KAWAWA, NKUMBA WADAIWA KUJILIPA MAMILIONI TTB
 
    MJADALA wa Bunge jana jioni ulitawaliwa na kauli nzito baada ya 
wabunge kadhaa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kutuhumiana kuhusika na 
ubadhirifu katika vyama vya ushirika nchini. Hoja
 hiyo iliibuka wakati Bunge likijadili muswada wa sheria ya vyama vya 
ushirika wa mwaka 2013 uliowasilishwa na Waziri wa Kilimo, Chakula na 
Ushirika, Balozi Christopher Chiza. Aliyekuwa
 wa kwanza kuwasha moto huo baada ya mapumziko ya mchana alikuwa mbunge 
wa Busega, Dk.Titus Kamati (CCM), ambaye alisema waziwazi kuwa wanasiasa
 ndio wezi wa vyama vya ushirika. Dk.
 Kamani alihoji ni kwa nini serikali inapata kigugumizi kuwachukulia 
hatua wahusika na kusisitiza kuwa hapo kuna kulegalega kumaliza ufisadi 
katika ushirika.
 
      “Wanasiasa hawa kwa nafasi zao wameingia kwenye ushirika na 
kufanya ufisadi lakini serikali inashindwa kuwachukulia hatua. “Huku
 ni kulegalega na ndio maana hata tumeshindwa kuwataja wauza dawa za 
kulevya, waziri anaishia kusema tunayo orodha,” alisema. Alihoji
 ni kwa nini sasa serikali isiige mfano wa China wa kuwafunga na hata 
ikibidi kuwanyonga watuhumiwa wa ufisadi wa vyama hivyo ikithibitika 
bila kujali nafasi zao kwenye siasa. Mbunge
 wa Mpanda Vijijini, Moshi Kakoso (CCM), ndiye aliyefuata na kuchafua 
hali ya hewa kwa kumtuhumu Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Nchini (TTB) 
kufanya ufisadi mkubwa ambao serikali inaujua lakini imeamua 
kuunyamazia. Bila
 kumtaja kwa jina lakini alikuwa akimlenga mbunge mwenzake wa Namtumbo, 
Vita Kawawa, akisema kuwa anajilipa mshahara mara mbili ya ule 
uliopitishwa na serikali.
 
     Alisema kuwa analipwa sh milioni mbili za mawasiliano na anachukua 
dola 1200 (zaidi ya sh milioni 1.8) kwa ajili nyumba badala ya sh 
800,000 zilizoidhinishwa. Mbunge huyo alisema mwenyekiti huyo anayajua mambo hayo na ndiye aliyeidhinisha. “Nina
 uhakika na ninachozungumza, waziri nilishamletea taarifa juu ya jambo 
hili lakini amenyamaza, hivi hapa tunategemea ushirika utakuwa hai 
wakati mabosi wanautafuna?” alihoji. Wakati mbunge huyo anaendelea kuzungumza, Kawawa akitaka kumpa taarifa juu ya jambo analolizungumza. Kawawa
 alisema muda wake wa kuwa mwenyekiti kwenye bodi hiyo uliisha Juni 31 
mwaka huu, hivyo ni vema mbunge mwenzake akatoa ushahidi wake juu ya 
tuhuma za watendaji wa bodi husika. Baada
 ya Kawawa kumaliza, Kakosa aliendelea kuchangia ambapo alikataa taarifa
 hiyo kwa madai ana ushahidi wa kile kilichofanyika.
 
     Mara baada ya Kakoso kumaliza kuchangia muswada huo, mbunge wa 
Kondoa Juma Nkamia alipewa fursa ya kutoa taarifa ambapo alisema tuhuma 
zilizotolewa na Kakoso dhidi ya Kawawa ni nzito sana na Bunge lipate 
fursa ya kuangalia jambo hilo pamoja na mhusika kutoa ushahidi. Naibu Spika, Job Ndugai, alisema ofisi ya Bunge iko wazi kwa Kakoso kuwasilisha ushahidi wake juu ya kile alichosema. Mara
 baada ya Ndugai kutoa ufafanuzi huo, alimpa nafasi mbunge wa Sikonge, 
Saidi Nkumba (CCM), ambaye alimtuhumu Kakoso kwa kushindwa kuliambia 
ukweli Bunge kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Chama Kilele (APEX) ambacho 
kinapigiwa kelele kuwa kinawanyonya wakulima. Alisema
 wakiwa Dar es Salaam kwenye vikao vya kamati za Bunge, Katibu wa Apex, 
aliitwa katika kamati kama mdau ambapo alipobanwa juu ya wizi 
unaofanyika kwenye chombo hicho alisema serikalini ikiiba kelele 
zinapigwa lakini APEX ikiiba kidogo kelele zinakuwa kubwa sana.
 
      “Katibu wa Kakoso ndiye aliyetuambia hivyo. Huu ni wizi, sisi 
hatuwezi kukubaliana na jambo hilo, serikali haivumilii wizi, huyu 
Kakoso anasema APEX ni mkombozi lakini pale Tabora wamewaibia wananchi 
bilioni 16, hivi kweli hizi si fedha nyingi? “Hii
 APEX ni lazima ifutwe, wenye tamaa ya kwenda kwenye ushirika ni vema 
waache siasa, na wenye ushirika ni vema wakabaki huko huko.” Alibainisha
 kuwa wizi unaofanyika kwenye vyama vya ushirika unasababishwa na 
wanasiasa ambao wana kinga za kisiasa ndiyo maana wanaendelea kutafuna 
fedha za wananchi. Mbunge
 wa Kasulu Mjini, Moses Machali, alisema wabunge wana taarifa za wizi 
wanatoa taarifa hapa bungeni lakini hakuna wanachokifanya. “Yaani
 kila kukicha mnalea wizi halafu leo hii mnaanzisha tume za kuwanyonya 
wakulima, kule kwangu wakulima waliuza tumbaku, msianzishe vitu vya 
ajabu ajabu…, huu ni wizi mtu, msituletee wizi hapa kwa kubadilisha 
majina ya vitu,” alisema.
 
     Tundu Lissu wa Singida Mashariki (CHADEMA) alisema sababu kubwa ya 
kuporomoka kwa ushirika ni serikali kuuingilia, kuudhibiti na 
kuuporomosha. Alisema
 serikali ilianza kuvuruga mambo 1966 sheria za ushirika ilibadilishwa 
na msajili wa vyama vya ushirika alipewa mamlaka ambayo alianza 
kuyatumia vibaya ambapo mwaka 1976 alipigwa marufuku zikaja bodi za 
mazao. Mwaka 1982 vilirejeshwa vyama vya ushirika lakini mamlaka yake yalikuwa yakitolewa na mrajis ambaye ni serikali. Mbunge
 wa Nzenga, Andrew Kigwangalah, aliibua upya mzozo wa awali kwa kuanika 
nyaraka za ufisadi katika TTB kama ilivyokuwa imedokezwa awali na 
Kakoso. Kingwangalah
 ambaye alidai kuwa hatarudi nyuma kuwataja mafisadi na wauza dawa za 
kulevya alisema kuwa kodi ya nyumba ya mwenyekiti wa bodi inalipiwa 
gahara tofauti na ile iliyoidhinishwa.
 
     Alionyesha nyaraka kadhaa za malipo ya viongozi wa bodi hiyo na 
kisha kumvaa Nkumba akisema kuwa tatatizo la nchi hii si Apex bali ni 
rushwa, wizi, ubadhirifu halafu watu wanaona wizi wanaungalia badala ya 
kuchukua hatua. “Waliobaki kwenye ushirika ni wezi watupu, wazalendo wameisha, wezi tunawajua lakini hatuwawajibishi wala kuwachukulia hatua. “Nkumba
 ni msaidizi wa Kawawa katika bodi ya tumbaku anajua ukaguzi 
haujafanyika na ukifanyika wao hawatasalimika ndiyo maana wanaanza 
kuipiga vita Apex. “Kuna
 watu wanatumiwa na kampuni za ubebari ambazo zilikuwa zikisafirisha 
tumbaku na kusambaza pembejeo, hawa sasa wanaona hatari za kampuni zao 
ndiyo maana zinawatumia wabunge ili APEX ifutwe, tuwe makini na wabunge 
waovu,” alisema.
 
     Mzozo huo ulidumu huku Kawawa na Nkumba wakisimama kujitetea bila 
mafanikio hatua iliyomlazimu Naibu Spika wa Bunge kutoa nafasi kwa 
baadhi ya wabunge kuomba viongozi, lakini akaliahirisha Bunge hadi leo 
ambapo atatoa uamuzi wake. Mapema
 asubuhi, wabunge walipendekeza wabadhirifu wa mali za ushirika 
walazimishwe kufidia hasara iliyotokea pamoja na kufilisiwa mali zao. Pendekezo
 hilo limetolewa na Nkumba alipokuwa akisoma hotuba ya Mwenyekiti wa 
Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Peter Msolla. Nkumba
 alisema ushirika umewakatisha tamaa wananchi kutokana na ubadhirifu wa 
viongozi wake hivyo ujio wa sheria hiyo utakuwa mkombozi.
 
    Aliongeza kuwa watuhumiwa wa ubadhirifu wa ushirika wafikishwapo 
mahakamani mashauri yake yamekuwa hayathibitiki licha ya taarifa za 
fedha kuonyesha kuwa upotevu fedha upo; ni vema kuwepo na utaratibu wa 
kuwabana wahusika. Nkumba
 alisema vyama vya ushirika vimekuwa vikikaguliwa na Shirika la Ukaguzi 
na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (Coasco) ambalo halifanyi kazi zake 
vizuri na kuitaka serikali kuweka utaratibu mzuri ikiwemo kuhusishwa kwa
 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali. Waziri wa Kilimo, Chiza alisema kuundwa kwa sheria hiyo litakuwa suluhisho la matatizo ya ushirika nchini. Alisema
 serikali inalenga kuifuta sheria ya vyama vya ushirika namba 20 ya 
mwaka 2003 na inaamini sheria mpya itaimarisha, kuendeleza na kuufufua 
ushirika. Chiza
 alisema sheria ya ushirika ya mwaka 2013 ina lengo la kutekeleza sera 
ya maendeleo ya ushirika ya mwaka 2002, inayovitaka  vyama vya ushirika 
imara, endelevu na vyenye kukidhi mahitaji ya wanachama kiuchumi chini 
ya mazingira ya soko huria.
 
 
No comments:
Post a Comment