, Michael Mrutu na Patrick Paul na kesi hiyo itaendelea 
kusikilizwa Agosti 13 na 14.
 
 
No comments:
Post a Comment