LADY JAYDEE, AFANDE SELE, MKOLONI NA JB WAKIMBILIA CHADEMA

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeendelea kuwavuta wasanii kujiunga na chama hicho, ambapo sasa wasanii wanne wa muziki wa kizazi kipya, maarufu Bongofleva na filamu, wanatarajiwa kutangazwa kuhamia chama hicho wiki hii.
Wasanii
 hao wanadaiwa tayari kukubali kuingia kwenye chama hicho na 
wanatarajiwa kutangazwa rasmi hadharani katika mkutano wa hadhara 
utakaofanyika jijini Dar es Salaam.
Kukubali
 kwao kuingia katika siasa, kunatajwa kutokana na ushawishi mkubwa 
uliofanywa na wabunge vijana wa chama hicho, pamoja na Diwani wa CCM 
kutoka kata moja ya Wilaya ya Kinondoni, ili chama hicho kivune kura za 
vijana katika uchaguzi mkuu wa 2015.
Wabunge
 hao wa Chadema na majimbo yao katika mabano ni Halima Mdee (Kawe); 
Kabwe Zitto (Kigoma Kaskazini); John Mnyika (Ubungo) na Joseph Mbilinyi,
 jina la kisanii Sugu (Mbeya Mjini).
Habari
 kutoka kwa watu wa karibu na wasanii hao pamoja na ndani ya Chadema, 
zinawataja wasanii hao kuwa ni wanamuziki Judith Wambura maarufu Lady 
Jaydee na wa miondoko ya Hip hop, Selemani Msindi ama Afande Sele.
Taarifa
 zinawataja wengine kuwa ni mwanamuziki Fredy Maliki maarufu Mkoloni na 
mwigizaji wa filamu, Jacob Steven kwa jina la kisanii JB.
Inadaiwa
 wasanii hao lengo la kuingia katika siasa kupitia chama hicho, ni 
kuwania ubunge ambapo Jaydee anatajwa kutaka kugombea wilayani Musoma; 
Afande Sele Morogoro Mjini; Mkoloni Jimbo la Tanga na JB Jimbo la Mkoa 
wa Dar es Salaam.
Hata
 hivyo gazeti hili lilipowatafuta kuzungumzia taarifa hizo wote walikana
 ingawa wapo waliokiri kushawishiwa kuingia kwenye chama hicho na 
viongozi wa Chadema na wananchi, ili wagombee ubunge.
 Afande
 Sele alikana kujiunga na chama hicho na kusema hana taarifa hizo 
isipokuwa ni kweli ameshawahi kufuatwa na viongozi wa Chadema wa Mkoa wa
 Morogoro, wakimtaka ajiunge na chama hicho na agombee ubunge Morogoro 
Mjini.
“Nimeshafuatwa
 na viongozi wa Chadema wa mkoa na kata nijiunge na chama hicho na 
nigombee ubunge …tena hata vijana wengi na baadhi ya wazee wamenitaka 
nigombee ubunge kwa kupitia Chadema lakini nimekataa.
“Pia
 Sugu ni mshikaji wangu na anapokuja Morogoro, vijiwe vyake ndio vyangu 
naye vijana wameshamfuata wakimwambia anishawishi nigombee ubunge 
kupitia Chadema, amekuwa akiniambia vijana wananitaka lakini mimi 
sitaki, sijawahi kujiunga na chama chochote na naona mbunge wa sasa 
(Abdulaziz Aboud) anafanya kazi nzuri.
“Mimi
 sio mwanasiasa, lakini ni mwanaharakati kupitia muziki na mtandaoni na 
nimekuwa nikitoa maoni mengi na kukosoa lakini narudia si mwanasiasa na 
sijawahi kujiunga na chama chochote,” alisema Afande Sele.
Vilevile
 amekanusha kushawishiwa na viongozi wa kitaifa wa Chadema au wabunge, 
ingawa amekiri kuna wabunge wa chama hicho kuwa ni marafiki zake 
wakiwemo Mbilinyi na Zitto.
Kwa
 upande wa Jaydee alisema hafuati itikadi ya chama chochote cha siasa na
 hapendi siasa kutokana na imani kuwa siasa ni uongo na yeye hapendi 
uongo. Alisema hana nia ya kujiunga na chama chochote cha siasa wala 
kugombea ubunge kupitia chama chochote.
Hata hivyo alipoulizwa iwapo atagombea baada ya Katiba kuruhusu mgombea binafsi, alisema kwa wakati huo atajua.
Hata
 hivyo, Licha ya kuwaona wanasiasa ni waongo, anakiri wapo wanasiasa 
anawaamini kutokana na kazi zao na kumtaja miongoni mwao ni Mwenyekiti 
wa UDP, John Cheyo na Mbunge wa Afrika Mashariki, Shy-rose Bhanji.
Mwanamuziki
 huyo alisema licha ya kuwa na marafiki wa Chadema na CCM kama Sugu na 
Profesa Jay wa Chadema na Mbunge wa Viti Maalumu, Catherine Magige na 
Bhanji wa CCM, hawajawahi kumshawishi kujiunga na vyama vyao. 
Mkoloni
 Akizungumzia taarifa hizo za kujiunga na Chadema, JB alikana na kusema;
 “mimi na siasa ni vitu tofauti, sijawahi kufuatwa na mtu wa Chadema na 
angalau kungekuwa na dalili basi uniulize, hiyo ni taarifa ya 
kutengenezwa na wewe ndiye uliyetengeneza hakuna aliyekupa ni udaku 
huo.”
Kwa
 upande wa Mkoloni, alisema hajawahi kufuatwa wala kushawishiwa kujiunga
 na chama chochote, isipokuwa ni mwanachama wa muda mrefu wa Chadema na 
amekuwa akishiriki kampeni, mikutano ya hadhara na matukio yote ya 
uhamasishaji ndani ya chama hicho. 
Alisema
 kuhusu kuombwa kuwania jimbo mkoani Tanga kwa tiketi ya chama hicho, 
alisema hajawahi kuombwa na chama hicho kufanya hivyo.
“Sijawahi
 kuombwa nigombee jimbo, na kuhusu nia ya kugombea, ni mapema mno 
kuzungumzia suala hilo sasa na hata kanuni za chama changu haziruhusu 
labda uniulize swali hilo mwakani naweza kuwa na jibu,” alisema Mkoloni.
Kwa
 upande wake, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, alikataa 
kuzungumzia taarifa hizo akidai yuko barabarani na masuala yote 
yanayohusu chama hicho aulizwe Msemaji wa chama hicho.
 
 
No comments:
Post a Comment