Pages

Translate

Tuesday 2 July 2013

MHUBIRI MMOJA ASHIKWA NA POLISI MKOANI IRINGA KWA TUHUMA ZA UTAPELI


Mhubiri Raia  wa Uganda Richard Mwangusi akiwa  chini ya  ulinzi wa  polisi  usiku  huu baada  ya kutuhumiwa kujipatia  fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia huduma ya M-PESA  


 Kamanda  wa  polisi  mkoa  wa Iringa (RPC) Ramadhan Mungi akitoa  kituo  cha  polisi mjini Iringa ambako mhubiri  huyu anashikiliwa na  jeshi la polisi kufuatia wananchi kulalamika kufanyiwa  vitendo vya kitapeli na mhubiri  huyo ,kamanda  Mungi amekuwa ni mmoja kati ya makamanda wa mfano  nchini kutoka na kufanya kazi usiku na mchana na kuwa  jirani  zaidi na askari  wake 
 Kikosi  cha kazi  cha  jeshi la polisi  mkoa  wa Iringa  wakiwa njeya  kituo  cha  polisi ambako mhubiri  huyo anashikiliwa usiku  huu kwa  tuhuma za kujipatia  fedha  kwa njia ya udanganyifu



KILIO  cha  wengi kuhusiana na vitendo vya utapeli  vinavyofanywa na baadhi ya  wahubiri ambao  wamekuwa  wakijitafutia  fedha  kupitia  injili hapa nchini ,kimeanza kusikilizwa  baada ya  jeshi la  polisi mkoa  wa Iringa  kumkamata  na kumtupa mahabusu  mhubiri  Richard Mwangusi ambae ni raia  wa nchini uganda   kwa  tuhuma za kujipatia  fedha kwa njia ya udanganyifu.

Mapema  leo  kupitia mitandao mbali mbali ya  kijamii  baadhi ya  wasamaria  wema  wameeleza kusikitishwa na  kito cha utapeli kinachofanywa na  mhubiri   huyo ambae  amekuwa akiishi katika nyumba moja ya kulala  wageni   ya  Wihanzi mjini  Iringa kuwa amekuwa akiwataka  watu mbali mbali  kutuma  pesa kwa  njia ya  M-PESA kuanzia kiasi cha kati ya  TSh 10,000 na kuendelea iwapo  wanahitaji  kupanga  muda wa kuongea na mhubiri  huyo kupitia  simu ya kiganjani .

Baadhi ya  wananchi  ambao  walitoa malalamiko yao leo  walidai  kuwa  mhubiri  huyo amekuwa akitumia namba ya simu ya Lodge ya  Wihanzi ambayo ni 0262700222 kwa kuwataka   watu  wenye matatizo  kupiga simu kwa namba hiyo na mara  baada ya  kupiga  simu mhudumu  ambaye  yupo  zamu amekuwa akimtaka  mtu aliyepiga   simu  kueleza shida yake na mara  baada ya kueleza iwapo anataka kuongea na mhubiri  huyo amekuwa akitaka  kurushiwa  kwanza kiasi cha Tsh 10,000 na kuendelea kwa namba ya mhubiri  huyo  ndipo  apewe huduma  anayotaka.

Mmoja kati ya watu ambao  wamepata  kulizwa na mhubiri huyo amedokeza  kuwa namba  za mhubiri  huyo amezipata  kupitia  kituo kimoja  cha  Radio  mjini Iringa  na kutokana na baadhi ya  watu  kutoa ushuhuda  kuwa  wamepona magonjwa sugu  ndio  sababu ya kuchukua namba yake  ili  kuweza  kuombewa  pia ila baada ya kuchukua namba  hiyo amejikuta akiishia  kuliwa  pesa  bila kupewa  huduma husika .

Pia  alisema  kila anapomtafuta mhubiri huyo kwa njia ya simu  ili kuombewa amekuwa akimtaka  kuongeza  pesa zaidi  ili  kuombewa hadi kupona jambo ambalo amekuwa akijiuliza kama kwa sasa injili ya biashara na kama  biashara  basi  ni  vema wahubiri kutoangaza  bei  kamili  ili mtu apata kununua kulingana na uwezo  wake.

Hata  hivyo kufuatia  kuwepo  kwa malamamiko hayo  mtandao  huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com na www.matukiodaima.com leo  ulipata  kupiga  simu  hiyo majira ya saa 10  jioni na kuomba  kuongea na mhubiri huyo ambapo simu   hiyo ilipokelewa na mhudumu ya  Wihanzi na  kudai kuwa kwa  wakati  huo  mhubiri anatoa  huduma kwa wateja wengine  hivyo ili  kuweza kupewa maelekezo ni vema kuwasiliana nae  kesho majira ya saa 4 asubuhi.

Kikosi  cha  jeshi  la polisi  mkoa  wa Iringa  chini ya kamanda Ramadhan Mungi na  watenda kazi  wengine akiwemo OCD ,ofisa  upelelezi  wilaya na  wengine  usiku  wa  leo  wameamua kuingia kazini na kupata kumtia nguvuni mhubiri  huyo ambae hata  hivyo maelezo yake bado  yanatia shaka.

Mhubiri  huyo anadai kuwa yeye ni Raia wa Uganda  na ni  mchungaji wa kanisa la I.M  na amepata  kuifanya  huduma kama  hii ya mjini Iringa katika nchi kama Zambia , Botswana na nyingine  nyingi na katika Tanzania amepata  kuzunguka maeneo mbali mbali japo kwa  sasa ana zaidi ya  miezi  miwili  katika mji  wa Iringa akiishi katika nyumbaya kulala  wageni ya Wihanzi .

Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi ameuthibitishia mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com  kukamatwa  kwa mhubiri  huyo na  kuwa bado  jeshi la polisi linaendelea  kufanya  uchunguzi wa kina ili kujua ukubwa wa madhara ambayo yamessababishwa na mhubiri  huyo kwa  wananchi na  kuwataka  wananchi ambao  wamepata  kuingizwa mjini na mtu  huyo kufika  kituo cha polisi na kutoa ushirikiano kabla ya  mtuhumiwa  kufikishwa mahakamani.

Mtandao  huu  unalipongeza  jeshi la polisi mkoa  wa Iringa kwa hatua  nzuri  iliyochukua  kuanza  kukabiliana na wimbi la wahubiri wasio  waaminifu ambao  wanaendelea  kuchukua  fedha  kidogo za madafu ambazo  wananchi  maskini  wanazo kwa kisingizio cha kuwasaidi kutatua matatizo  waliyonayo .


No comments:

Post a Comment