Chadema
 cha Demokdrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesisitiza kuwa kitasimamia 
azimio la kikao cha Kamati Kuu yake kuhusu kuimarisha kitengo chake cha 
ulinzi na usalama na kuibua nyaraka ‘nyeti’ za Chama Cha Mapinduzi (CCM)
 zinazoweka hadharani mikakati ya CCM kufundisha vijana kukabiliana na 
wapinzani. Pia
 kimemtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuachia madaraka kama amechoka 
kuendelea kuwa kiongozi anayepaswa kusimamia misingi ya uongozi bora, 
ikiwamo kufuata haki za binadamu, sheria na demokrasia kwa ajili ya 
ustawi wa jamii ya Watanzania. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, 
aliyasema hayo wakati akihutubia mkutano wa hadhara, katika viwanja vya 
Mahakama ya Mwanzo, Nguzo Nane, mjini Shinyanga juzi. Alisema
 ili kujilinda dhidi ya vitendo alivyodai wanafanyiwa na vijana wa Green
 Guards wanaotoka kikosi cha vijana wa CCM, Chadema itaendelea na 
mipango ya kuwapa vijana wake mafunzo ya ukakamavu.
        Katika mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya wakazi wa mji huo 
na vitongoji vyake, Mbowe alionyesha nyaraka mbili za CCM zinazoonyesha 
kuwa chama hicho kupitia wanachama wa Umoja wa Vijana (UVCCM), kimekuwa 
kikitoa mafunzo ya ukakamavu kwa vijana wake, huku nyaraka moja 
ikionyesha kuwa moja ya malengo ya mafunzo hayo ni kukabiliana na 
upinzani. “Tunashambuliwa, watu wetu wanapigwa, wanateswa, wanatekwa na 
wengine kuuawa, kwa sababu tu wanataka mabadiliko na wanapenda Chadema,”
 alisema Mbowe na kuongeza: “Majuzi mlisikia Waziri Mkuu, Pinda anasema 
wamechoka...sasa tunasema, Pinda  kama umechoka ondoka upishe ofisi ya 
umma hiyo, upishe kwenye ofisi ya watu kama umechoka. Maana kuchoka huko
 ni kuchoka kwa CCM. Pisheni ofisi siyo za kwenu hizo, ni za 
Watanzania.”
      “Wananchi 
hapa mkononi nimeshika nyaraka mbili za CCM. Moja ni cheti cha kuhitimu 
mafunzo na nyingine hapa juu imeandikwa: ‘Sera za Msingi za CCM’. Sasa 
mi sitawasomea. Naomba aje hapa jukwaani mtu yeyote anayejua kusoma, 
awasomee mjue tunaposema CCM wamekuwa na kikundi kinachoshambulia, 
kupiga, kutesa, kuteka na hata kuua Watanzania wenzao eti tu kwa sababu 
wanaunga mkono Chadema, huwa tunamaanisha nini.” Mmoja
 wa wananchi aliyehudhuria mkutano huo wa hadhara, ambao ulikuwa ni 
sehemu ya shughuli za ukamilishaji wa kuzindua Kanda ya Ziwa Mashariki 
(mikoa ya  Shinyanga, Simiyu na Mara), alipewa kabrasha kubwa 
lililoandikwa: “Sera za Msingi za CCM” na kusoma sehemu inayozungumzia 
majukumu ya jumuiya za chama hicho.
Kifungu cha 9.1 kinachozungumzia UVCCM kinasomeka kuwa:
        ‘Umoja wa vijana wa CCM unapaswa kuwajenga vijana katika 
itikadi, ukakamavu na mafunzo yatakayowafanya wajiamini, wawe vijana 
wenye ari ya kutimiza wajibu wao wakiwa walinzi wa wa chama, viongozi na
 wagombea wa CCM.’ ‘Utaratibu wa kuandaa makambi ya vijana usimamiwe kwa
 dhati. Chama kiwe na mipango mizuri ya kutafuta na kuwateua wakufunzi 
watakaofaa kuwapatia vijana mwelekeo unaotakiwa ikiwa ni pamoja na elimu
 ya uchaguzi/uraia.’  ‘Mafunzo ya makambi ya vijana, mbali ya kujifunza 
nyimbo za hamasa yatilie mkazo pia mafunzo ya ukakamavu kwa lengo la 
kukabiliana na vitendo vya kihuni vya baadhi ya vijana wa vyama vya 
upinzani,’ inasomeka sehemu ya kitabu hicho cha CCM. Mbowe pia alimwomba
 mtu huyo asome cheti cha mmoja wa wahitimu wa kile alichodai ni mafunzo
 ya makambi ya vijana wa CCM.
     Cheti hicho kinaonyesha mhitimu alianza mafunzo Juni 27, 2009 na 
kumaliza Julai 4, 2009, Wilaya ya Dodoma mjini, kimesainiwa na watu 
wawili; mmoja mwenye jina la Jumanne Kitundu, akiwa ni Katibu wa UVCCM, 
Dodoma Mjini na mwingine, ni Robert Mwinje, Mwenyekiti wa Umoja huo 
Wilaya ya Dodoma Mjini. Pia cheti hicho kinaonyesha mhusika (jina 
linahifadhiwa) alihitimu mafunzo ya kanuni ya UVCCM, wajibu wa vijana 
katika chama, ulinzi na usalama, ujasiriamali, ukakamavu, wajibu wa 
vijana katika uchaguzi, rushwa, Ukimwi, historia ya Tanu na ASP pamoja 
na maadili. Katika mkutano huo, Mbowe aliwataka Watanzania kuacha 
kugombana kwa sababu ya vyama, badala yake wasumbuliwe na waunganishwe 
pamoja na matatizo yanayowakabili sasa, ambayo alidai yanasababishwa na 
uongozi mbovu wa CCM.
     Alisema Chadema inajiandaa kusambaza ushahidi ilionao wenye tuhuma 
nzito dhidi ya CCM kushindwa kufanya siasa na kuongoza nchi, badala yake
 imekuwa ikishambulia, kupiga, kutesa, kuteka na hata kuua 
watu. Ushahidi huo umewekwa kwenye kitabu kimoja ambacho kwa mujibu wa 
Mbowe, kitatolewa nakala nyingi, kinaonyesha matukio mbalimbali ya 
kisiasa ambayo wananchi wamepigwa, wameumizwa na wengine kuuawa katika 
shughuli za siasa, huku uchunguzi huru ukiwa haujawahi kufanyika kubaini
 wahusika wa matukio hayo na sheria kuchukua mkondo wake. Mwenyekiti wa 
Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), John Heche, katika mkutano huo, 
aliifananisha kodi mpya ya kadi za simu kuwa ni zaidi ya iliyokuwa kodi 
ya kichwa ambayo ilifutwa.
 

 
No comments:
Post a Comment