Habari hii inatokea Nchini Kenya ambapo Msichana mwenye
umri wa miaka 14 Mwanaharabu Wamukoya kutoka katika
kijiji cha Harambee katika wilaya ya Kakamega amejifungua
watoto watatu wote wakiwa ni Wavulana wawili kati yao
wamezaliwa wakiwa na uzito wa 1.5 kilogram na mwingine
akiwa na uzito wa Kilogram 1.3.
Nesi wa zamu katika Hospitali hiyo ya Bugoma Bi,Mary
Marumbu alisema Watoto hao pamoja na Mama yao wanaendelea
vizuri na wakati wowote wanaweza kuluhusiwa kutoka Hospitalini
hapo. Mshangao zaidi ni pale ilipokuja kujulikana kwamba Baba
Mzazi wa watoto hao watatu waliozaliwa bado ni mtoto mdogo
kama alivyo Mama yao kwani Baba yao ana Umri wa Miaka 16
ambae pia bado anasoma,Zaidi aliishukuru sana Serikali kwa
kuweza kuondoa garama kwa wajawazito wakiwa wanajifungua
na ivyo kuweza kumuwezesha mzazi mwenzie kujifungua pasipo
Garama zozote zile.
|
No comments:
Post a Comment