 Habari kutoka Dodoma zinasema Mbunge wa Kasulu Mjini kupitia chama cha  NCCR-Mageuzi, Mhe. Moses Machali (pichani), amelazwa katika hospitali ya mkoa ya Dodoma kuuguza majeraha aliyoyapata baada ya kushambuliwa na  watu wasiojulikana jana  jioni  mjini Dodoma.
Habari kutoka Dodoma zinasema Mbunge wa Kasulu Mjini kupitia chama cha  NCCR-Mageuzi, Mhe. Moses Machali (pichani), amelazwa katika hospitali ya mkoa ya Dodoma kuuguza majeraha aliyoyapata baada ya kushambuliwa na  watu wasiojulikana jana  jioni  mjini Dodoma.
 Tukio hilo lilitokea jana jioni  wakati Mh. Machalli  akiendesha gari lake mita kadhaa kutoka ilipo nyumba anayoishi baada ya  kuwapigia honi vijana kadhaa waliokuwa wakitembea katikati ya barabara  ili wasogee pembeni naye aweze kupita ....
 Kitendo hicho  kilionekana  kuwaudhi na kuwakera vijana hao ambao walianza kuipiga na kuigonga kwa  nguvu bodi ya gari ya Mh. Machalli jambo ambalo lilimfanya Machalli  kusimamisha gari na kushuka ili kujua kulikoni ....
 Baada ya kushuka, vijana  hao walimtolea  matusi kadhaa ya nguoni na pindi machalli alipowajibu kwa  hasira ndipo kipigo kikali kilipoanza. 
Shuhuda aliyekuwa jirani na eneo la tukio anasema Mh. Machalli alipigwa na vijana zaidi ya nane jambo ambalo lilipelekea hata yeye kushindwa kumsaidia kwa kuhofia kuunganishwa katika kipigo.
Shuhuda aliyekuwa jirani na eneo la tukio anasema Mh. Machalli alipigwa na vijana zaidi ya nane jambo ambalo lilipelekea hata yeye kushindwa kumsaidia kwa kuhofia kuunganishwa katika kipigo.
Mhe Mbatia amesema leo mjini Dodoma kwamba amemtembelea Mhe. Machali asubuhi hii na kumkuta anaendelea vyema na matibabu.
 
 
No comments:
Post a Comment