WATOTO WANNE WA SHULE YA MSINGI WAMBAKA MWENZAO WA DARASA LA PILI MPAKA KUPOTEZA FAHAMU..!!
MATUKIO
 ya uvunjifu wa maadili kwenye shule mbalimbali hapa nchini yameendelea 
kushamiri baada ya wanafunzi wanne wa Shule ya Msingi Lulanzi wilayani 
Kibaha mkoani Pwani kutuhumiwa kumbaka mwanafunzi wa darasa la pili na 
kumsababishia maumivu yaliyopelekea kulazwa Hospitali ya Tumbi kwa 
matibabu.
Akizungumza
 na mwandishi wa habari hizi jana babu wa mtoto huyo, Jacob Mrope 
alisema tukio hilo lilitokea Septemba 2 saa 6 mchana ambapo mjukuu wake 
ambaye ni yatima alikuwa akitoka shuleni huku akiwa na wenzake wawili 
wakike, walikimbizwa na watuhumiwa hao ambapo yeye alishindwa kukimbia 
kutokana na kuumia mguu na kujikuta akibakwa.
Mrope
 alisema kuwa wanafunzi wenzake aliokuwa nao walisema kuwa baada ya 
watuhumiwa hao kumkamata walimziba mdomo kisha wakaanza kumuingilia kwa 
zamu ambapo mwanafunzi huyo hakuweza kupata msaada wowote hadi 
watuhumiwa hao kutimiza haja zao.
"Wenzake
 waliokuwa nao walitoa taarifa nyumbani kwa mlezi wake ambaye ni dada 
yake ambapo alikwenda na kumkuta akitokwa na damu nyingi na alipomuuliza
 alisema kuwa wenzake wamembaka ndipo alimchukua na kumpeleka shuleni 
kutoa taarifa," alisema Mrope.
Kwa
 upande wake dada yake Lwiza alisema kuwa yeye alipata taarifa kupitia 
kwa wanafunzi hao ambao alikuwa nao wakati wanatoka shule na kukimbizwa 
na watuhumiwa hao, ambapo walisema kuwa ilibidi warudi na kumkuta 
mwenzao akitokwa damu, wamkokota mwenzao hadi nyumba iliyojirani na 
kumjulisha.
"Alikuwa
 kwenye hali mbaya kwani alikuwa akitokwa na damu nyingi na 
nilipomuuliza alisema kuwa amebakwa na mtuhumiwa ambaye alimtambua na 
kumtaja jina mwenye umri wa miaka 10 akiwa na wenzake watatu," alisema 
Lwiza.
Lwiza
 alisema kuwa baada ya kuona hali ile walimpeleka shule na uongozi wa 
shule ukamwelekeza kufuata taratibu za kisheria ambapo walikwenda 
Serikali ya mtaa kisha kwenda polisi na baadaye Hospitali ya Tumbi kwa 
matibabu zaidi ambapo hadi juzi mwanafunzi huyo alikuwa bado kalazwa na 
hali yake inasemekana kuwa ni mbaya.
Naye
 Mwalimu mkuu wa shule hiyo ya Lulanzi, Anna Bilali alisema kuwa wao 
kama uongozi wa shule hawawezi kusema lolote kwani suala hilo liko 
kwenye vyombo vya sheria pamoja na kitabibu na watakuwa tayari kusema 
mara taarifa zitakapokamilika.
"Ni
 kweli tukio hili limetokea lakini bado haijathibitishwa kama ni kweli 
au la na pia lilitokea nje ya shule na muda wa shule kwa wanafunzi wa 
madarasa ya chini walisharuhusiwa kurudi nyumbani mara baada ya masomo 
kwisha," alisema Bilali.
Akizungumzia
 tukio hilo mjumbe wa mtaa wa Lulanzi, Rasul Shaban alisema kuwa 
walipata taarifa hiyo na kushangazwa na kitendo hicho ambapo tukio hilo 
ni la mara ya kwanza kutokea katika shule hiyo ambayo iko kwenye mtaa 
huo na pia walitoa barua za kuwadhamini wanafunzi wanaotuhumiwa kufanya 
tukio hilo.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alisema kuwa hadi sasa wanawashikilia wanafunzi wanne wenye umri kati ya miaka 10 na 13 kuhusiana na tukio hilo.
Source: Majira
 

 
No comments:
Post a Comment