Pages

Translate

Wednesday 4 September 2013

MTOTO WA MIAKA 14 AZAA MAPACHA WATATU.BABA PIA NI MTOTO ANA MIAKA 16.


Habari hii inatokea Nchini Kenya ambapo Msichana mwenye 

umri wa miaka 14  Mwanaharabu Wamukoya kutoka katika 

kijiji cha  Harambee katika wilaya ya Kakamega amejifungua 

watoto watatu wote wakiwa ni Wavulana wawili kati yao

 wamezaliwa wakiwa na uzito wa 1.5 kilogram na mwingine 

akiwa na uzito wa Kilogram 1.3.

Nesi wa zamu katika Hospitali hiyo ya Bugoma Bi,Mary 

Marumbu alisema Watoto hao pamoja na Mama yao wanaendelea 

vizuri na wakati wowote wanaweza kuluhusiwa kutoka Hospitalini 

hapo. Mshangao zaidi ni pale ilipokuja kujulikana kwamba Baba 

Mzazi wa watoto hao watatu waliozaliwa  bado ni mtoto mdogo 

kama alivyo Mama yao kwani Baba yao ana Umri wa Miaka 16 

ambae pia bado anasoma,Zaidi aliishukuru sana Serikali kwa

 kuweza kuondoa garama kwa wajawazito wakiwa wanajifungua 

na ivyo kuweza  kumuwezesha mzazi mwenzie kujifungua pasipo

 Garama zozote zile.

No comments:

Post a Comment